Subscribe:

Ads 468x60px

UCHAGUZI AFRIKA KUSINI NA MALAWI JUKWAA LA KATIBA LATOA TAMKO



JUKWAA LA KATIBA TANZANIA
P. O. Box 78466, Plot No. 201 Block 46 Kijitonyama, Adjacent to Kijitonyama UDSM Hostels Flats,
Dar Es Salaam, TANZANIA; Tel: +255 22 2773795 Fax: +255 22 2773764 Cell: 0783 993088
E-mail: jukwaa.katiba@gmail.com,info@jukwaalakatibatz.com Web site: www.jukwaalakatibatz.com
CHAGUZI ZA AFRIKA KUSINI NA MALAWI NA
MAFUNZO MAKUU YA KIKATIBA KWA TANZANIA
TAMKO KWA UMMA KUPITIA
VYOMBO VYA HABARI
Kama sehemu ya majukumu yake ya kufuatilia masuala ya michakato
ya Katiba na utekelezaji wake nchini Tanzania na katika nchi jirani,
JUKWAA LA KATIBA TANZANIA limekuwa na utaratibu wa kupeleka
waangalizi wa uchaguzi na upigaji kura za maoni katika nchi za
Afrika. Lengo kuu limekuwa ni kutazama na kujifunza namna
ambavyo uchaguzi, kama sehemu muhimu ya utekelezaji wa katiba
za nchi husika umekuwa ukifanyika huku msisitizo ukiwa ni
kuchunguza jinsi vyombo vikuu vinavyoanzishwa kikatiba vinafanya
kazi zake katika uchaguzi. Ni wazi kuwa utendaji bora wa vyombo na
taasisi za Kikatiba ni muhimu sana katika kuufanya uchaguzi ufanyike
kwa uwazi, uhuru na haki au kinyume chake.
2
Tamko hili linafuatia uangalizi wa JUKATA katika uchaguzi
uliofanyika nchini Afrika Kusini tarehe 7/5/2014 na nchini Malawi
tarehe 20/5/2014 ambapo Jukwaa la Katiba Tanzania lilipeleka
waangalizi kadhaa kwa uchaguzi katika nchi zote hizi mbili. Mambo
makuu tuliyoyaona na mafunzo muhimu kwa Tanzania yamo katika
tamko hili kwa Umma.
UCHAMBUZI LINGANISHI WA NCHI YA MALAWI NA AFRIKA YA
KUSINI
1.1 MAZINGIRA AMBAMO UCHAGUZI UNAFANYIKA
Tuanze kwa kukiri kuwa katika nchi hizi mbili mazingira ya kisiasa,
kiuchumi na kijamii ni tofauti sana pamoja na kwamba nchi zote mbili
ni nchi za kiafrika na zote ziko Kusini mwa Afrika. Kwa mfano, wakati
hali ya kiuchumi ya Afrika Kusini ni ahueni kubwa labda kuliko nchi
nyingine yoyote ya Afrika, hali ya Kiuchumi ya Malawi mbaya sana.
Kumekuwa na mdororo wa Kiuchumi katika nchi ya Malawi kwa
miaka mingi sasa lakini hasa kuanzia mwaka 2012. Zipo fununu kuwa
hata kifo cha Rais wa Zamani wa Nchi hiyo, Dkt. Bingu wa Mutharika
ambako kulisababishwa na msongo wa mawazo na shinikizo la damu
kunaweza kuwa kulichangiwa na maandamano ya wananchi hususan
vijana kutokana na matatizo ya ajira na mengineyo kutokana na
mdororo wa uchumi. Ikumbukwe kuwa Rais Mutharika alianguka
akiwa kazini ikulu ya Malawi baada ya mjadala mrefu wa namna ya
kushughulikia matatizo ya Malawi ya ukosefu mafuta na fedha za
kigeni ambayo yalionekana kutokuwa na suluhu yoyote. Uchaguzi wa
3
Malawi umekuja wakati ambapo Malawi iko hoi na kusababisha hata
maandalizi yake kuathiriwa vibaya sana. Ziko gharama za huduma
ambazo Tume ya Uchaguzi Malawi (MEC) iliziombea kwa wafadhili
lakini kwa kuchelewa kupata fedha iliilazimu Tume kuingia mikataba
kwa kutegemea malipo yatafanywa moja kwa moja na mfadhili
husika. Hilo nalo limechangia sana katika kuathiri utendaji wa Tume
ya Uchaguzi wa Malawi kwa kuwa watumishi na watoa huduma
wengi walikuwa na malalamiko mengi ya kucheleweshewa malipo
kiasi cha kuwa na hamasa ndogo sana ukilinganisha na morali
iliyokuwepo kwa watumishi na watoa huduma wa Afrika Kusini.
