Subscribe:

Ads 468x60px

MATUKIO MBALIMBALI WILAYANI SERENGETI.

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Chamoto Mamlaka ya mji wa Mugumu wilaya Serengeti Rhobi Magoiga akikabidhi zawadi ya sh 25,000 kwa nahodha wa timu ya Magetta Fc baada ya kushinda mashindano ya Sabasaba.
 Rhobi akitoa zawadi ya soda kwa timu ya Magetta baada ya kuibuka washindi
 Mitambo ya Kampuni ya Samota Ltd kutoka Nzega ikisawazisha barabara ya mjini Mugumu wilaya ya Serengeti inayojengwa kwa kiwango cha lami nyepesi
 Mtambo ya Samota ikisawazisha barabara ikiwemo kubomoa majengo,vibanda vilivyojengwa katika hifadhi ya barabara
 Thomas Burito kada wa ACT WAZALENDO katikati akiwa na viongozi wa chama hicho wakati wa kuchukua fomu za kuwania ubunge wa jimbo hilo.
 Thomas akisaini kuchukua fomu ya kutaka kuteuliwa ndani ya chama hicho kuwania nafasi ya Ubunge ,anayeshuhudia ni katibu mwenezi wilaya Hamisi Lazaro
 Burito akielekea ofisi ya Act wilaya kuchukua fomu,msafara wake ulisimamiwa na kuongozwa na askari wa usalama barabarani
 Uboreshaji wa barabara unaendelea
 Burito anamwaga sera zake nini atawafanyia wakazi wa jimbo hilo iwapo atateuliwa na chama kisha kuchaguliwa na wananchi
 Huyo ni mmoja wa boda boda mjini Mugumu ambaye inadaiwa ni kada maarufu wa chama hicho,hapo akiwa eneo la ofisi ya wilaya hiyo mtaa wa NHC
 Pokea fomu kajaze kisha urudishe na ukiteuliwa peperusha vema bendera yetu,anasisitiza Katibu mwenezi wa wilaya Hamisi
 Msafara wa mtia nia ulipambwa na burudani mbalimbali ikiwemo pikipiki,magari na muziki
 Msafara wa ACT Wazalendo
Mambo ya Act Wazalendo

0 comments:

Post a Comment