Subscribe:

Ads 468x60px

BARAZA LA KATIBA LA ASASI

 WASHIRIKI WA BARAZA LA KATIBA LA ASASI YENYE MALENGO YANAYOFANANA WILAYANI SERENGETI(SENGONET)CHINI YA UFADHILI WA THE FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY





TEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

 SERONERA LOJI
 TEMBO NDANI YA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI
HAPO AKIPATA CHAKULA KUTOKA KWENYE MATAWI YA MTI JUU

ABAKA


MWENYEKITI WA KITONGOJI ATUHUMIWA KUBAKA WATOTO WAWILI WA SHULE YA MSINGI,
Agosti 17,2013.
Serengeti;MWENYEKITI wa kitongoji cha Matumaini kijiji cha Miseke kata ya Manchira wilayani Serengeti Machaba Morumbe(53)(CCM)anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kubaka watoto wawili wa shule ya msingi.

Matukio hayo yanayodaiwa kutendeka kwa nyakati tofauti yamethibitishwa na polisi wilaya na Shirika la wasaidizi wa kisheria na Haki za Binadamu(Washehabise)na uongozi wa hospitali teule ya Nyerere ddh yanadaiwa kutokea agosti 9 na 13 katika kitongoji hicho mwaka huu.
                  
Akielezea matukio hayo  akiwa eneo la polisi Mwenyekiti wa shirika hilo Samwel Mewama alisema ,tukio la kwanza linadaiwa kutokea agosti 9 majira ya saa 10 jioni,ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la 5 mwenye umri wa miaka 12 shule ya msingi  Zakhia Meghji kijijini hapo.

“Akiwa machungani alimsihi mtoto huyo apeleke ng’ombe mtoni na kufika huko akambaka,huku akimtishia kutosema…hakusema kabisa licha ya kuwa na maumivu makali…lakini alipata ushujaa baada ya mwenzake kutendewa siku nyingine  naye akawaeleza wazazi wake kuhusu unyama wa kiongozi huyo”alisema Mewama.

Kujitokeza kwa mtoto huyo alipokelewa na dawati la jinsia la polisi Mugumu na kufunguliwa jalada Mug/dawati 148/2013 na kupelekwa hospitali teule ya Nyerere ddh kwa uchunguzi zaidi.

Katika tukio la pili mtuhumiwa huyo kwa mtindo ule ule anatuhumiwa kumbaka  mwanafunzi wa darasa la 3 mwenye umri wa miaka 10  Agosti 11 majira ya saa 11.00 jioni mwaka huu wakati akichunga ng’ombe na mbuzi.

Mtoto huyo alisema mtuhumiwa alimwambia eneo la mtoni kuna malisho mazuri ,walipofika ghafla akamkamata na kumvua nguo na kuanza kumwingilia huku amemziba mdomo,na kumsababishia majeraha sehemu za siri.

Baba mzazi wa mtoto huyo jina tunalo alibaini hali hiyo baada ya kumwona mwanae akiwa katika hali isiyo ya kawaida,na alipoulizwa alibainisha unyama aliotendewa na kiongozi huyo na kuchunguza walibaini amechanika vibaya na kumpeleka hospitali kupitia polisi na kufunguliwa jalada Mug/dawati 147/2013.

Mganga wa zamu hospitalini hapo aliyejitambulisha kwa jina moja la  Nyanokwe aliyempokea na kumfanyia uchunguzi mtoto huyo amebaini kuchanika vibaya sehemu za siri na pia katika nyonga zake.

Mganga mkuu wa hospitali teule ya Nyerere ddh,Dk,Kelvin Mwasha amethibitisha kumpokea mtoto huyo kuwa wamemlaza wakiendelea na matibabu,hata hivyo mtuhumiwa ametoroka kijijini baada ya kusikia anasakwa.

Mwisho.

JINSI MWL ALIVYOMFANYIA UKATILI MWANAE

MAJERAHA ALIYOPATA MTOTO HUYO BAADA YA KUPIGWA NA BABA YAKE AMBAYE NU MWL SHULE YA MSINGI MOROTONGA WILAYANI SERENGETI ,KISHA KUMWEKEA PILIPILI NA  KUMLAZIMISHA KULA KINYESI

MWANAFUNZI ALIYEFANYIWA UKATILI NA BA A YAKE AMBAYE NI MWL

MTOTO ALIYEFANYIWA UKATILI NA BABA YAKE AMBAYE NI MWL SHULE YA MSINGI MOROTONGA WILAYANI SERENGETI AKIPATA MATIBABU

MWALIMU AMFANYIA UKATILI MWANAE,AMWEKEA PILIPILI KWENYE VIDONDA NA KUMLAZIMISHA KULA KINYESI CHAKE.