1.2 UHURU NA KUKUBALIKA KWA TUME ZA UCHAGUZI
Kukubalika kwa Tume ya uchaguzi katika nchi husika ni jambo
muhimu sana. Aidha, upo uhusiano kati ya imani ya wadau wa
uchaguzi na wananchi kwa Tume na kuwepo au kukosekana amani
katika uchaguzi husika. Wakati nchini Afrika Kusini kuna Tume Huru
ya uchaguzi ya Afrika Kusini (IEC) yenye uongozi na watumishi huru
Tume ya uchaguzi ya Malawi (MEC) imeonyesha udhaifu mkubwa
kuhusu namna ya uundwaji wake na kutokana na hilo uhuru wake
unaonekana kutiliwa mashaka ingawa matatizo ya kiuchaguzi
ambayo yametokea Malawi Tume imejitahidi kwa kiasi chake kuhimili
na kutatua matatizo pamoja na mashiniko toka kwa viongozi wa nchi.
Tume Huru ya uchaguzi ya Afrika ya Kusini ilionekana kutoa
maamuzi makini na ya haraka kwa hitilafu za uchaguzi zilizotokea,
kila zilipotokea. Kwa mfano, kwa kuwaondoa maafisa wake hapo
4
hapo bila kupoteza muda kwenye kituo cha kupigia kura cha Nigel –
Eastrand baada ya kuhifadhi vifaa vya kupigia kura nyumbani kwa
kada wa chama, Tume huru ya Uchaguzi ya Afrika Kusini iliweza sio
tu kukomesha vitendo kama hivyo kutfanywa na watumishi wengine
lakini pia Tume iliweza kujijengea heshima na imani kubwa toka kwa
wadau wa uchaguzi na wapiga kura. Hiyo ilikuwa tofauti sana na
Malawi, ambako Tume ya Uchaguzi ambayo ni kipande na huungwa
wakati wa uchaguzi pekee kama ilivyo nchini Tanzania ilishindwa
kushughulikia watumishi wake waliohusika na tuhuma za kutaka
kuiba karatasi za kupigia kura kabla ya siku ya upigaji kura. Katika
sakata hilo, Mkuu wa Wilaya ya Lilongwe na Mkurugenzi wa Jiji la
Lilongwe walijiuzulu nyadhifa zao kama waratibu wa uchaguzi baada
ya kuhusika na tuhuma za kuvuruga uchaguzi lakini badala ya
kuchunguzwa na kuadhibiwa na Tume, Tume iliwaomba kufikiria
kurejea kazini na kuendelea na majukumu yao kama kawaida. Katika
maeneo mengine ambako vifaa vya uchaguzi hafikuwepo bila sababu
za kuridhisha kama Area 24 (Lilongwe) na Blantyre, watumishi
walioshindwa kufikisha vifaa hivyo hawakuchukuliwa hatua zozote
kiasi cha kusababisha maandamano na vurugu za wananchi
wakitaka watendaji hao wachukuliwe hatua, bila mafanikio.
Uhuru wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi pia ulikuwa ukitiliwa shaka
kutokana na Mwenyekiti wake, Jaji Maxon Mbendera kuwa Jaji wa
Mahakama kuu ya Malawi ambayo inaonekana kuwa upande wa
serikali zaidi. Katika Nchi ya Afrika Kusini, Mwenyekiti wa Tume Huru
ya Uchaguzi ya nchi hiyo ni Mwanasheria na Wakili huru na wa
5
kujitegemea ambaye hafungamani na chombo chochote cha kiserikali
zaidi ya Tume Huru ya Uchaguzi. Hili limesaidia sana imani kubwa ya
wadau na wananchi kwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Afrika Kusini.
