Subscribe:

Ads 468x60px

ZABURI YA 72 ALIYOITUMIA DK,MATHAYO DAVID MATHAYO KUSALI WAKATI MAWAZIRI WALIPOWEKWA KITI MOTO KISHA KUMWAGWA


.1.Ee  mungu ,mpe  mfalme  hukumu   zako,  na  mwana  wa  mfalme   haki  yako.
2.Atawaamua  watu  wako kwa haki, na watu  wako   walioonewa  kwa  hukumu.
3.Milima  itawazalia  watu  amani,na  vilimaa  navyo  kwa  haki.
4.Atawahukumu  walioonewa  wa watu,atawaokoa  wahitaji  , atamseta  mwenye  kuonea.
5.Watakuogopa   wakati  wote  wa  kudumu  jua,na wakati  wa  kung’aa  mwezi  kizazi  hata  kizazi.
6.Atashuka  kama  mvua  juu  ya majani  yaliyokatwa,Kama  manyunyu  yainyweshayo  nchi.
7.Siku zake  yeye, mtu  mwenye  haki  atasitawi,na  wingi  wa  amani  hata  mwezi  utakapokoma.
8.Na   awe  na enzi  toka  bahari   hata bahari,Toka  mto  hata  miisho  ya  dunia.
9.Wakaao  jangwani  na wainame  mbele  zake;adui  zake  na  warambe  mavumbi.
10.Wafalme  wa tarshishi na  visiwa  na  walete  kodi,Wafalme  wa Sheba  na  Seba   na  watoe  vipawa.
11.Naam, wafalme  wote  na  wamsujudie,na  mataifa  yote   wamtumikie.
12.Kwa  maana atamwokoa  mhitaji  aliapo,na  mtu  aliyeonewa  iwapo  hana  msaidizi.
13.Atamhurumia   aliye  dhaifu  na maskini,na nafsi  za  wahitaji  ataziokoa.
14. Atawakomboa  nafsi  zao na  kuonewa  na  udhalimu,na  damu  yao  ina  thamani  machoni pake.
15.Basi na aishi;na  wampe  dhahabu  ya Sheba;na wamwombee  daima;  nakumbariki  mchana  kutwa.
16.Na  uwepo  wingi  wa  nafaka  katika  ardhi  juu  ya milima;matunda  yake  na yaweyawe  kama  lebanoni,
na  watu  wa  wastawi  kama  majani  ya  nchi.
17.Jina  lake  na  lidumu  milele,Pindi  ling’aapo  jua    jina  lake  liwe na wazao.
Mataifa  yote    na wajibariki  katika  yeye,na  kumwita  heri.
18.Na  ahimidiwe  Bwana,  Mungu,Mungu  wa  Israeli,atendaye  miujiza  yeye peke  yake.
19.Jina  lake    tukufu  na  lihimidiwe  milele;dunia  yote  na  ijae  utukufu  wake. Amina  na  amina.
20.Maombi  ya  Daudi  mwana  wa  yese  yamekwisha.
 

j