Subscribe:

Ads 468x60px

ASOMEWA MASHITAKA YA KUBAKA NA KULAWITI MTOTO AKIWA WODINI



Novemba 30,2013.
SERENGETI.
MAHAKAMA ya Hakimu wa Wilaya ya Serengeti imelazimika kuhamia hospitali ya wilaya ya Nyerere na kumsomea mashitaka  Marwa Ibrahimu(30)mkazi wa Kijiji cha Matare wilayani hapo,anayekabiliwa na mashitaka mawili  ya kubaka na kulawiti mtoto wa miaka 12.
Hakimu wa Mahakama hiyo Franco Kiswaga alilazimika kuhamia hospitalini hapo kutokana na mtuhumiwa kushindwa kufikishwa mahakamani kufuatia kupigwa na kuumizwa na wananchi walipomkuta anafanya unyama huo .
Mwendesha mashitaka wa polisi Jakobo Sanga akisoma maelezo ya shitaka hospitalini hapo alisema mnamo novemba 19 mwaka huu majira ya saa 2 usiku katika kitongoji cha Bukore kijiji cha Nyichoka kata ya Kyambahi mtuhumiwa anadaiwa kumbaka na kumlawiti mtoto wa miaka 12.
Akisoma hati ya mashitaka alisema kuwa mshitakiwa huyo anakabiliwa na makosa mawili ikiwemo la ubakaji na kulawiti mtoto kinyume cha maumbile ikiwa ni kinyume cha sheria.
Na kuwa mtuhumiwa akijua kuwa ni kosa alimkamata mtoto huyo na kumwingilia kwa nguvu na kumsababishia majeraha sehemu za siri na haja kubwa mtoto huyo.
Mwendesha mashitaka alisema kuwa upelelezi umekamilika,hata hivyo mshitakiwa alikana mashitaka  na hakimu kuamru apelekwe mahabusu atakapopona  hadi desemba 5 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Mwisho.

VYOMBO VYA HABARI VISAIDIE KUELIMISHA JAMII KUHUSU MAAMBUKIZI YA HIV






MEYA WA JIJI LA ARUSHA GAUDENCE LYIMO AKIFUNGUA SEMINA KWA WAANDISHI WA HABARI WA MKOA HUO JUU YA UGONJWA WA UKIMWI.

 ,VYOMBO vya habari nchini,vimeombwa kusaidia Taifa katika vita dhidi
ya ugonjwa wa Ukimwi na unyanyapaa,kwani hivi sasa kumebainika kuanza
maambukizi mapya ya ugonjwa wa ukimwi.

Meya wa jiji la Arusha,Gaudence Lyimo,ametoa  wito huo ,wakati akifungua
semina ya siku moja ya waandishi wa habari,juu ya ugonjwa wa ukimwi na
kupinga unyanyapaa.

Katika semina hiyo,iliyoandaliwa na Taswa Arusha ,chama cha wanaoishi na
vvu mkoa wa Arusha(TUPO) na kampuni ya Ms unique na kudhaminiwa na shirika
la PSI,Mifuko ya hifadhi ya jamii ya PPF,PSPF,NSSF,LAPF na Shirika la
Pingos Forums meya Lyimo,amesema hali ya maambukizi ya vvu ni mbaya.

Amesema  kwa hali ilivyo sasa,ni muhimu vyombo vya habari,kushiriki
ipasavyo katika vita dhidi ya Ukimwi kwani hali sio nzuri.

Na kuwa  kila siku kukiwa na taarifa za HIV katika vyombo vya habari
kutasaidia kukumbusha jamii kuendelea kuchukua  tahadhali

Mapema  Mratibu wa Ukimwi mkoa wa Arusha,Brandina Nkini ametoa taarifa
ya maambukizi ya  HIV yanavongezeka  jijini Arusha kutoka 1.6 mwaka
2007 hadi kufikia3.2 mwaka  2012..

Mwisho.

Plight of Tanzanian journalists with the advent of multipartism


By David Kisanga
28th November 2013




Tanzania electronic, print media doing news coverage
The Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) has completed its country’s security needs assessment survey for human rights, Non Governmantal Organizations (NGOs), and journalists.

According to their findings and what was recorded in the questionnaires distributed, media practitioners working for public media outlets are facing severe hatred from fractions of the citizenry or from supporters of certain political parties.

These have led to commotions during political rallies and in situations where there is a tug of war between the citizenry in one side and the government and investors on the other side.