1.1. MAZINGIRA YA KIUCHAGUZI
Katika nchi zote mbili Marais walioko madarakani walikuwa
wanagombea tena kwenye chaguzi hizi zilizopita lakini tumeona kuwa
kulikuwa na utulivu zaidi Afrika Kusini kutokana na uhuru na uimara
wa Tume ya uchaguzi kwa kutoegemea upande wowote na vyombo
vingine vya kikatiba kuliko nchini Malawi ambapo Tume ya Uchaguzi
na vyombo vingine vya kikati vilijaribu kuyumbishwa sana na Rais
aliyeko madarakani, Dkt. Joyce Banda, hasa baada ya kutangaza
kufuta uchaguzi wa Malawi 2014. Matumizi mabaya ya ibara za
Katiba yalionekana wazi wakati wa kutangaza kufuta uchaguzi kwa
kutumia ibara ya 88 (2) ambayo inampa Rais Jukumu la kulinda na
kuimarisha umoja na Mshikamano wa Nchi ya Malawi. Ilishangaza
sana wengi kuwa Rais Banda alichukulia kuwa kukaribia kuanguka
kwake na Chama chake katika uchaguzi kulikuwa ni sawa na
kuvurugika kwa umoja na Mshikamano nchini humo. Jambo la
kujifunza hapa ni kwamba ipo haja ya kukemea wanasiasa
wanaojaribu kucheza na ibara na vifungu vya Katiba kwa kuvipa
tafsiri inayowasaidia kwa wakati husika. Mchezo kama wa Malawi
ungeweza kuleta vurugu hadi kupelekea machafuko na umwagaji
damu katika nchi hiyo isingekuwa uimara wa Mahakama katika
kukemea na kubatilisha kauli ya Rais la kufuta uchaguzi.
6
Kuhusiana na haki za makundi mbalimbali katika uchaguzi na
mazingira ya kuwawezesha waweze kufaidi haki yao ya kupiga kura
bila vikwazo, JUKATA tumebaini tofauti kubwa iliyopo kati ya
mazingira ya Afrika Kusini na yale ya Malawi. Wakati mazingira ndani
ya Afrika Kusini yaliandaliwa vizuri sana hadi kuwezesha watu wenye
ulemavu, wazee, vikongwe, wagonjwa, na wajawazito kuweza kupiga
kura kabla ya siku ya watu wote, hali ilikuwa tofauti huko Malawi
ambako hakukuonekana kuwa na utaratibu wa mazingira mazuri kwa
makundi maalum. Aidha, miundombinu katika vituo vya kupigia kura
ndani ya Afrika kusini iliruhusu watu wenye ulemavu kuweza kuvifikia
vituo na kupiga kura bila matatizo. Pia JUKATA tulishuhudia
watumishi na maafisa wa Independepent Electoral Commission (IEC)
wakitoa msaada na kuwapa kipaumbele watu wenye mahitaji maalum
ikiwemo wazee na wenye ulemavu hata siku ya uchaguzi kwa nchi
nzima. Tofauti na huko, vituo vya kupigia kura katika maeneo yaliyo
mengi nchini Malawi vilikuwa katika maeneo ya wazi na ambayo
hayajafunikwa kiasi kwamba watu kadhaa wenye ulemavu wa ngozi
walionwa wakiwa wamejifunika vichwa kwa shida ya kuumizwa na
jua. JUKATA tulibaini kuwa watendaji wengi wa Tume ya Uchaguzi
ya Malawi nao walikuwa wakilalamikia kuunguzwa na jua huku
wakiombea mvua isinyeshe kwa kuwa ingeathiri vibaya zoezi la
uchaguzi. Katika vituo viwili vya Lilongwe manispaa na area one,
JUKATA tulishuhudia ngazi ambazo si rafiki kwa mwenye ulemavu
zikiwa katikati ya sehemu ya kuchukuwa karatasi za kura na sehemu
ya kupigia kura. JUKATA tungependa kushauri Tume ya Taifa ya
7
uchaguzi hapa Tanzania kuanza maandalizi mapema ya sehemu
zitakazofanywa vituo vya kupigia kura ili kepuka mapungufu
yaliyojitokeza Malawi.
1.2. KASHFA KWA WAGOMBEA
Katika nchi zote mbili kulikuwa na kashfa kwa wagombea Urais
ambao walikuwa marais walioko madarakaniHuku Rais Jacob Zuma
alikabiliwa na kashfa ya Nkandla ya matumizi mabaya ya pesa za
umma kuboresha makazi binafsi, Rais Joyce Banda alikabiliwa na
kashfa ya Cashgate inayohusu uchotaji wa mabilioni ya pesa za
Malawi zinazofikia zaidi ya dola milioni 60 wakati akiwa Makamu wa
Rais wakati wa serikali ya DPP iliyoongozwa na marehemu Rais
Bingu wa Mutharika aliyefariki mwaka 2012. Rais Banda
ametuhumiwa kuendelea na uchotaji wa mabilioni hata baada ya
kushika nafasi ya urais ambayo ameshikilia kwa miaka takribani
miwili. Rais Jacob Zuma aliathiriwa kidogo sana kwa sababu katika
mfumo wa uchaguzi wa Afrika Kusini Chama ndicho kinagombea na
kupigiwa kura na sio mtu binafsi wakati Rais Joyce Banda wa Malawi
aliathirika vibaya sana hata kuelekea kupoteza nafasi ya Urais.