Serengeti:MWALIMU wa shule ya MsingI Morotonga wilayani Serengeti Karata Mugunda anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kumpiga kisha kumlazimisha kula kinyesi mwanae wa darasa la tano aliyedaiwa kujisaidia ndani kwa kuogopa kwenda nje sababu ya giza.
Tukio hilo ambalo limepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi linadaiwa kutokea agosti 13,2013 majira yausiku nyumbani kwa mwalimu huyo anayeishi shuleni,limethibitishwa na Mwalimu mkuu wa shule,polisi,wanaharakati na uongozi wa hospitali teule ya Nyerere ddh.
Akisimulia tukio hilo Mwenyekiti mtendaji wa shirika la Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu wilaya ya Serengeti(Washehabise)Samwel Mewama amesema ,mtoto huyo alisema aliogopa kwenda kujisaidia nje kutokana na giza nene na kujisaidia ndani ,hatua iliyopelekea kupata adhabu hiyo.
“Baba yake licha ya kutambua umri wake na nafasi a;liyonayo aliamua kumfanyia ukatili mwanae ikiwa ni kinyume cha sheria ya mtoto ya mwaka 2009… kumpiga bila huruma…matako yameharibiwa kwa viboko…kana kwamba haitoshi akachukua kitambaa na kuweka pilipili akamwekea…kisha akamlazimisha kula kinyesi chote na hakumpa huduma ya tiba”alisema.
Mewama alisema agosti 14 baba yake alimlazimisha kwenda shuleni ,hata hivyo hakuweza kukaa kutokana na vidonda matakoni”mwalimu wa darasa alipomuuliza na kueleza ,akaona hali aliyonayo akanipigia simu…nilikwenda kumchukua nikampeleka hospitali kupitia polisi”alibainisha.
Alisema kabla ya kwenda alimpigia simu baba yake lakini akamjibu aendelee na hatua anayoona inafaa ,na kulazimika kumfikisha hospitali Teule ya Nyerere ddh,hata hivyo alipokea simu ya vitisho kutoka kwa mwalimu huyo kuwa hana imani na chakula anachompa,hali iliyompelekea kumkabidhi Mwalimu mkuu wa shule hiyo aliyemtaja kwa jina la Mlay,ambaye naye alitishwa na mtuhumiwa.
Kutokana na vitisho hivyo Mwalimu Mlay alilazimika kutoa taarifa polisi na mtuhumiwa kukamatwa na polisi wamesema atafikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya taratibu kukamilika,huku mtoto akiwa amekabidhiwa ndugu zake kwa uangalizi zaidi.
Akiongea kwa wasiwasi mtoto huyo alisema ,hiyo ni mara ya tatu anapigwa na kuumizwa yeye na ndugu zake,na kuwa mama yao aliachika kutokana na vipigo na mama yao mdogo ndiye anawachongea yeye na ndugu zake watano ili wafukuzwe hapo.
Mmoja wa wanafunzi wa darasa la tano jina tunalo alisema tabia ya kupiga si kwa watoto wake tu hana wanafunzi darasani anawachapa bila utaratibu maalum,na walimu wanajua lakini wanaonekana kumwogopa kuwa ni mkorofi.
Baadhi ya walimu wamesema matukio ya kupiga watoto ni ya mara kwa mara lakini hilo ni kubwa zaidi nainapaswa sheria ichukue mkondo wake.
Mganga wa zamu Hooka Paul alisema majeraha hayo ni makubwa na anapaswa kupata kinga ya tetenasi kwa kuwa amechelewa kupata matibabu,na kisaikolojia mtoto huyo ameathirika kwa kuwa anastuka mara kwa mara.
Polisi wanaendelea na mahojiano kwa walimu wengine na wamesema utaratibu ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Mwisho.

CHADEMA WAKUSANYA MAONI YA RASIMU

 CHOPA YA CHADEMA ILIYOMBEBA KATIBU MKUU WA CHADEMA DK.WILBROAD SLAA  IKIWAAMBAA KIWANJA CHA KILOMBELO JIJINI ARUSHA KWA AJILI YA BARAZA LA KATIBA .
 CHOPA LA CHADEMA
 DR WILBROAD SLAA AKIWASILI UWANJA WA KILOMBELO JIJINI ARUSHA
BAADHI YA WANANCHI WAKIFUATILIA MKUTANO WA BARAZA LA KATIKA KIWANJA CHA KILOMBELO JIJINI ARUSHA