Given this situation this coalition foreseen of worst scenario as this country is heading towards the 2015 General Elections. Incidents of hurling stones and other forms of humiliations to this group are a common practice according to leaders of the 16 regional press clubs that were visited by this coalition.

Good examples to elucidate this scenario are found in all regions which are strong mainstay of the opposition, or which are endowed with rich reserves of natural resources.

In this category regions like Mbeya, Iringa, Mtwara, Arusha, Kigoma and Dar es Salam have witnessed incidents of humiliating journalists like what happened to the TBC broadcaster Marin Hassani Marin when he was harassed by sympathizers to one of the main opposition parties in the country, when it was launching its presidential candidate in the 2010 General Elections at the Jangwani grounds following a sudden blackout of the national television coverage.

Happenings like these could hinder the work of media practitioners in public media outlets which are run on coffers money.

According to Tanzania Human Rights Defenders-Coalition (THRDC) National Coordinator Onesmo Olengurumwa any sudden blackout of this media outlets have always created a critical risky situation towards these journalists as the public at large tend to assume that it is the journalists who decide what should and should not be aired without any attempt to understand that reporters operate under orders from their managements and editors.

Just to mention a few, Olengurumwa pointed out that a similar blackout of news from the TBC led to the unprecedented violence against the Mtwara based TBC reporter Kassimu Mikongolo in May this year, whose house was set ablaze by the irate mobs condemning him for terminating this coverage deliberately.

He mentioned other similar incidents that also occurred in Arusha, where TBC reporters were sidelined during the Arumeru by-election, and in other rallies by CHADEMA. This has forced them to use stories which have been collected by their colleagues from such rallies.

He mentioned Journalists from public media outlets who faced difficulties as Leonard Manga, Sechela Kongola, Khalfan Mshana and Ben Mwaipaja.

Olengurumwa gave an example of Kigoma where journalists working in public media outlets have a working confidence with leaders from all parties. However, citizens at large do not have trust with such outlets. In Kigoma TBC reporter Dotto Elias once faced a stiff challenge at the CHADEMA rally where he was harassed by its sympathizers. In that occasion CHADEMA’s leaders came to his rescue.

Gervas Msigwa also with TBC has been facing harassments whenever he attends CHADEMA’s rallies he had a narrow escape from an attack during the by-election in Lisabon Songea in 2011.

“There is a need to improve managerial capacity to the runners of these institutions so that they can get well acclimatized to the multiparty era in which this country is now operating.”

The current chairman of the Iringa Press Club Frank Leonard, who is employed by a public media outlet publisher of Daily News and Habari Leo, says there is a problem with politicians who fail to construe journalists as members of the community and that whatever they report reflect people’s wishes.

Citing in the 2010 General Election the ruling CCM top leadership had substituted its candidate who emerged an overall winner and replaced him with the one who happened to be their own choice.

By reporting this discrepancy he was seen as an agent of the opposition so he was confronted by the CCM’s Green Guards on grounds that he was working against their party, at the end of the day the ruling party lost in the Iringa Urban Constituency. 
SOURCE: THE GUARDIAN
More News


ABAKA NA KULAWITI MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI


                                
.