Haijajulikana bado kama Rais Banda ataweka kutoka nafasi ya tatu
alipo hivi sasa kwa kura theluthi moja zilizokwishahesabiwa hadi
kuibuka mshindi wa kinyang’anyiro cha Urais.
1.3. MATUMIZI YA VIFAA VYA KAMPENI SIKU YA
UCHAGUZI
8
Waangalizi wa JUKWAA LA KATIBA TANZANIA walishuhudia baadhi
ya wapiga kura wakiwa wamevaa mavazi ya kampeni siku ya
uchaguzi na hasa maeneo ya Pretoria na Johanesburg ambako
katika itongoji kama vya Yeoville, Alexandra, Soweto, Hillbrow na
Diepsloot watu kadhaa waliovalia fulana za ANC, kofia za EFF na
vikoti vya DA walionekana kwenye misitari wakielekea kwenye
vyumba vya kupigia kura wakiwa hawana wasiwasi wowote. Hata
wasimamizi wa uchaguzi na vyombo vya usalama vilionekana
kutojishughulisha kabisa na uvaaji wa mavazi yenye nembo na picha
za vyama vya Siasa hata pale mavazi hayo yalipokuwa yakigawiwa
kwa watu wengine katika vituo vya kupigia kura. Watu wengine
walikuwa wakipeperusha bendera za vyama vyao kwenye baiskeli
walizokuwa wanaendesha. Tulishuhudia na ikatolewa kwenye
vyombo vya habari pia kwamba mahali penginepo ndani ya Afrika
Kusini, vyama vikubwa vilikuwa vinagawa vifaa hivi karibu na vituo
vya kupigia kura siku ya upigaji kura bila kukemewa na yeyote.
Jambo hili linahitaji kuchunguzwa na kuona kama limeleta madhara
yoyote kwa uchaguzi wa Nchi hiyo. Itakumbukwa kuwa mavazi
yanayoashiria Kampeni ni maraufuku siku ya upigaji kura katika nchi
nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania. Katika Malawi, jambo hili
liliheshimiwa sana na hakuna hata vazi moja lilionekana katika vituo
vya kupigia kura ambavyo vilitazamwa na waangalizi wa JUKWAA LA
KATIBA TANZANIA.
1.4. HAMASA YA WAPIGA KURA
9
Hamasa ya wapiga kura nchini Afrika Kusini ilikuwa kubwa sana
kama ilivyokuwa pia Malawi. Kabla ya siku ya kupiga kura baadhi ya
maeneo kama Mpumalanga wananchi waliohojiwa walisema
hawatatoka kwenda kupiga kura kwa sababu serikali inawatembelea
kipindi cha kupiga kura tu nabaada ya hapo serikali inapotea. Wapiga
kura walionekana wakilalamikia ukosefu wa huduma muhimu kama
maji na umeme na pengo linalozidi kuongezeka kati ya masikini na
matajiri wan chi hiyo. Machafuko pia yalionekana sehemu za
Alexandra na baadhi ya maeneo huko Kwa Zulu Batal (KZN). Hata
hivyo, ilipofika siku ya kupiga kura, wananchi wa marika na rangi
mbalimbali (wazungu, wahindi, wenye asili ya mchanganyikohalfcaste
na waafrika) walionekana kwenye mistari ya kupigia kura
kwa wingi wa kutosha. Takwimu za mwisho za mwitikio wa wapiga
kura katika uchaguzi wa Afrika Kusini imeonesha kuwa asilimia 73%
ya wananchi milioni zadi ya 25 waliojiandikisha Afrika Kusini
waliweza kupiga kura. Hamasa ya wapiga kura pia ilikuwa kubwa
sana nchini Malawi kuashiria kuwa wananchi walitaka kufanya
mabadiliko katika uongozi wa nchi. Vijana wa Malawi walionekana
kuwa ndio wenye hamasa zaidi ya kutaka kupiga kura, wengi wakiwa
wanapiga kura kwa mara ya kwanza. Ingawa takwimu halisi za
mwitikio wa wapiga kura (turn out) katika uchaguzi wa Malawi
hazijatoka, inakadiriwa kuwa zaidi ya ailimia 80 ya Wamalawi milioni
7.5 walijitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa tarehe 20 Mei 2014.