UKUKWAJI HAKI ZA BINADAMU


WALIMU WALALAMIKIWA KWA UBAGUZI WA UKABILA.
Serengeti:UBAGUZI wa kikabila,ukiukwaji wa Haki za Binadamu unadaiwa kutawala zoezi la kuhamisha wafugaji katika kijiji cha Nyamokhobiti kata ya Maji moto  Tarafa ya Ngoreme wilayani Serengeti,umevuka mipaka hadi shuleni .
Ubaguzi huo umeanza kuleta madhara kufuatia baadhi ya watoto wa wafugaji wa jamii ya Wakenye kutoka wilaya ya Butiama waliokuwa wanasoma Isereserekutokwenda shule kwa madai ya ubaguzi kutoka kwa walimu wa shule hiyo ambao wengi ni kabila la Wangoreme wazawa wa kijiji hicho.
Alex Mang’era(68)mfugaji alisema aliingia kijijini hapo mwaka 2003 kwa kuridhiwa na serikali ya kijiji na mkutano mkuu,na wanae watatu wanaosoma hapo kwa sasa hawaendi shule kutokana na ubaguzi ulio ndani ya jamii na walimu wa shule.
“Wanangu Kadogo Alex wa darasa la 6,Neema na Habibu wa darasa 3 hawaendi shule…wanabaguliwa na wanafunzi,jamii nahadi walimu kuwa ni Wakenye warudi kwao Butiama ….wamezaliwa na kuanzia shule hapa..mimi nimekaa miaka 10…nimepiga kura hapa…ubaguzi huu ni mbaya sana”alisema kwa masikitiko.
Alisema shule hiyo yenye walimu 7 watano ni wazawa wakijijini hapo na wanaishi kwenye miji yao ,badala ya kutekeleza majukumu yao wamegeuka kuwa sehemu ya jamii,wanashiriki vikao vya kimila ritongo na matokeo yake wanapeleka ubaguzi shuleni.
 Moroni Nyancharu(30)wa kitongoji Getenga kijijini hapo  anasema katika zoezi hilo mtoto wake  Bhoke Mroni wa darasa la kwanza haendi shule kwa kuhofia usalama wake,na kubaguliwa .
”Walimu wanatutukana sisi kuwa Watoto wa Wakenye ni wajinga hamjui kusoma…na wanafunzi nao wanatutukana kuwa sisi ni watu wa kuja…njiani mkipita jamii inatuzomea kuwa Makenye mrudi wilayani kwenu…hatuna raha shuleni”anasema mwanafunzi wa darasa la tatu jina tunalo.
Ofisa elimu akiri.
Ofisa elimu ufundi wilaya Christopher Mossi alikiri kuwa walimu karibu wote ni wazawa wa kijijini hicho,”ni kweli ni hapo…kwa malalamiko hayo tunafuatilia kwa kuwa yanalenga kuwanyima elimu hao watoto”alisema.
Mwenyekiti  wa serikali ya kijiji cha Iseresere Mosi Ng’ombe alipotakiwa kujibu tuhuma za kuwapokea wafugaji na sasa amewakana,alisema yeye hawezi kulizungumzia hilo labda aulizwe mkuu wa mkoa ama Dc.
Agizo la RC  latekelezwa na wazee wa mila badala yaSerikali ya kijiji.
Katika hali isiyo ya kawaida  ambayo imechangia ukiukwaji wa Haki za Binadamu agizo la Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tupa la kuhamisha  wafugaji haramu linatekelezwa na wazee wa mila chombo kisicho cha kiserikali.
Uamzi huo umelalamikiwa na makundi ya wanaharakati akiwemo Mbunge wa jimbo hilo Dk,Stephen Kebwe ambaye aliiambia blog hii  kuwa chombo hicho hushughulikiwa masuala ya ulinzi na usalama ,lakini hakina nguvu kwa maagizo ya kiserikali kama hayo.
“Zoezi lilikuwa na nia njema lakini njia zilizotumika si sahihi…huwezi tumia ritongo kwa agizo la serikali wakati inavyombo vyake…uonevu ,ukiukwaji haki utatendeka…pia kuna udhaifu katika zoezi hilo maana hakuna waraka wenye maelekezo alioutoa kwa watekelezaji,hii inaweza kuleta vurugu”alisema Mbunge.
Alikwenda mbali zaidi na kudai ameishamwambia mkuu wa mkoa ajaribu kuangalia vema suala hilo kwa kuwa tafsri ya mhamiaji haramu ijulikane,na wabainishwe na wananchi ,kwa kuwa watu walipokea kwa utaratibu ,wameishi miaka mingi,wanamazao,wana vitu kuwaondoa kwa kutumia ritongo hawatapata muda wa kuweka sawa mali zao,wala kusikilizwa.
Wazee wa mila wafunga zizi kwa dawa.
Mbali na malalamiko ya ubaguzi na ukiukwaji haki za binadamu,wazee wa mila wamelazimika kufunga zizi la ng’ombe wa Simion Maitari Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nyamokhobiti kijiji jilani kwa kuweka matawi ya miti ambayo inaaminika kuwa wamezindika ng’ombe wakirudi humo watakufa,na wao ndio wenye uwezo wa kuzindua tego hilo.
 Majeruhi.
Wakati Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara  Ferdinand Mtui na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Iseresere Mosi Ng’ombe kudai kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa wakati wa zoezi la kuwafukuza wafugaji,Mwananchi  imebaini watu wawili kujeruhiwa kwa kupigwa na kukatwa kwa sime.
Polisi kituo cha Maji moto kimekiri kuwapokea majeruhi hao na kuwapa Pf 3 agosti 5 ,mwaka huu iliyosainiwa ditektivu Mohammed ambayo nakala yake tumeiona ,pia hati ya kuwakamata watuhumiwa George Rabani na Mohi Morigo kwa kosa kujeruhi Ref No MAJ/RB/281/2013 hata hivyo hawajakamatwa
Wanaharakati.
Mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu (Washehabise)Samwel Mewama anasema zoezi hilo limekiuka haki za binadamu,kwa kuwa linavunja katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977.
“Ibara ya 17,uhuru wa mtu kwenda atakako,sheria ya 1984  na ibara ya 24 haki ya kumiliki mali,kwa kitendo hiki kilichofanyika ni uvunjaji wa katiba,watu wamekosa haki ,watoto wanashida ya chakula,wameacha mazao,chombo kinachotumika kutekeleza si cha kisheria,tutahakikisha haki inatendeka,maana mhamiaji haramu anawezaje kuchagua kiongozi yeye akawa halali”anasema.
Rc
Mkuu wa mkoa wa Mara John Tupa anasema waraka wake amesambaza kwa wakuu wa wilaya,na kuwa mwisho wa zoezi hilo ni agosti 16 mwaka huu,hata hivyo waraka huo wakuu wa wilaya hawajausambaza kwa viongozi wa vijiji .
Mwisho.


