Subscribe:

Ads 468x60px

majambazi yadaiwa kuua mwangalizi wa shamba la Nyanza Road



MAUAJI
Mnamo tarehe 01.12.2012 majira ya saa 00.30 hrs huko Kampuni ya Nyanza road katika kijiji cha Nyatwali kata ya kunzugu, Tarafa ya Serengeti, Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara Mtu mmoja aitwaye ROHITA  GANTIRALALL  umri 20yrs, msimamizi wa shamba, aliuwawa kwa kupigwa risasi chini ya kidevu na majambazi ambao waliiba simu yake ya mkononi aina ya NOKIA. Majambazi hao waliokuwa takribani sita (6) kabla ya tukio hili walifyatua risasi hewani na kuvunja mlango wa nyumba kwa kutumia jiwe kubwa maarufu kama “Fatuma”. Walimshambulia PATEL VISHAL VINUBHAI na kumjeruhi usoni, kichwani, na mkono wa kulia kwa kutumia nondo kasha kumpora fedha taslimu Tshs. 500,000/= na US DOLLAR 600 pamoja na simu mbili, JAGINAL  NARAM Umri 23yrs, msimamizi wa shamba alijeruhiwa kichwani, usoni kwa kutumia npondo na kuporwa simu – Sum sung, VINUDI  RAMJI Umri 45yrs, msimamizi wa shamba alipigwa sehemu mbalimbali za mwili na kuporwa simu moja aina ya NOKIA. PATEL  VISHAL  VINUBAL alilazimishwa atoe fedha za mishahara nae kwa kujitetea aliwaeleza fedha ziko ofisini ambako ni kilometa moja toka wanapoishi. Wakiwa njiani kuelekea kwenye ofisi hiyo waliona Askari Polisi, wakamwachia na kutokomea gizani. Uchunguzi na ufuatiliaji wa kina umeanza kufanyika. Wito yeyote anayekusudia kusafirisha fedha kiwango kikubwa aombe ulinzi wa Polisi wenye  silaha.


ABSALOM  A. MWAKYOMA – S.A.C.P
KAMANDA WA POLISI ‘M’ MARA, MUSOMA