Huu ni mwitikio mkubwa sana ikilinganishwa na Tanzania ambako
katika uchaguzi wa mwaka 2010 ni asilimia 42 tu ya watanzania
milioni 20 walio katika daftari la kudumu la wapiga kura waliweza
10
kupiga kura. JUKWAA LA KATIBA TANZANIA tumebaini kubwa
mwitikio mkubwa wa wapiga kura Afrika Kusini na Malawi
kumechangiwa na elimu kubwa nay a mapema ya uraia na
uhamasishaji wa wapiga kura iliyofanywa katika nchi hizo.
Ilitushangaza na kutufurahisha kuwa kazi ya uhamasishaji wa wapiga
kura kujiandikisha ilifanywa hata na vyama vya siasa ndani ya Afrika
Kusini kitu ambacho si utamaduni wa vyama vya Siasa nchini
Tanzania.
2.0. MAFUNZO KWA TANZANIA
2.1. UIMARA WA TAASISI ZINAZOSIMAMIA UCHAGUZI NA
ULINZI NA USALAMA WA TAIFA
Kutokana na hali iliyojitokeza nchini Malawi ambapo Rais aliyeko
madarakani alikuwa anagombea na hamasa ya wananchi ilikuwa juu
kuashiria kutaka mabadiliko ya uongozi, Rais aliyeko madarakani alipoona
dalili za kushindwa akaanza kutoa amri ovyo kwa taasisi na vyombo
mbalimbali muhimu vya usimamizi wa uchaguzi na ulinzi wananchi.Somo
hapa kwa Tanzania ni kuwa lazima vyombo hivi visukwe katika namna
ambayo havitapendelea mtu yeyote na kusikiliza amri wakati wa uchaguzi.
Vyombo hivi ni pamoja na Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC), Jeshi la
Polisi, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Vyombo vya habari vya
umma yaani Televisheni na Redio ya Taifa (TBC) na Idara ya Usalama wa
Taifa. Hii itasaidia kulinda usalama wa Raia, mali zao na Taifa kwa ujumla
kuliko kulinda chama na kikundi cha watu au hata kuishia kumlinda mtu
mmoja anayegombea Urais. Aidha, nafasi ya mahakama katika sio tu
11
kusikiliza na kutolea uamuzi mashauri yahusuyo uchaguzi kwa haraka
lakini pia kutoa tafsiri juu ya maamuzi ya vyombo na wanasiasa
imejidhihirisha wazi ndani ya Afrika Kusini lakini hasa Malawi. Nafasi ya
vyombo vingine kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
nayo imeonekana kuathiri uchaguzi katika nchi mbili tulizoangalia uchaguzi
wake mwezi Mei, 2014. JUKATA tunapendekeza kuwa mahakama zetu
lazima zifanye jitihada ya kuwa huru na kujiweka katika nafasi ya kuepuka
upendeleo kuelekea, wakati na baada ya uchaguzi.
2.2. ELIMU YA URAIA NA ELIMU YA MPIGA KURA NI MUHIMU
Elimu ya uraia ni muhimu sana ifanywe Tanzania muda wote na serikali
itoe ruzuku kwa vyombo vya habari hata vya binafsi ili kusambaza elimu hii
muhimu kwa upana zaidi na kufika kila pembe ya nchi ili kuwa na wapiga
kura na wananchi wenye uelewa wa kutosha kwa ajili ya kulinda maslahi
na usalama wa Taifa ili kuepusha fujo na vurugu katika nchi. Ni wito wetu
kwa wadau wa uchaguzi nchini kuwa Elimu ya Uraia na elimu ya Mpiga
kura lazima ianze angalau mwaka mmoja kabla ya uchaguzi na sio
kufanyika ndani ya miezi sita (6) kabla ya siku ya kupiga kura.
2.3 UANDIKISHAJI NA UHAKIKI WA MARA KWA MARA WA WAPIGA
KURA KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
JUKWAA LA KATIBA TANZANIA linapenda kukumbusha tume ya uchaguzi
kuanza kurekebisha daftari la wapiga kura. Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya
mwaka 1985 (kama ilivyorekebishwa) inatutaka kuhakiki daftari la wapiga
kura angalau mara mbili ndani ya miaka mitano. Jambo hili halijawahi
kutekelezwa na huo ni uvunjaji wa sheria. Kama tulivyokumbushia mwaka
12
jana kwamba Zanzibar wamesha rekebisha daftari lao, tunapenda
kuchukua fursa hii kuuliza -je daftari la Jamhuri ya Muungano wa
Tananialinasubiri nini? Hii ndio inapelekea urekebishaji wa haraka haraka
na wananchi wengine wanakosa haki zao za msingi za kupiga kura kwa
kushindwa kuingia kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Tatizo liko
wapi?