JELA MIAKA MINANE KWA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO


ALIYEKUTWA NA MENO YA TEMBO AHUKUMIWA MIAKA 8 JELA.
Serengeti:MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi mfawidhi wa wilaya ya Serengeti imemhukumu  Idd Abdallah Adamu (39 ) mkazi wa Nyakato Mwanza miaka 8 jela kwa kosa la kupatikana na  meno ya tembo  kilo 46 yenye thamani ya sh, 26,250,000 .
Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 59/2011 washitakiwa wengine kwenye shitaka hilo   Lameck James (29) mkazi wa Sirari, Kasika John(46) mkazi wa Ushashi Bunda na Mwita John(44) mkazi wa kijiji cha Kibeyo wilaya ya  Serengeti  wameachiwa huru kutokana na udhaifu wa polisi kushindwa kuwasilisha fedha sh.3,835,000 walizokutwa nazo  mahakamani kama ushahidi  siku ya tukio.
Hakimu Amon Kahimba wa mahakama hiyo alisema,mshitakiwa Adamu amekumbwa na adhabu kufuatia ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo kuanzia maelezo ya polisi ,mahakamani na mashahidi kuwa vipande vinne vya meno ya tembo vilikutwa ndani ya chumba alichokuwa amelala nyumba ya wageni ya Leopard.
Na kuwa alikiri kununua meno hayo,kwa washitakiwa  wawili kwa sh,2,400,000 na washitakiwa Lameck James na Kasika John walikiri kununua vipande  hivyo vya meno kwa mshitakiwa wanne Mwita John kwa sh,200,000,na fedha walizokutwa nazo hotelini sh,3,835,000 hazikuwasilishwa mahakamani kama kielelezo licha ya washitakiwa kuzidai.
“Kutokana na maelezo yote ya ushahidi na washitakiwa ,mahakama inamhukumu Idd Abdallah miaka minane jela…na wengine wanaachiwa huru kutokana na uzembe wa polisi..wote hawa wangehukumiwa kama mpelelezi wa kesi na aliyekuwa Oc Cid wilayani hapo kwa sasa Mkuu wa Operesheni Mkoani Arusha Paul Ngonyani aliyewakamata,kuwapekua,lakini hakufika kutoa ushahidi mahakamani licha ya kuitwa na wala fedha alizowakutana nazo hazikuwasilishwa kama ushahidi”alisema.
Alikwenda mbali hakimu huyo na kudai kuwa kosa la kujihusisha na biashara ya meno ya tembo mazingira yake  wangekutwa na mzigo au pesa,lakini wao walikutwa na pesa katika nyumba ya kulala wageni ya Galaxy Motel ,lakini hazikuwasilishwa mahakamani.
Aliomba jeshi la polisi nchini liwachukulia hatua kali Paulo Ngonyani ,kwa kushindwa kufika kutoa ushahidi kwenye kesi hiyo licha ya kuitwa mara tatu,na mpelelezi wa shitaka hilo Ditektivu Sajenti Yona,kwa  kutowasilisha fedha za washitakiwa ambazo wamezidai na mahakama ikaagiza ziwasilishwe mahakamani..
Mapema mwendesha mashitaka inspekta msaidizi wa Polisi Abdallah Idd aliitaka mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili liwe fundisho kwa wengine kwa kuwa makosa ya uhujumu uchumi yamekithiri hapa nchini.
Katika utetezi wake Adamu aliomba ahurumiwe kwa kuwa ni kosa lake la kwanza ,ana watoto 5,mke na watu wanaomtegemea.
Februari 18,2013 katika mahakama hiyo mshitakiwa huyo aliyehukumiwa aliyekuwa akijifanya Mmachinga anayetembeza vyombo kutoka Mwanza  aliachiwa huru na mahakama hiyo katika kesi 184/2011 ya uhujumu uchumi baada ya kukamatwa katika nyumba ya kulala wageni ya Silent Inn mjini Mugumu wakiwa na meno mawili ya tembo.
Katika kesi hiyo ilimhusisha mmiliki wa nyumba hiyo Julius Mwita Marwa(43)waliachiwa na Hakimu Amon Kahimba kwa kutumia kifungu cha sheria namba 235 cha mwenendo wa makosa ya jinai kilichorekebishwa mwaka 2002 kwa madai kuwa upande wa mashitaka ulikuwa dhaifu.
Mwisho.