MWANAFUNZI wa darasala tano mwenye umri wa miaka (12) shule ya msingi(Nyichoka)wilayani Serengeti amelazwa katika hospitali ya wilaya akiguza majeraha ya kubakwa na kulawitiwa na mkazi mmoja wa kijiji cha Matare wilayani humo.
Mratibu wa dawati la jinsia la polisi wilaya Wp Sijali Nyambuche amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Marwa Ibrahimu(33) ambaye anadaiwa kutenda unyama huo Novemba 20 majira ya saa 2 usiku katika kitongoji cha Bukore kijiji cha Nyichoka kata ya Kyambahi.
Alisema mtuhumiwa huyo ambaye wanamshikilia alimfanyia ukatili(jina limehifadhiwa)baada ya kumkamata kwa nguvu na kumchania nguo zake  za siri  .
“Siku ya tukio mtuhumiwa ambaye anafanya kazi kwenye roli la kusomba mawe,walifika kijijini hapo ili kununua mawe na mchanga…mtoto huyo alikuwa na mawe aliyokusanya kwa ajili ya kuuza apate fedha za mahitaji yake ya shule…gari liliharibika wakashindwa kuondoka na kulazimika kulala….ndipo usiku akamfanya ukatili huo”alisema mratibu wa dawati.
Nyambuche alisema kuwa kabla ya kumfanyia unyama huo usiku mtuhumiwa aliombwa kuwa mlinzi wa gari hilo na kusindikizwa na  mtoto huyo kuelekea kwenye gari,ghafla akamkamata na kumwingiza ndani ya gari na kumtendea unyama huku akimtishia kumuua.
“Tulimpkea mtoto huyo na kumpeleka hospitali kwa matibabu baada ya kupata PF3 kwa ajili ya matibabu  na uchunguzi zaidi ili kubaini amejeruhiwa kiasi gani na kama amepata magonjwa ya zinaa”alisema Nyambuche.
Akiongea kwa kusita sita mtoto huyo alisema baada ya kufika kwenye gari mtuhumiwa alimlazimisha kupanda ndani ya gari,alipokataa  akanishika kwa nguvu na kumpandisha ndani ya gari  akafunga mlango na kuchana nguo zake za  ndani na kuanza kumlawiti na baadae kumbaka na kuchanika sehemu zote na damu pamoja na kinyesi kutoka mfululizo.
“Nilipochelewa kurudi nyumbani usiku huo mama alniifuatilia…nilipomsikia nilimwita nikilia…akamkuta  mtuhumiwa akiendelea kunifanyia maneno ya aibu..akapiga yowe wananchi wakajitokeza na kuanza kumpa kipigo mtuhumiwa na kumpeleka polisi.”alisema.
Waganga katika hospitali ye Nyerere wamesema hali ya motto huyo inaendelea vizuri na polisi wanasema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote.
Matukio hayo yanatokea ikiwa wanaharakati wametawanyika nchi nzima katika kampeini za siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.      
MWISHO.

MATUKIO YA UZINDUZI WARIPOTI YA TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFENDERS

 BAADA YA KUZINDUA RIPOTI PICHA ZA PAMOJA ZIKAPIGWA
 MGENI RASMI JAJI MKUU WA TANZANIA OTHMAN CHANDE KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAJUMBE WA THRDS WALIOSHIRIKI UZINDUZI WA RIPOTI YA HALI HALISI ILIVYO KWA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU NA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA
PICHA YA PAMOJA

RIPOTI YA TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFENDERS COALITION YAZINDULIWA

 JAJI MKUU WA TANZANIA OTHMAN CHANDE AKIZINDUA RIPOTI YA TANZANIA HUMAN RIGHTS DEFENDERS COALITIONS UKUMBI WA HOTELI YA KEMPISKI DAR ES SALAAM
 MRATIBU WA MTANDAO WA THRDS ONESMO OLENGURUMWA AKIMKABIDHI JAJI MKUU RIPOTI YA MTANDAO HUO .
 MWENYEKITI WA MTANDAO HUO BI MARTINA KABISAMA AKIWA PAMOJA NA VIONGOZI WENGINE WAKATI WA KUFUNGUA RIPOTI YAMTANDAO HUO

 JAJI MKUU WA TANZANIA OTHMAN CHANDE KATIKA PICHA YA PAMOJA NA VIONGOZI WA MTANDAO WA THRDS,MABALOZI NA WADAU WENGINE MARA BAADA YA KUZINDUA RIPOTI HIYO
BAADA YA UZINDUZI  WA RIPOTI KILA MMOJA NI FURAHA TU