Mwisho, tunapenda kushauri pia kuwa siku ya kupiga kura Tanzania
ifanywe kuwa siku ya katikati ya wiki na itangazwe kuwa siku ya
mapumziko ili kuruhusu watu wa Kada mbalimbali kupata fursa ya kupiga
kura. Aidha, inapendekezwa kuwa Mchakato unaendelea wa Katiba
uachwe ukamilike ipasavyo ili usuke vema vyombo vikuu vya uwajibikaji
vya kikatiba. Katiba ya Afrika Kusini inaweza kutoa mfano mwema kwa
Tanzania kupitia sura ya tisa (9) ambayo imeweka taasisi imara za Kikatiba
ambazo haziko tayari kutetereka hata wakati wa uchaguzi. Taarifa kamili ya
uangalizi wa JUKWAA LA KATIBA TANZANIA kwa uchaguzi wa Afrika
Kusini na Malawi itakabidhiwa kwa baadhi ya wadau wa uchaguzi nchini
kwa kuanza na Tume ya Taifa ya Uchaguzi hapa Tanzania na Tume ya
Uchaguzi Zanzibar.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika!
Ahsanteni sana kwa usikivu.
Deus M.Kibamba
Mwenyekiti

Asilimia 25 ya walimu hufundisha ‘makorokocho


“Kama suala la walimu halitapatiwa ufumbuzi sasa, tofauti kwenye ufundishaji itakuwepo kwa vizazi vingi huku ikitoa tafsiri mbaya dhidi ya jitihada za kuondoa umaskini duniani na kufikiwa kwa maendeleo endelevu.” Dk Shukuru Kawambwa 
Na Goodluck Eliona, Mwananchi

Posted  Mei31 
Kwa ufupi
  • Mchanganuo uliofanyika katika nchi 41 zenye kipato cha chini, zaidi ya nusu ya vijana wenye umri kati ya miaka 15 na 24, hawawezi kusoma wala kuandika.
Dar es Salaam. Wakati Serikali ikiahidi kuboresha elimu nchini kwa kuhakikisha inaajiri walimu wa kutosha, imebainika kuwa asilimia 25 ya walimu huwafundisha wanafunzi mambo yasiyo ya msingi.
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco), iliyozinduliwa Dar es Salaam hivi karibuni, imebainisha kuwa wakati wananchi wakilalamika kuwa elimu inayotolewa haimsaidii mwanafunzi kupata ajira nzuri, wanafunzi hawajifunzi mambo ya msingi yatakayowasaidia kupambana na changamoto za maisha.
Akizindua ripoti hiyo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa ripoti hiyo imeweka wazi ukubwa wa tatizo la ufundishaji, akieleza kwamba jumla ya watoto milioni 250, duniani wanakosa mafunzo ya msingi ya kusoma, kuandika na kuhesabu, ingawa wanaingia darasani.
“Tanzania kama sehemu ya dunia, haijakwepa tatizo hilo. Baadhi ya watoto wetu wamekuwa wakimaliza shule za misingi bila ya kuwa na ujuzi huo. Hii ni hali ya kushtua, inayohitaji nguvu za pamoja za wadau wote wa elimu duniani,” alisema Kawambwa.
Alibainisha kwamba ripoti hiyo imependekeza mpango wa elimu mwaka 2015, uzingatie ubora utakaotokana na mipango sahihi inayotekelezeka akitaka tatizo la walimu lipatiwe ufumbuzi wa kudumu kwa lazima ili kuwanusuru wanafunzi.
“Kama suala la walimu halitapatiwa ufumbuzi sasa, tofauti kwenye ufundishaji itakuwepo kwa vizazi vingi huku ikitoa tafsiri mbaya dhidi ya jitihada za kuondoa umaskini duniani na kufikiwa kwa maendeleo endelevu,” alisema Dk Kawambwa.
Aliongeza kuwa kwa namna hali ilivyo sasa, Serikali inalazimika kuhakikisha inaajiri walimu wenye dhamira ya kweli ya kufundisha na kutoa elimu bora.