MADHIRA YA WAFUGAJI SERENGETI


 WAFUGAJI JAMII YA WAKENYE WA KIJIJI CHA ISERESERE KATA YA MAJI MOTO WILAYANI SERENGETI WAMEFUKUZWA KIJIJINI HAPO KWA MADAI KUWA NI WAHAMIAJI HARAMU KUTOKA WILAYA YA BUTIAMA
 BAADHI YA WANAHARAKATI KUTOKA SHIRIKA LA WASAIDIZI WA KISHERIA NA HAKI ZA BINADAMU WILAYANI SERENGETI WAKIWA NA BAADHI YA WAFUGAJI KATIKA MAENEO WALIYOFUKUZWA
 FAMILIA HIYO NI YA MWENYEKITI WA SERIKALI YA KIJIJI CHA NYAMOKHOBITI KATA YA MAJI MOTO KIJIJI JILANI NA ISERESERE NAYO IMEFUKUZWA KAMA WAHAMIAJI HARAMU
MZOGA WA NG'OMBE ALIYEKUFA BAADA YA KUPIGWA NA WANANCHI WAKATI WA ZOEZI LA KUHAMISHWA

UKATILI WAFUGAJI

MMOJA WA WAFUGAJI WA KIJIJI CHA ISERSERE KATA YA MACHOCHWE WILAYANI SERENGETI AKIWA NA FAMILIA YAKE WAKITAFAKARI NAMNA YA MAISHA KUFUATIA KUFUKUZWA KIJIJINI HAPO KWA MADAI KUWA NI WAHAMIAJI HARAMU KUTOKA WILAYA YA BUTIAMA INGAWA WAMEISHI HAPO KWA MIAKA 10 NA WALIPITIA MIKUTANO YA SERIKALIZA VIJIJI NA MKUTANO MKUU WAKAKUBALIWA.LAKINI KWA AGIZO LA RC MARA WAMEFUKUZWA NA MIFUGO YAO.


HAPO MAISHA YANAKWENDA KAMA INAVYOONEKANA NDIVYO ILIVYO KWA WAFUGAJI WA KABILA LA WAKENYE KUTOKA WILAYA YA BUTIAMA WALIOKUWA WAKIISHI KIJIJINI HAPO BAADA YA KUKUBALIWA SASA WANAITWA WAHAMIAJI HARAMU SAWA NA WALE WANAOTOKA NJE YA NCHI.

Add caption
MASAKA MKAZI WA KIJIJI CHA NYAMOKHOBITI KATA YA MAJIMOTO NI MIONGONI MWA WALIOPIGWA NA MKUTANO WA MILA(RITONGO)WA KIJIJI CHA ISERESERE KATA HIYO KUWA NI MHAMIAJI HARAMU ,LICHA YA KUPIGWA NG.OMBE 29 HAZIJULIKANI ZILIPO.
HAPO NI OFISI YA SERIKALI YA KIJIJI CHA NYAMOKHOBITI KATA YA MAJIMOTO WILAYNI SERENGETI
NG'OMBE HUYO ALIACHWA BAADA YA KUPIGWA NA WANARITONGO WAKATI WA KUHAMISHA WAFUGAJI ,ALIBAKI BAADA YA KUSHINDWA KUTEMBEA,WAPO WALIOKUFA KWA KIPIGO NA KUZAMISHWA MTO MARA,KUPOTEA.
NYUMBA HIYO ILIEZULIWA NA WANANCHI WALIOKUWA WAKITEKELEZA AGIZO LA MKUU WA MKOA JOHN TUPA,HATA HIVYO HAWANA WARAKA WA MAELEKEZO .FAMILIA ILIPOTEZA NG'OMBE WAKATI WA ZOEZI HILO LINALODAIWA KUKIUKA HAKI ZA BINADAMU.