ANG’ATWA NA SIMBA

 Novemba 24,2013

Serengeti:MKAZI  mmoja wa kijiji cha Rwamchanga kata ya Manchirawilayani Serengeti Jimoka Nyihocha (20)amenusurika kufa baada yakuvamiwa na Simba katika zoezi la kuwaua baada ya kuvamia kijijinihapo na amelazwa hospitali ya wilaya ya Nyerere.
Tuko hilo limethibitishwa na afisa maliasili na wanyama pori wilaya
John Meitamei ,diwani wa kata hiyo na uongozi wa hospitali ya wilayalimetokea novemba 21 majira ya saa 6 mchana katika eneo la Bwawa laManchira.
Afisa Maliasili na wanyama pori Meitamei alisema Nyihocha alijeruhiwabaada ya wananchi kufuatilia nyayo za Simba waliodaiwa kupita kijijinina kuwakuta katika kichaka eneo la bwawani wakiwa wawili,na katikapurukushani hizo mmoja akakimbia na aliyebaki ndiye akaleta madhara
hayo.
“Baada ya wananchi kumzingira ili wamuue baada ya jike kukimbia hilodume lilianza kuwatisha …ghafla likatoka kichakani na kumvamia huyokijana na kumng’ata matakoni na kwenye paja,lakini wananchi kwa kuwawalikuwa wengi wakasaidia akakimbia na kurudi kichakani”alisema.
Alisema askari wa halmashauri kwa kushirikiana na mapori ya Ikorongona Grumeti walifika eneo la tukio na kuanza kukabiliana na simba huyokwa muda mrefu ,na kufanikiwa kumuua.
“Toka saa sita hadi saa kumi ndio tukafanikiwa kumuua…maana alikuwaeneo baya kwenye kichaka na kuingia haikuwa kazi rahisi…alipopigwarisasi akaruka kuja kumvamia askari…wakamuwahi na kumpiga risasi yapili na kufa…vinginevyo angeleta madhara mengine”alisema.
Hata hivyo alisema wanaendelea na msako wa simba aliyekimbia asije akaleta madhara kwa wananchi na mifugo.
Diwani wa kata hiyo Marko Shaweshi alisema kijana huyo alishambuliwana Simba wakati anajaribu kukimbia”Simba huangalia mtu mwoga na hakuwana uzoefu…mara baada ya kuunguruma akajaribu kukimbia,hilo ni kosa kwasimba kumtega mgongo akamvamia…kama watu wasingewahi angemuua”alisema.
Alisema kukithiri kwa wanyama katika makazi ya wananchi ni kutokana nahali huko ndani kuwa ngumu ya kupata mawindo na chakula hivyohukimbilia maeneo ya watu ili kujipatia chakula.
Muuguzi mkuu wa hospitali hiyo Neema Mechara amesema majeruhi huyoaliyelazwa kitanda namba moja wodi ya wanaume anaendelea vizuri na ameanza kufanya mazoezi baada ya kusafishwa vidonda na mifupa
haikupata madhara.
Mwisho.

AFA KWA KUJINYONGA BAADA YA KUTISHIWA NA BABA YAKE.


Aliambiwa akimuua ndama aliyekuwa ana mpiga atakula nyama yake mbichi,
Novemba 24,2013
Serengeti:
JULIANA MARWA(14)mkazi  wa kijiji cha nyamakendo katika wilaya ya serengeti mkoani mara amejinyonga  hadi kufa kwa kutumia kamba ya katani baada ya kutishiwa na baba yake mzazi kuwa akimuua ndama aliyekuwa anampiga atakula nyama yake mbichi.
Tukio hilo ambalo limeacha maswali mengi kwa wananchi limethibitishwa na diwani wa kata hiyo Samweli Gibewa na polisi wilayani kuwa limetokea mwanzoni mwa mwezi huu katika kitongoji cha Bwisabuka kijijini hapo.
Alisema siku ya tukio majira ya saa 12.00 jioni msichana huyo akiwa anakamua maziwa ndama alikuwa anamsumbua kwa kutaka kunyonya ndipo akaanza kumpiga ,kitendo kilichomuudhi baba yake na kumtolea maneno kuwa  akifa atamla mbichi,kauli inayodaiwa kumuudhi na kuamua kwenda kunjinyonga.
“Alikutwa ndani ya shamba la mihogo mita 100 kutoka nyumbani kwao majira ya saa 1:00 asubuhi kesho yake kwa kuwa baada ya kugombezwa alitoweka kwao….Mama yake alipokwenda shambani kupalilia ndipo akamkuta ana ning’inia ameishakata roho na kulazimika kupiga kelele kuomba msaada”alisema diwani.
Mama mzazi wa marehemu  Mugosi Marwa akielezea tukio hilo alidai kuwa baada ya binti huyo kutoelewana na baba yake alitoweka nyumbani majira ya usiku  wakidhani ameenda kulala  kwa bibi yake ambaye wanaishi jirani hivyo hawakuwa na sababu ya kumfuatilia wakijua kuwa atarudi asubuhi mwenyewe kinyume chake akaenda kujinyonga.
Hata hivyo Marehemu hakuacha ujumbe wowote kuhusiana na uamzi wake wa kujinyonga ,jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi  kuhusiana na tukio hilo  baada ya kuhoji familia akiwemo baba mzazi Marwa Mwita Yahara.
Mwisho.