Ripoti ya Unesco inaeleza kuwa licha ya kuwepo kwa mafanikio ya kuridhisha katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, wananchi masikini ndiyo walioathirika zaidi na tatizo la utoaji elimu mbaya sababu ikiwa kutokuwepo kwa walimu wenye mafunzo ya kutosha.
Unesco ilisema kuwa kutokana na matatizo ya walimu, wanafunzi 130 milioni wanaosoma shule za msingi duniani, hawana uwezo wa kusoma hata sentensi moja, jambo linalowafanya washindwe kujiunga na sekondari.
“Matatizo ya elimu siyo tu yanaathiri malengo ya watoto ya baadaye, lakini pia uchumi wa Serikali hizo. Gharama ya watoto 250 milioni kutosoma elimu ya msingi ni Dola 129 bilioni za Marekani,(Sh 212.85 bilioni), ambayo ni asilimia kumi ya matumizi ya dunia katika elimu,” inasema ripoti hiyo. 
Ripoti hiyo imelinukuu shirikali lisilo la Serikali la Uwezo, linaloeleza kuwa asilimia 26 ya wanafunzi wa darasa la tatu ndiyo wanaoweza kusoma vizuri hadithi ya Kiswahili ya darasa la pili.
Akizungumza na gazeti hili kuhusu takwimu hizo, Mratibu wa Uwezo-Taifa, Zaida Mgalla alisema kuwa asilimia 44 ya wanafunzi wa darasa la tatu walifaulu jaribio la hisabati la darasa la pili, huku asilimia 11 pekee wakifaulu kusoma hadithi ya Kiingereza.
Zaida alisema walimu wamekata tamaa ya kufundisha kutokana na Serikali kushindwa kuwatimizia mahitaji ya msingi, huku pia heshima yao ikishuka mbele ya jamii.
“Walimu hawaheshimiwi, wanapigwa na wanafunzi, mtoto akipigwa na mwalimu anapiga simu polisi waje kumkamata mwalimu. Kwa hiyo walimu wamewasusa wanafunzi na wazazi nao wapo bize na kazi,” alisema Zaida.
Pia alisema wanafunzi hawafundishwi mambo ya msingi kutokana na walimu kutojua kitu wanachofundisha.
Hata hivyo, Unesco imeimwagia sifa Tanzania kwa kuongeza idadi ya wanafunzi  waliomaliza shule ya msingi kati ya mwaka 2000 na 2007, lakini ikasema kuwa asilimia 27 ya wanafunzi hao hawakujifunza mambo ya msingi.
Vijana milioni 175 katika nchi zenye kipato cha chini na cha wastani ambao ni sawa na robo ya vijana duniani, hawana uwezo wa kusoma na kuandika. Katika nchi zilizopo chini ya Jangwa la Sahara, asilimia 40 hawajui kusoma wala kuandika.
“Ripoti inathibitisha kwamba lazima mtoto asome miaka minne ili aweze kujua kusoma na kuandika vizuri; kati ya wale waliosoma miaka minne au chini ya hapo, asilimia 77 hawawezi kusoma sentensi,” inasema ripoti hiyo.
Akisoma hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka 2014/2015 bungeni, Dodoma, Dk Kawambwa alisema kuwa vyuo vya Serikali na umma vimefanikisha upatikanaji wa walimu wapya 36,000 waliohitimu na kuajiriwa.
“Kati ya idadi hiyo, walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ni 2,364, ngazi ya cheti 17,928, ngazi ya stashahada 5,416 na ngazi ya shahada 12, 994.  Ofisi ya Waziri Mkuu - Tamisemi imewaajiri na kuwapanga katika halmashauri mbalimbali nchini, hivyo kuendelea kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la uhaba wa walimu ngazi mbalimbali,” alisema.
Waziri huyo alisema kuwa baada ya ajira ya walimu hao kufanyika, kwa sasa, taifa litabaki na upungufu wa walimu 30, 949 wa shule ya msingi na walimu 24, 596 wa sekondari katika masomo ya sayansi na hisabati.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Emmanuel Mallya alisema kuwa walimu wanashindwa kuwafundisha wanafunzi mambo ya msingi kutokana na kukosa ubunifu wa kutumia mifano iliyopo kwenye jamii husika.
Pia alisema baadhi ya walimu waliingia katika taaluma hiyo baada ya kufeli katika masomo mengine, hivyo hawana uwezo mkubwa wa kuchambua mambo mapya na muhimu kwa wanafunzi hao.
Mallya alisema walimu hawana vifaa vya  kutosha vya kufundishia, kisha akatoa ushauri kwa mwandishi.