BODABODA

 MAKAMANDA WA CHAMA CHA WAEBDESHA PIKIPIKI(BODA BODA )WILAYANI SERENGETI WAKIWA WAMEMDHIBITINMWENZAO BAADA YA KUKIUKA MAADILI YA WALIYOJIWEKEA WAKATI WANAPOKUWA KWENYE MIKUTANO YAO.
 CHINI YA ULINZI KWA KUKIUKA MAADILI
 UTII BILA SHURUTI KWA BODA BODA
BODA CHINI YA ULINZI

TEMBO ALIVYOMUUA FARU

                                                                                                                             



 

  
By Anthony Mayunga and Syriacus Buguzi The Citizen Reporters

In Summary
The bizarre incident occurred at Nyabikwabe area in Natta ward on Thursday evening and has compelled conservationists and game experts to scratch their heads hard, in attempts to find appropriate answers to the killing.
Serengeti/Dar es Salaam. In what has puzzled game officers and authorities, an elephant reportedly killed one of two heavily protected rhinos at Makunduzi village in a reserve run by Singita Grumeti Fund.
The bizarre incident occurred at Nyabikwabe area in Natta ward on Thursday evening and has compelled conservationists and game experts to scratch their heads hard, in attempts to find appropriate answers to the killing.
The incident was confirmed by both the wildlife director, Prof Alexander Songorwa and the management of Singita Grumeti reserve.
Prof Songorwa said the rhino called Limpopo, was one of the two remaining out of the five brought to the reserve from South Africa in 2007. The animals were famously referred to as ‘Kikwete Rhinos’ in recognition to efforts by President Jakaya Kikwete to have the rare white Rhinos bred in the country.
President Kikwete personally received the huge animals that are among major tourist attractions when they were first flown in from South Africa. Three of them vanished in circumstances that include killings by brazen poachers. The President ordered a manhunt for the perpetrators, in the wake of which one Thomas Nchagwa was arrested and arraigned in court in 2010.
He was charged under economic sabotage laws, but the suspect and those who had bailed him subsequently disappeared.
The rhino killed on Thursday was male and the youngest. “It was aged 11 when it met its sudden demise,” said Prof Songorwa.
He said the rhino, which was well protected in a fenced enclosure, was furious when it spotted the elephant that had entered its habitat by tearing through the fence.
“It charged at the elephant to chase it out, igniting what looked like a furious fight between the two animals. They fought for some time before the rhino was overpowered and lost the fight,” he explained.
He said one of the elephant tusks pierced the rhino’s underbelly while the second one sank deep into the rhino’s hump, killing it instantly. “It has taught us a big lesson,” he said, noting that poaching was the only threat to such rare animals until that fateful day.
In reaction to inquiries by The Citizen on Sunday on the security of the animals in the reserves, Prof Songorwa explained that the incident happened so suddenly that it was not easy for the wardens to intervene during the fight.
He said no one expected that the elephant could trespass into the rhino’s enclosure at that time. It is reported that the fighting occurred in the twilight hours and the wardens’ attention was drawn when the rhino was already dead.
He said following the death of the male rhino, efforts were underway to find a replacement since the rhinos customarily live in pairs.
The management of the company declined to comment but game warders confessed that intrusion by elephants into the area had never occurred previously.
Rare phenomenon
In a separate interview, an expert in tourism management said such incidences usually happen but the cases were very rare.
‘’Fighting usually occurs when the animals struggle to win feeding grounds. Both the elephant and rhino are browsers; they feed on green leaves on top of trees. This leaves a competing ground for them,’’ said Mr Asantael Melita, Ngorongoro’s principal tourism officer.
Mr Malita explained that one animal was likely to kill on its rival, depending on which one is older or bigger in size, but swiftly pointed out that such behaviour was usually abnormal amongst the animals.
‘’An elephant can knock a rhino over and trample it by driving a tusk through its chest. If the elephant is older, it’s likely to kill the rhino,’’ he further explained.