WANASHERIA(AG)KENYA,UGANDA NA RWANDA WAFUNGULIWA MASHITAKA MAHAKAMA YA A.MASHARIKI



 Wakili Jimmy Obedi kushoto akiwasilisha maombi ya kufungua kesi katika mahakama ya Afrika Mashariki kuitaka mahakama hiyo itoe amri ya kusitisha utekelezaji wa maazimio ya vikao vitatu vilivyoshirikisha Uganda,Kenya na Rwanda kwa kuwa ni ukiukwaji wa vifungu vya sheria ya jumuiya hiyo,anayepokea ni afisa wa masijala ya mahaka hiyo Richard Ogoti kwa niaba ya msajili wa mahakama hiyo




 Wakili Jimmy Obedi mwenye miwani akipokea hati maalum kutoka kwa karani wa masijala wa mahakama ya Afrika Mashariki Richard Ogoti mara baada ya kuwasilisha maombi na kufungua kesi namba 9/2013 iliyofunguliwa na watu watatu(picha zote na Blog hii)


WAFUNGUA KESI MAHAKAMA YA A.MASHARIKI
Novemba 18,2013

Arusha-
WANASHERIA wakuu wa nchi  za Kenya,Rwanda na Uganda wamefunguliwa mashitaka katika Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutokana na kukiuka vifungu vya Mkataba wa jumuiya hiyo.

Maombi namba 6 kesi namba 9/2013 imefunguliwa na wanajumuiya hiyo Ally Msangi,David Makata na John David Mbendo wanaowakilishwa na wakili Jimmy Obedi wa kampuni ya Jimmy Obedi ya jijini Dar es salaam imepokelewa leo na afisa masijala wa mahakama hiyo

Boniphace Ogoti  kwa niaba ya msajili.

Mbele ya waandishi wa habari wakili Obedi amesema wamewasilisha maombi ya kutaka maazimio yote ya vikao vilivyofanyika juni 24,25 mwaka huu Entebe Uganda,kikao cha agosti 28,2013 Mombasa na oktoba 28,2013 Kigali Rwanda bila kushirikisha nchi mwanachama ambaye ni Tanzania.

“Lengo la maombi haya ni kuzuia utekelezaji wa maamzi yaliyofikiwa kwenye vikao hivyo kwa kuwa ni kinyume na vifungu vya mkataba wa jumuiya,ibara ya 71(f)71(b) na vingine….mahakama itoe amri ya kusitisha vikao vyote vinavyoendeshwa kinyume cha sheria ya jumuiya .... tumeomba maombi hayo yasikilizwe upande mmoja na kutoa uamzi wa kusitisha utekelezaji huo”amesema wakili.

Wakili huyo amesema wakati kesi hiyo ikisubiri kupangiwa jaji watu wengine kutoka katika jumuiya hiyo wanaruhusiwa kujiunga na walalamikaji hao ,kwa nia ya kuhakikisha mkataba wa shirikisho hilo unafuatwa kwa mjibu wa  vifungu vya sheria iliyounda shirikisho hilo.
.
“Hapa walalamikiwa ni wanasheria wakuu wan chi hizo tatu ambao marais wao wamekuwa wakikutana kinyume cha mkataba wa shirikisho la jumuiya ya Afrika Mashariki….na sisi tunataka sauti ya kimahakama ya kusitisha utekelezaji wa maazimio yao… mahakama ndio chombo kikuu kitakachotoa tafsri si siasa tena…amebainisha wakili.

Kwa upande wake Msangi ambaye amewakilisha walalamikaji wenzake mahakamani hapo amesema kuwa wamefikia uamzi huo ili kupata ufafanuzi wa kisheria kwa kuwa taarifa zinazotolewa na wanasiasa zinawachanganya wananchi wan chi zote ili kujua hatima ya shirikisho hilo.
mwisho. 

Marekani yaiweka pabaya Tanzania, yaiita kitovu cha ‘biashara’ ya binadamu



Na Goodluck Eliona, Mwananchi

Posted  Ijumaa,Novemba15  2013 
Kwa ufupi
  • Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.

