Subscribe:

Ads 468x60px

MTOTO ALIYEZALIWA UTUMBO UKIWA NJE APELEKWA BUGANDO




 MTOTO ALIYEZALIWA UTUMBO UKIWA NJE AKIWA CHINI YA UANGALIZI WA WAUGUZI NYERERE HOSPITALI WILAYANI SERENGETI KABLA YA KUPELEKWA HOSPITALI YA RUFAA YA MWANZA


MTOTO ALIYEZALIWA UTUMBO NJE APELEKWA BUGANDO
Oktoba 22,2013.
Serengeti:HOSPITALI Teule ya Nyerere wilayani Serengeti imetoa rufaa ya mtoto  aliyezaliwa katika kijiji cha Nyichoka wilaya ya Serengeti utumbo ukiwa nje kwenda hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya matibabu zaidi.
Mtoto huyo wa kike  alizaliwa oktoba 20 mwaka huu utumbo ukiwa nje hali iliyowachanganya wazazi wake Edward Mgabo(25)na Hadija Rajabu(21) kutokana na hali aliyokuwa nayo,lakini akiwa mwenye afya njema.
Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dk,Calvin Mwasha amesema wamelazimika kutoa rufaa kwenda Bugando kwa kuwa hawana madaktari bingwa wa matatizo kama hayo,na hali aliyonayo anahitaji huduma za haraka ili kunusuru maisha yake.
“Matatizo kama haya hutokana na ukuaji…miezi mitatu ya mimba …viungo hutengenezwa ,hapo ndipo hutokea mambo kama hayo….ni mambo ambayo hutokea kitaalam yanajulikana na ndiyo maana kuna wanaoyashughulikia”alisema.
Alisema inapotokea inahitaji huduma za haraka sana ikiwa ni pamoja na upasuaji mara moja ili kudhibiti mambo yanayoweza kuchangia kupata maambukizi mengine.
Akisimulia tukio hilo baba wa mtoto huyo Mgabo alisema,”tukiwa tunaenda zahanati ya Nyichoka mke wangu alizidiwa na kujifungulia njiani…tulisaidiwa na watu wakamfunga kitovu mtoto …lakini utumbo ukaonekana uko nje,tukaambiwa tuwahi zahanati Muuguzi naye akasema hana uwezo twende wilayani”alisema.
Alibainisha walipofika kila mmoja anaonekana kushangaa na kusema hilo tatizo wanatakiwa kwenda Bugando”huyu ni mtoto wangu wa kwanza kwa mwanamke huyu ambaye nilimkuta na mtoto mwingine…tunapambana kupata fedha ili kuokoa maisha ya mtoto wetu “alisema kwa masikitiko.
Mama mzazi wa mtoto Hadija alisema wakati wa ujauzito hapakuwa na tatizo lolote ,na hata wakati anajifungulia njiani hapakuwa na shida kwa kuwa mtoto alikuwa mzima ,lakini alishangaa kuona utumbo uko nje na akawa amekata tamaa kama ataweza kuishi.
Muuguzi wodi la wajawazito Anjelina Biseko alisema kuwa watoto kama hao wanapofikishwa Bugando huwekwa kwenye mifuko maalum kwa muda wa miezi mitatu kisha hufanyiwa upasuaji ili kurudisha hali yake ya kawaida
Muuguzi mkuu wa hospitali hiyo Neema Mechara alisema kwa mwaka huu hilo ni tukio la kwanza kutokea,lakini kumewahi kutokea tukio kama hilo kwa mtoto kuzaliwa viungo vya ndani vikiwa nje,na wengine maumbile ya ajabu ajabu.
Mwisho.