Subscribe:

Ads 468x60px

MKUU WA SHULE,OFISA ELIMU WATUHUMIWA KUCHOTA FEDHA ZA NYUMBA YA MWALIMU.


 MKUU WA SHULE,OFISA ELIMU WATUHUMIWA KUCHOTA FEDHA ZA NYUMBA YA MWALIMU.
MEI 1,2013.
Serengeti.

WAKATI taifa likiwa kwenye kihoro cha matokeo mabaya ya kidato cha nne,mkuu wa sekondari ya Nyambureti  kwa kushirikiana na ofisa elimu sekondari wilayani Serengeti wanatuhumiwa kula sh,mil.9 za ujenzi wa nyumba ya Mwalimu.

Fedha hizo zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mwalimu toka akaunti ya Maendeleo ya halmashauri hiyo,ikiwa ni kuchangia nguvu za wananchi kwa ujenzi wa nyumba ya Mwalimu.

Ubadhirifu huo  unadaiwa kumhusisha mkuu wa shule hiyo  Patrick Majige kwa kushirikiana na ofisa elimu sekondari William Makunja na kupelekea nyumba hiyo  kutokujengwa.

Blogu hii ilibaini kuwa fedha hizo zilitolewa mwaka 2010 na kuwekwa akaunti ya shule benki ya NMB tawi la Mugumu wilayani hapa,hazikufanya kazi kusudiwa badala yake zilitumika kulipana  posho za safari zisizo na  na wito kwa idhini ya ofisa elimu sekondari.

Kwa mjibu wa uchunguzi wa blogu  ulibaini tarehe 1,1,2011 akaunti hiyo ilikuwa na kiasi cha sh,10,489,660= baada ya kupokea sh.mil.9 fedha za mradi na sasa benki hakuna fedha na nyumba haijajengwa.

Blogu hii imeona  ripoti ya mkaguzi wa ndani ya halmashauri hiyo ikionyesha kwa kipindi cha januari 1/2011 hadi desemba 31.2012 posho za safari zilikuwa zimegharimu sh.7,703,400=.

Safari zote zikiwemo za  kuitwa wilayani ambazo ziligharimu sh.1,254,000  hazikuwa na  viambatanisho vya barua za wito zote zikiidhinishwa na ofisa elimu sekondari ambaye pia hukaimu nafasi ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri mara kwa mara.

Taarifa hiyo imebainisha kuwa fedha hizo zimetumika kinyume cha lengo kusudiwa la ujenzi wa nyumba bila kufuata sheria,kanuni na taratibu za kubadili matumizi ya fedha ya miradi husika.

Katika hitimisho la mkaguzi amebainisha kuwa mkuu wa shule hiyo Majige anawajibika kwa kubadilisha matumizi ya fedha sh,mil.9 za ujenzi wa nyumba ,malipo ambayo yameidhinishwa na wakuu wake wa idara wakijua fedha hizo si za utawala.

Kuchulikuwa kwa fedha hizo kunakwamisha juhudi za wananchi waliokuwa wameandaa viashiria kama mawe,mchanga na saruji mifuko 48 toka  mwaka 2011ambayo iko hatarini kuharibika kutokana na kukaa muda mrefu.

Ofisa elimu.

Ofisaelimu shule za sekondari William Makunja ambaye hukaimu nafasi ya  Mkurugenzi Mara kwa mara  alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusiana na tuhuma hizo kwanza alisita kisha akasema”shule gani hiyo Nyambureti…nilikuwa sijui nitafuatilia ili kujua kama nyumba haijajengwa”alisema.

Alipotakiwa kufafanua kama ameishampitishia  fedha mkuu wa shule na  kwa kazi zipi ,hakukubali wala kukataa,bali alibaki kushangaa kuhusu mwandishi kupata taarifa hizo.

Mkuu wa sekondari.

Majige ambaye ni mtuhumiwa wa ufujaji huo alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi na kuulizwa  atoe ufafanuzi kuhusiana na tuhuma hizo  akasema”nipo hapa Mugumu..ulikuwa unataka kujua suala la nyumba ya Mwalimu…niko Mwanza ,unataka kujua fedha za nyumba….mimi nasema,aaah….sihusiki”alisema kwa kusitasita.

“Haya mambo tunatakiwa tuonane ili tuongee vizuri….maana haya mambo si mazuri …umepata wapi hizo habari zote….mimi sihusiki wala sijui….lakini ninge…”akakata simu bila kumalizia sentensi yake.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Good Pamba hakupatikana ofisi kwa kile kilichodaiwa kuwa yuko Musoma kikazi,hata hivyo anadaiwa kutokuchukua hatua licha ya kukabidhiwa taarifa ya ukaguzi.

Diwani.

Nicholaus Maro diwani wa kata hiyo anasema kutokana na ukosefu wa nyumba za walimu amepokea walimu wawili waliopangia hapo wanaishi kwake,huku akisisitiza kuwa tatizo hilo linapelekea walimu kuikimbia shule hiyo.

“Kama fedha zinaletwa za kujenga nyumba ya mwalimu ,mkuu anashilikiana na afisa wake wanakula fedha hizo,mamlaka ziko kimya ….hii inakatisha tamaa ,na wanaoathirika ni watoto wetu kitaaluma …hili hatutalinyamazia”amedai.

Mwisho.