Subscribe:

Ads 468x60px

MSIMU WA NYUMBU KUZALIANA KWAWAVUTA WATALII NA WATAFITI WENGI HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI.

NYUMBU KATIKA MAENEO YA NDUTU HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI AMBAKO WANAENDELEA KUZALIANA



kundi la nyati

MSIMU WA NYUMBU KUZALIANA KWAWAVUTA WATALII NA WATAFITI WENGI HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI.

WATALII na watafiti 16,500 wa masuala ya wanyamapori kutoka mataifa mbalimbali duniani wamefurika katika Hifadhi ya Taifa Serengeti, kushuhudia tukio la aina yake la nyumbu zaidi ya 8,000 kuzaliwa kwa siku, katika kipindi cha wiki sita.

Nyumbu hawa, wameanza kuzaliwa mapema mwezi huu na baada ya wiki sita wanatarajiwa kuzaliwa 500,000 lakini kati ya hao, karibu nusu yao, huliwa na wanyama wengine, wakiwapo simba, fisi na mamba kabla ya kukua huku wengine wakifa kutokana na kupotezana na wazazi wao.

Hifadhi hiyo yenye zaidi ya nyumbu 1.5 milioni, ina jumla ya simba 3,000 na fisi 7,500 ambao ndio walaji wakubwa wa nyama katika hifadhi hiyo.

Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya watalii hao, toka nchini Ubelgiji, Uingereza, Marekani na Ufaransa, walieleza kuvutiwa na tukio hilo, waliloliita kama “The Great Migration” .

Robert Joseph Raia wa Ubelgiji alisema, wamevutiwa sana na tukio la idadi kubwa ya nyumbu kuzaa kwa wakati mmoja.

“Ni tukio la ajabu duniani kila siku hapa nyumbu zaidi ya 8,000 wanazaliwa na watoto baada tu ya kuzaliwa dakika tano hadi nne,wanatembea”anasema.

Nicky Johnson raia wa Ufaransa, anaeleza kuwa, huu ni mwaka wake wa kwanza kufika Tanzania na Serengeti na alikuwa akiona kwenye mikanda ya video tukio la nyumbu zaidi ya 1.5 milioni kuhama na baadaye wakiwa Serengeti wanavyozaa na kuendelea na safari yao.
“Hili ni tukio zuri, sikuwahi kuliona sehemu yoyote duniani,hili ni jambo la ajabu , Tanzania mnapaswa kujivunia kwa tukio hili”alisema Jonson.

Mkuu wa Idara ya Utalii wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Godson Kimaro alisema tofauti na miaka ya nyuma mwaka huu kuanzia Februari Mosi hadi Februari 24, jumla ya watalii 10,621 toka nje ya nchi wamefika Serengeti kushuhudia nyumbu wakizaliwa.

Kimaro alisema katika kipindi hiki pia kuna Watanzania 5,815 wametembelea hifadhi, ikiwa pia ni ongezeko la zaidi ya asilimia 50 katika kipindi kingine.

Naye Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) Pascal Shelutete alisema Tanapa kuanzia mwaka jana, imeanza kulitangaza kimataifa tukio la nyumbu kuingia nchini, kuzaliana na kuondoka ili kuwavutia watalii.
Shelutete alitoa mwito kufika kuona maajabu hayo.
Hifadhi hiyo yenye zaidi ya nyumbu 1.5 milioni, ina jumla ya simba 3,000 na fisi 7,500 ambao ndio walaji wakubwa wa nyama katika hifadhi hiyo.
Mwisho.


kozi kwa waandishi wa habari za biashara


logo1
SAUTEMB1












































































































         





























Investigative Business Environment Journalism Course

St. Augustine University of Tanzania – Mwanza






































SAUT in collaboration with BEST-AC and ANSAF is offering a course in Investigative Business Environment Journalism for young media professionals in Tanzania.  The course aims to equip journalists with the knowledge to successfully report on the business environment effectively and efficiently. At the end of this course, journalists should have the ability to use data with a compelling narrative to educate and impart essential business news to the readers. The course starts on the 11th March, 2013 and entails a total 4 weeks funded intensive training in Mwanza. The course will be followed by 8 weeks attachment period at or close to the students’ duty station (Non-funded)
During the attachment period, students will be mentored by senior media practitioners who will review the products their field assignments and provide guidance to nurture the skill of business reporting. The course aims to prepare journalists to competently report and successfully publish on the business environment. The course targets young media practitioners with at least 3 years’ experience and or demonstrated interest in reporting on agri- business, and the ease or unease of doing business in Tanzania.
Admission into the program will be competitive, where preference will be given to those that demonstrate aptitude and serious interest to excel in investigative business environment journalism. The criteria for selection will be based on the following minimum requirements:
·         Professional qualification in Journalism or Media Studies.
·         At least 3 years’ experience with print or broadcast media in Tanzania (print journalists are encouraged to apply)
·         At least 5 published print or broadcast content within the last 12 months should be submitted.
·          Media products previously published in agri-business, policy environment and budgeting processes (national and local) will have an advantage.
To apply for this course, kindly send an Email to SAUT, Attaching the following Information:
·         A compelling 2 pages motivation essay
·           Brief Curriculum Vitae with details three referees and their contact information.
·         Scanned copies of your published work and copy of radio material ( or a web- link)
Make sure that all materials submitted are original products and that your ownership or role (when produced in team work) is sufficiently clear.
Note:
The nature of this course is competitive and will require dedicated focus from successful applicants throughout the course. There will be attachments available after the one month course at SAUT that will require motivation letters to selected partners from students. Only serious applicants are invited to apply.
Application deadline 25th February, 2013.
Kindly Email your 2 pages motivation essay, Curriculum Vitae (CVs), and articles or audio / broadcasts or web link to:
For any inquiry call 0755 963189 
Note: Indicate IBEJ + Surname on the Subject line of your email.
Come learn and grow your skills in business environment reporting and build you capacity to serve Tanzania!