“Wewe tembelea shule za msingi kumi, utashangaa kugundua kuwa wanatumia vitabu tofauti kujifunza somo moja, wakati zamani wanafunzi wote tulikuwa tunasoma kitabu cha aina moja,”alisema.

WARSHA YA WAHARIRI YAANZA

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Maimuna Tarishi akifuatilia taarifa za utangulizi wa warsha ya Tanapa na Wahariri wa habari kutoka kwa Shelutete hayupo pichani
Baadhi ya wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakifuatilia taarifa,

Sh6bn drugs seized in 2-and-half years




Intelligence reports suggest that the drug lords have changed their tactics to avoid detection. They now use airports outside Tanzania and recruit more women mules to transport the drugs with the help of middlemen operating in Nigeria and Tanzania. PHOTO/FILE 
By Bernard James The Citizen Reporter

Posted  Sunday, May 25  2014 at  00:00
In Summary
The Citizen on Sunday established that Nigerians topped the list of foreigners nabbed at local airports with drugs. Eighteen were Nigerian and four were Ghanaian.
Dar es Salaam. About Sh6 billion worth of heroin and cocaine has been seized at Tanzania’s major airports in the past two-and-half-years, according to police reports. That haul came from only 56 drug trafficking suspects at Julius Nyerere International Airport (JNIA) and Kilimanjaro International Airport (KIA).
The Citizen on Sunday established that Nigerians topped the list of foreigners nabbed at local airports with drugs. Eighteen were Nigerian and four were Ghanaian.
Intelligence reports suggest that the drug lords have changed their tactics to avoid detection. They now use airports outside Tanzania and recruit more women mules to transport the drugs with the help of middlemen operating in Nigeria and Tanzania.
The foreigners dealing in drugs work with cartels operating principally in East Africa but with a reach as far as China, Brazil, Canada, Japan, the United States and the United Kingdom.
The Brazil connection
Statistics from the Anti-Drugs Unit indicate that the Brazilian city of Sao Paulo has been a major source of cocaine entering Tanzanian through airports, with over 90 per cent sourced there. The travel documents of most of the suspects nabbed in airports also confirm that the drugs are sourced in that city.
Drug dealers who want to ferry huge quantities of drugs appear to prefer KIA for moving the drugs in and out of the country. Not a single suspect who has swallowed drug pellets has been arrested at the airport in two years, unlike those nabbed at JNIA.
Police statistics indicate that 22 traffickers were arrested in 2012, but the number dropped to 17 last year. The trend so far suggests, though, that arrests could double or even triple compared to last year given intensified security checks at all major airports.
Already, 18 people have been caught out at the airports this year, exceeding the total number of suspects arrested last year. This week, anti-narcotics officers at JNIA arrested a 65-year-old Nigerian woman as she attempted to download a large quantity of heroin she had swallowed.
The arrest of Olabisi Ibidum Cole, who had swallowed 82 heroin capsules came a few weeks after President Jakaya Kikwete scolded airport authorities, saying he was not happy with the state of security at key airports.
A visibly annoyed President Kikwete said he was particularly concerned about the continued use of JNIA and KIA as conduits for drug trafficking.
He made the remarks during the laying of the foundation stone for the construction of JNIA Terminal Three, which is expected to significantly expand the capacity of Tanzania’s biggest and busiest airport.
President Kikwete expressed his disgust at how easily drug kingpins were using local airports. “I wonder how drugs go through our airports unnoticed only to be seized outside the country,” he said. “What is it that lacks at our airports? I’m not happy with this situation and how the ministry and the airports authority are handling this issue.”
President Kikwete said he had been directing the relevant officials to improve security at all airports in the country, to no avail.
In the past month, three Tanzanian women and a man have been arrested at Hong Kong airport for drug trafficking. One of the women had swallowed 43 capsules and is reported to have left from JNIA airport. Another, who had 40 pellets, departed from Zanzibar International Airport. They face a minimum of eight years in jail in prison.
Drug dealers seemingly prefer now using the Zanzibar airport to ferry the drugs.
Yesterday, Head of the Anti-Narcotics Unit Godfrey Nzowa said drug dealers are constantly changing their mode of operation but information they receive from local sources and international agencies has helped them keep the traffickers on their toes.
Security checks in the major airports has been tightened to scare off the drug traffickers. “We know their movements more than ever before and we are tracking every step they take,” Mr Nzowa told The Citizen on Sunday. “We are determined to tame the vice and we are on the verge of finishing drug dealers.”