TEMBO AUA FARU

 MZOGA WA FARU DUME AITWAYE LIMPOPO(11)ALIYEUAWA AGOSTI 1 MWAKA HUU NA TEMBO DUME ALIYEVUNJA UZIO WALIMOHIFADHIWA KATIKA ENEO LA NYABIKWABE KIJIJI CHA MAKUNDUSI KATA YA NATTA WILAYANI SERENGETI,FARU HUYO NI KATI YA WAWILI WALIOLETWA MWAKA 2007 NA KAMPUNI YA SINGITA GRUMETI RESERVES TOKA AFRIKA KUSINI.
 KUUAWA KWA FARU HUYO KUMETHIBITISHWA NA MKURUGENZI WA WANYAMA PORI TANZANIA PROFESA ALEXANDRE SONGORWA NA KUDAI KUWA WALIKUWA KWENYE ENEO MAALUM KAMA MRADI WA KAMPUNI HIYO,NA KUWA TEMBO DUME ALIPOINGIA KATIKA HIMAYA YA FARU HAO KULIPELEKEA FARU KUCHACHAMAA NA KUMFUKUZA NDIPO AKAMCHOMA KWA JINO LAKE SEHEMU YA MOYO NA KUMBANA SEHEMU YA NUNDU NA KUFA PAPO HAPO.
MBALI NA UJANGILI WA WANYAMA HAO PIA TEMBO NA FARU NI WANYAMA WASIOPATANA NA HUISHI KWA KUKWEPANA.

WATHAILAND WAFURAHIA UTALII SERENGETI

 NIKIWA NA MIHAYO NA MUSSA KIKAZI ZAIDI WAKATI WA ZIARA YA WAZIRI MKUU WA THAILAND YINGLUCK SHIWANATRA
 MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPA AKIWA NA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII KHAMISI KAGASHEKI,WENGINE NI MKURUGENZI WA TANAPA ALLAN KIJAZI
 MKUU WA MKOA WA MARAJOHN TUPA,MKURUGENZI WA WANYAMA PORI TANZANIA PROFESA ALEXANDRE SONGORWA NA BAADHI YA WATU WALIOAMBATANA NA WAZIRI MKUU WA THAILAND UWANJA WA NDEGE SERONERA
 CHAKULA HIKI KILITUMIKA KWA WAGENI WA THAILAND NA WATANZANIA HOTEL YA FOUR SESSION SAFARI LTD
WAZIRI KAGASHEKI,KIJAZI NA MMOJA WA WAGENI WALIOKUWEPO ZIARA YA SHINAWATRA

 Utalii wamkuna Waziri Mkuu wa Thailand
Kwa ufupi
Alisema kutokana na ziara hiyo, Tanzania na Thailand zimekubaliana na kutiliana saini mkataba wa miaka mitatu wa ushirikiano katika kulinda, kuendeleza na kukomesha biashara haramu ya wanyamapori.
Dar es Salaam. Ziara ya siku tatu ya Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra imemvutia kiongozi huyo na kuahidi kufanya ziara binafsi katika mbuga za wanyama akiambatana na familia yake.
Akizungumza wakati wa kumuaga waziri huyo aliyeondoka nchini jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki, alisema ziara ya Shinawatra imekuwa ya mafanikio makubwa kwa taifa.
Alisema kiongozi huyo ameahidi kurudi nchini wakati wowote akipata nafasi.
“Amesema anakwenda lakini atarudi katika ziara ya kibinafsi yeye na mume wake, mtoto wake na ndugu zake na tumemwambia akiwa tayari atufahamishe,” alisema Balozo Kagasheki.
Alisema kutokana na ziara hiyo, Tanzania na Thailand zimekubaliana na kutiliana saini mkataba wa miaka mitatu wa ushirikiano katika kulinda, kuendeleza na kukomesha biashara haramu ya wanyamapori.
Mkataba huo ulisainiwa na Balozi Kagasheki na Naibu Waziri Mkuu wa Thailand Plodprasop Suraswad, aliyeambatana na Shinawatra.
Akizungumzia manufaa ya mkataba huo, Waziri Kagasheki alisema utasaidia taifa kuongeza mapato kupitia sekta ya maliasili kwa kuongeza watalii.

MKATABA WA ULINZI WA MALIASILI WASAINIWA


 
 TANZANIAYATILIANASAINI NA THAILAND MKATABA WA KULINDA  MALIASILI NA KUKOMESHA UJANGILI,
Julai 31,2013.
Serengeti:SERIKALI ya Tanzania imetiliana saini mkataba wa maelewano  wa miaka mitatu wa ushirikiano wa kulinda na kuendeleza maliasili na Utalii na Jamhuri ya Kifalme ya watu wa Thailand.

Mkataba huo umesainiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii balozi Khamisi Kagasheki kwa niaba ya serikali ya Tanzania  na Naibu Waziri Mkuu wa Thailand Plodprasop Suraswad  aliyeambatana na Waziri Mkuu wa Thailand Yingluck Shinawatra kwenye ukumbi wa  Four Session Safari Hotel Ltd  iliyoko hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Akizungumzia manufaa ya mkataba huo Waziri Kagasheki amesema hatua hiyo itasaidia taifa kuongeza mapato kupitia sekta ya Maliasili kwa kuongeza watalii kutoka milioni moja kwa sasa kama ilivyo kwa nchi ya Thailand pamoja na raslimali chache wanapata watalii hadi milioni 22 kwa mwaka.