UJANGILI WACHAFUA SIFA YA TANZANIA KWA NCHI ZA ULAYA NA ASIA.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII BALOZI KHAMISI KAGASHEKI AKIJIBU MASWALI YA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MKAKATI WA SERIKALI WA KUKABILIANA NA KASI YA UJANGILI ,KWENYE VIWANJA VYA HOTELI YA MOUNT MERU JIJINI ARUSHA AMBAPO ALISEMA VITENDO HIVYO VIMEICHAFUA TANZANIA KWA MATAIFA YA AMERIKA,ULAYA NA ASIA

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA BAADHI YA WABUNGE WALIOSIMAMA KWENYE UKUMBI WA MOUNT MERU HOTEL SIKU YA KUTANGAZA VIVUTIO VILIVYOSHINDA KWENYE MAAJABU SABA YA ASILI AMBAPO TANZANIA ILIIBUKA KIDEDEA KWA VIVUTI VITATU VILIVYOSHINDANISHWA KUSHINDA.

UJANGILI WACHAFUA SIFA YA TANZANIA KWA NCHI ZA ULAYA NA ASIA.
Na Anthony Mayunga-Arusha.
Februari 17,2013.
SERIKALI ya Tanzania inahusishwa na vitendo vya ujangili na uuzaji wa meno ya tembo nje ya nchi.
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wake na wadau wa sekta ya utalii kwenye ukumbi wa hoteli ya Mount Meru jijini Arusha alisema tatizo hilo limeichafua nchi.
Alisema kwa nchi za Marekani na barani Asia sifa ya Tanzania kwa suala la ujangili ni mbaya kwa kuwa inahusishwa na vitendo hivyo vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya watu wa ndani na nje ya nchi.
“Hatuwezi kukubali kubeba sifa mbaya hiyo.. wanatusema sana wenzetu huko nje…hata wadau wa sekta ya utalii kwenye kikao wamesema…wakihusisha baadhi ya watendaji wa serikali na mtandao huo”alisema.
Kagasheki alisema mtandao wa ujangili ni mkubwa tena unatumia silaha za kivita ambazo zinatishia uhai wa askari wa hifadhi hizo na kuwa tayari mkakati wa kuunganisha nguvu za pamoja umekamilika ili kuhakikisha wanatokomeza mtandao huo.
“Ni mtandao mkubwa lakini hautatushinda lazima utokomezwe maana tusipofanya hivyo sifa tulizopata kwa vivutio vyetu kushinda kwenye mashindano ya vivutio bora vya asili Afrika hautakuwa na maana …lazima tulinde raslimali hizi zinazochangia pato kuwa kwa taifa”alibainisha.
Aliwaonya baadhi ya watumishi wanaoshirikiana na wahujumu uchumi kuwa hatua kali zitachukuliwa kwao,huku akisisitiza kuwa wanakusudia kurekebisha sheria ili ziwe kali kwa wanaokamatwa kwenye makosa hayo.
Kuhusu suala la silaha zinazotumiwa na majangili alisema zinatishia usalama wan chi kwa kuwa wanatumia silaha kali za kivita ambazo zinatakiwa kudhibitiwa.
Alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa idara yake imejipanga kusafisha watendaji wasiokuwa waadilifu kwa kuwa baadhi ya wadau wa sekta ya utalii wameishapoteza imani na idara hiyo kutokana na urasimu wa watendaji kitendo alichosema atakikomesha mara moja.
Februari 11 mwaka huu Vivutio vya Mlima Kilimanjaro,Bonde la Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti zilitangazwa kuwa washindi kwa vivutio vya maajabu saba ya asili.
Mbali na hivyo pia mto Nile kwa Uganda,maporomoko ya Zambia,Jangwa la Sahara vilikuwa miongoni mwa vilivyoshinda ,mashindano yaliyoandaliwa na shirika la Seven Natural Wonders of Afrika la Taxes Nchini Marekani ,ambapo Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikabidhi tuzo kwa washindi.
Mwisho.