Dar es Salaam. Marekani imetoa ripoti inayozungumzia usafirishaji wa binadamu ya mwaka 2013, huku ikiitaja Tanzania kuwa kinara wa kunyanyasa wasichana, kuwatumikisha katika ngono na usafirishaji wa binadamu.
Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa Julai  mwaka huu   na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Seneta John Kerry inaweka bayana kwamba biashara ya usafirishaji wa binadamu hufanywa na baadhi ya ndugu na marafiki ambao hutoa ahadi kwa wahusika kwamba wanakwenda kuwasomesha au kuwatafutia ajira nzuri mijini.
“Unyonyaji wa wasichana wadogo na utumikishaji majumbani ndilo tatizo linaloongoza, ingawa kesi za watoto kusafirishwa kwa ajili ya biashara ya ngono katika mpaka wa Tanzania na Kenya zinaongezeka. Pia, wasichana wananyonywa kwenye maeneo ya utalii,” inasema sehemu ya ripoti hiyo.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, watoto kutoka Burundi na Kenya, watu wazima kutoka Bangladesh, Nepal, Yemen na India wanatumikishwa kufanya kazi kwenye sekta za kilimo, madini na majumbani nchini Tanzania.
“Baadhi ya raia kutoka nchi  jirani huingia Tanzania kwa hiari yao, lakini hulazimishwa kufanya kazi majumbani kabla ya kupelekwa kutumikishwa kwenye biashara ya ngono Afrika Kusini, Ulaya na Mashariki ya Kati,” inaeleza.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki alimtaka mwandishi kumtumia ripoti hiyo kwa njia ya baruapepe ili aweze kuisoma na kuitolea maelezo.
Alipotafutwa siku ya pili, alisema kuwa ameipokea na kuikabidhi ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) ili ifanyiwe kazi na baadaye kutoa majibu.
“Ripoti niliipata nikaikabidhi ofisi ya DPP kwa kuwa wao ndio wanaoweza kuitolea maelezo baada ya kuisoma. Maoni yangu lazima yawe ya kitaalamu siwezi kusema bila kupata taarifa kutoka kwao,” alisema.
Lawama kwa Serikali
Ripoti hiyo inaitupia lawama Tanzania kwa kutokuwa na sheria thabiti za kupambana na biashara haramu ya kusafirisha binadamu, huku ikitolea mfano namna ilivyoshindwa kuwasaidia raia wake waliokuwa wakinyanyaswa nje ya nchi.
“Kamati ya Serikali ya kupambana na usafirishaji binadamu, haijachukua hatua za kutosha katika kutekeleza mpango mkakati wa kupambana na vitendo hivyo,” inaeleza na kuongeza:
“Serikali imeshindwa kutenga fedha kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa usafirishaji wa binadamu kama ambavyo inaelekezwa kwenye sheria ya kudhibiti biashara hiyo ya 2008.”
Taarifa hiyo inaitaka Tanzania kuongeza nguvu katika kutekeleza sheria ya kudhibiti biashara ya kusafirisha binadamu ya 2008 kwa kuwakamata na kuwashtaki wahusika wote, lakini ikaikosoa kwa kusema inatoa adhabu ndogo kwa mtu anayebainika kufanya makosa, ikiwa ni pamoja na kumhukumu kwenda jela miaka 10, kulipa faini au vyote viwili kwa pamoja.
“Sheria hiyo haifanani na nyingine kama za mtu anayepatikana na kosa la kubaka au kufanya kosa jingine la jinai. Mamlaka imesema ina kesi nne inazozichunguza, saba zipo mahakamani toka mwaka jana, zikiwepo mbili mpya,” inasema ripoti.
Pia, Serikali ya Tanzania imelaumiwa kwa kushindwa kuripoti maendeleo ya uchunguzi wa maofisa wake waliotuhumiwa kujihusisha na biashara ya usafirishaji binadamu.
LHRC na TGNP
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema tatizo la usafirishaji wa binadamu pia linachangiwa na wasichana kuwa na tamaa ya maisha mazuri, hivyo kukubali ahadi ambazo hupewa kwamba wanapelekwa kusoma, wasifahamu  wanarubuniwa.
“Wengi wanatamani kwenda ‘majuu’ wakidhani watapata elimu, lakini baadaye wanaingizwa kwenye vitendo vinavyowafedhehesha na kuwafanya wakate tamaa kabisa,” alisema.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Usu Mallya alisema katika siku za karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wasichana waliochukuliwa vijijini kwenda mijini kufanya kazi.
Alisema pamoja na tatizo hilo kuongezeka hapa nchini, hakuna tafiti za kutosha ambazo zimefanywa na wadau mbalimbali kuonyesha madhara yaliyopatikana hadi sasa.
“Katika siku za usoni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya kunyimwa chakula, kupigwa na kufukuzwa kazi huku wasichana wengine wakitumika kwenye biashara ya ngono,” alisema na kuongeza:
“Ripoti hii isiishie kwenye makabrasha bali  ifanyiwe kazi ili jamii yote ijue kuwa hili ni tatizo.”
Ripoti hiyo inabainisha kuwa watu 47,000 pekee ndio walioweza kuokolewa mwaka jana kutoka kwenye mazingira ya utumikishwaji kati ya milioni 27 waliopo katika hali hiyo duniani.
Tanzania imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi 44 ambazo zinajaribu kupambana na biashara hiyo, lakini hali inazidi kuwa mbaya zaidi.