“Tunataka mchango wa maliasili  katika pato la Taifa utoke asilimia 17  …hali hiyo ikienda sambamba na kuongeza pato la wananchi….maana Thailand kupitia utalii pato la Mwananchi ni dola 5,000 kwa mwaka …na ndio mpango  wa taifa wa 20-25”alisema.

Waziri wa uwezeshaji na Uwekezaji  Dk,Mary Nagu amesema mkataba huo unafungua fursa za uwekezaji ambao utainua pato la taifa katika sekta ya utalii,pia kilimo na madini.

“Tanzania tuna fursa nyingi lakini hatujafanya vizuri kwa ajili ya kujipatia mapato….tuna maliasili nzuri na kubwa tunawazidi Kenya …lakini wao wana vitanda 11,000 wakati sisi tunavitanda 6,000 sasa tunakusudia kukuza kwa kasi sekta hii kwa kushirikiana na nchi ambazo zinamwelekeo na zinazofanya vizuri”alisema.

Alisema ili kuhakikisha watanzania wananufaika na uwekezaji kama huo ,kwa upande wa madini serikali haitauza madini ghafi bali kuyatengeneza na kuwa vito ili yaongezewe thamani ,na watanzania wakipewa fursa ya kwanza kwa kuangalia watakavyonufaika.

Alisema ziara hiyo imekuja siku chache baada ya viongozi wa mataifa ya China,Marekani na Uingereza kutiliana mikataba ya kimaendeleo na taifa la Tanzania..

Mkurugenzi wa Wanyamapori Tanzania  Profesa Alexander Songorwa alisema ,wanategemea kuimarisha utalii na kupunguza tatizo la ujangili kwa kuwa nchi hizo zote zitahusika katika masuala ya ulinzi na usimamizi.

“Soko la meno ya Tembo kutoka Tanzania ni kubwa nchini Thailand na China …kwa mkataba huu sasa nao watashiriki kukabiliana na vitendo hivyo vya uharifu,na hiyo nafasi itatusaidia sisi kudhibiti hali hiyo…maana ujangili wa tembo ni changamoto kubwa kwa uhifadhi hapa Tanzania”alisema.

Mapema Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya Taifa ya Serengeti William Mwakilema akitoa taarifa ya hifadhi hiyo alisema mbali na kuwa kivutio kikubwa kwa wageni,bali wanakabiliwa nanchangamoto za askari wachache wa ulinzi wa wanyama pori,nyumba za askari ,maji ,barabara za ndani na jamii zinazowazunguka .

Kwa upande wa falme za Thailand walisema ,Raslimali za Tanzania zikilindwa na kusimamiwa vema zitasaidia kuinua uchumi kwa kasi kubwa,kwa kuwa wana vitu ambavyo havipo katika maeneo mengine,lakini hawajafanya vizuri.

Mwisho.

NAIBU WAZIRI MKUU WA THAILAND PLODPRASOP SURASWAD AKITIA SAINI YA MAKUBALIANO YA ULINZI WA MALIASILI NA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII HAMISI KAGASHEKI UKUMBI WA HOTELI YA FOUR SESSION SAFARI LTD ILIOKO HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI
 SAINI YA MAKUBALIANO
 WAZIRI MKUU WA THAILAND YINGLUCK SHANAWATRA AKIANGALIA MCHORO WA MZUNGUKO WA NYUMBU
WANAKABIDHIANA MKATABA WA MAELEWANO

TEMBELEA www.antonymayunga.blogspot.com

 UWANJA WA NDEGE WA SERONERA KIKAZI WAKATI TUKIMSUBIRI WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA KIFALME YA THAILAND SHINAWATRA
 HATKUWA PEKEE YETU HAWA NI BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI NA MAAFISA WA USALAMA WA THAILAND WAKIWA UWANJA WA NDEGE SERONERA KUMSAUBIRI WAZIRI MKUU
 WAZIRI WA UWEZESHAJI NA UWEKEZAJI DK.MARY NAGU AKIHOJIWA NA WAANDISHI WA HABARI KATIKA HOTEL YA FOUR SESSION SAFARI LTD,ILIYOKO HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI
 MAZINGIRA YA HOTELI YA FOUR SESSION SAFARI LTD YANAPENDEZA
 CHAKULA HII UNAPATA HOTELINI HAPO
 WAKATI MWINGINE WAHITAJI KUPUMZIKA NA KUFURAHIA UUAMBAJI WA MUNGU
 KAMA ILIVYO HAPO
WAKATI MWINGINE HUACHI KAMERA KAMA ILIVYO KWA ASKARI KWA KUWA MATUKIO MENGINE NI YA KUSTUKIZA HASA UWAPO MAENEO YA HIFADHINI