ELIMU ,WAZAZI WANAWAJIBIKA KUFUATILIA MAENDELEO YA WATOTO WAO

 WAZAZI WAKILA PAMOJA NA WATOTO WAO KATIKA SHULE YA TWIBHOKI WILAYANI SERENGETI
 HAO NI WILBROADS NA ALICE ANTHONY WAKIWA TWIBHOKI
 HAWA NI FRANSISCA NA ALICE ANTHONY KATIKA MAZINGIRA YA SHULE
HAPO NI MSOSI NA KUULIZANA MAENDELEO YA TAALUMA KATI YA WAZAZI NA WANAFUNZI.

Kijazi awapa somo wabeba mizigo Kilimanjaro



  


na Grace Macha, Moshi

   





MKURUGENZI Mkuu wa Hifadhi za Taifa nchini, (TANAPA), Allan Kijazi, amewataka wapagazi wanaosaidia kubeba mizigo ya watalii kwenye  Mlima Kilimanjaro kuhakikisha wanatunza mazingira ya mlima huo kwani ukiharibika na wao wataathirika kwa kukosa ajira.
 Aidha, alisema atawasiliana na wadau wa utalii ili kuona namna ya kuboresha utendaji wao kwa kuwatafutia ziara ya mafunzo kwenye moja ya nchi zenye milima mirefu.
 Aliyasema hayo jana wakati akifungua kongamano la kwanza la Chama Cha Wapagazi nchini (TPO) lililofanyika kwenye ukumbi wa YMCA ambalo lilikuwa likijadili changamoto wanazokabiliana nazo na namna ya kuzitatua.
 Kijazi alisema kuwa kwenye kongamano lao hilo mbali ya kujadili changamoto zinazowakabili ni vema wakaangalia namna ya kuutunza mlima huo ambao unawapatia ajira.
 “Kuna malalamiko yanakuja kuwa wakati mwingine nyie mnaacha taka huko mlimani kwa kushindwa kuzikusanya vizuri, ni vema mkautunza mlima huu kwani ukipoteza sifa na hadhi yake wageni wataacha kuja na nyie mtakosa ajira,” alisisitiza mkurugenzi mkuu huyo wa Tanapa.
Aliwataka viongozi wa TPO kujenga mfumo wa kufuatilia mienendo ya wanachama wao ili kuona kama wanafuata taratibu na maadili waliyojiwekea, kwani kuna wakati yanaibuka malalamiko kuwa kuna baadhi ya wapagazi si waaminifu na wengine hawazingatii uvaaji sahihi, jambo linalohatarisha usalama wa afya zao.
 Kijazi alisema kuwa anaangalia uwezekano wa kukutana na wadau wa utalii wanaoendesha shughuli kwenye mlima huo wakiwemo Chama cha Waongoza Watalii kwenye mlima huo, KIATO, na Wizara ya Maliasili na Utalii ili waweze kuona namna sheria zilizowekwa hasa kwenye udhibiti wa uzito wa mizigo zitakavyosimamiwa kwa ukaribu zaidi.
 Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri, TPO, Richard Kessy, alisema changamoto kubwa zinazowakabili wapagazi ni kampuni za uwakala wa utalii  kubebeshwa mizigo mizito zaidi ya kiwango kilichowekwa na Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) ambacho ni kilogramu 20.
 “Wapagazi wakiwa huko mlimani kuna wengine wanapewa chakula mara moja kwa siku, wengine wanapewa mara mbili lakini kidogo sana ukinganisha na kazi ngumu ya kubeba mizigo yao na ya watalii wanayoifanya,” alisema Kessy.
 Naye Mwenyekiti wa TPO, Philip Mbise, alisema kuwa wana wanachama 2,820, ambapo kongamano hilo la siku moja limehudhuriwa na wapagazi 250 kutoka mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

WAZOA TAKA MJI MDOGO WA MUGUMU SERENGETI HATARINI KUAMBUKIZWA MAGONJWA YA MLIPUKO

 MIKAKATI MIZURI YA MAMLAKA YA MJI MDOGO WA MUGUMU WILAYANI SERENGETI KUONDOA TAKA MJINI,ZINAELEKEA KUSABABISHA MADHARA KWA VIBARUA HAO KUTOKANA NA MAMLAKA HIYO KUTOWAPA VIFAA MAALUM VYA KUJIKINGA WAFANYAPO HIYO KAZI,AMBAPO BAADHI WANASHIKA UCHAFU BILA VYOMBO VYA KUJIKINGA
 VIBARUAWAKIWA KAZINI,HATA HIVYO WANALALAMIKIAUJIRA MDOGO UKILINGANISHA NA KAZI WAIFANYAYO.




MAMA HUYO HANA GLOVUS LAKINI ANAENDELEA NA KAZI KATIKA MAZINGIRA HATARISHI

Matokeo darasa la saba; Ufaulu waongezeka



 Na Fredy Azzah, Mwananchi

Posted  Jumapili,Novemba3  2013 
Kwa ufupi
  • Matokeo hayo yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde aliyesema ufaulu huo ni ongezeko la asilimia 19.89 ikilinganishwa na mwaka jana.
Dar es Salaam. Zaidi ya asilimia 50 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba Septemba mwaka huu, wamefaulu.
Matokeo hayo yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde aliyesema ufaulu huo ni ongezeko la asilimia 19.89 ikilinganishwa na mwaka jana.
Alisema jumla ya watahiniwa 844,938 walifanya mtihani huo na kati yao 427,606 sawa na asilimia 50.61, wamefaulu kwa zaidi ya alama 100 kati ya 250.
Dk Msonde alisema kati ya watahiniwa hao waliofaulu, wasichana ni 208,227 sawa na asilimia 46.68 na wavulana ni 219,379 sawa na asilimia 55.01.
Matokeo hayo pia yanaonyesha kuwa, wanafunzi wengi wamefanya vibaya zaidi kwenye somo la Hisabati huku wakifanya vizuri kwenye somo la Kiswahili.
Dk Msonde alisema wavulana wamefanya vizuri zaidi kwenye mtihani huo ukilinganisha na wasichana.
Alieleza pia kuwa, mwaka huu udanganyifu kwenye mtihani huo umeshuka kwa kiasi kikubwa, kwani waliofutiwa matokeo ni 13.
Dk Msonde alisema kati ya hao, watano walibainika kukariri mtihani huo jambo ambalo kisheria hawaruhusiwi na wengine walikamatwa na karatasi za majibu kwenye vyumba vya mtihani.
Ufaulu
Alisema miongoni mwa waliofaulu, wenye ulemavu ni 476, kati yao wasichana wakiwa ni 219 sawa na asilimia 46.01 na wavulana ni 257 sawa na asilimia 53.99.
Dk Msonge alisema kuwa, mwaka 2012 watahiniwa waliopata zaidi ya alama 100 walikuwa ni asilimia 30.72, hivyo mwaka huu kuna ongezeko la asilimia 19.89.
Kuhusu sababu za ongezeko la ufaulu, Dk Msonde alisema baraza bado halijafanya tathmini ya kubaini chanzo cha ongezeko hilo.
isi tulicholetewa ni kile kilichofanyika kwenye chumba cha mtihani na haya hapa ndiyo majibu yake,” alisema Dk Msonde.
Ufaulu kimasomo
Alisema mwaka huu ufaulu kwa masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya sita mpaka 28.06, ikilinganishwa na mwaka 2012.
Somo ambalo watahiniwa wengi wamefanya vizuri ni Kiswahili ambalo ufaulu wake umefikia asilimia 69.62 na walilofeli zaidi ni Hisabati ambalo ufaulu wake ni asilimia 28.62.
Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 2012 ufaulu kwenye somo la Kiswahili ulikuwa ni asilimia 41.00 na Hisabati ulikuwa ni asilimia 18.74.
Kwenye somo la Kiingereza ufaulu mwaka huu ni asilimia 35.52 wakati mwaka jana ilikuwa ni asilimia 21.06, huku kwa Sayansi mwaka huu ufaulu ukiwa ni asilimia 47.49 na mwaka jana ilikuwa ni asilimia 41.48 na Maarifa ya Jamii mwaka huu ufaulu ni asilimia 53 na mwaka jana ilikuwa asilimia 28.61.
Usahihishaji wa mashine ni bora zaidi
Alisema ili kujiridhisha na usahihishaji wa kutumia Mashine Maalumu za OMR (Optical Mark Reader), sampuli 20,795 za karatasi za majibu ya watahiniwa wa shule 200 kutoka wilaya 48 za mikoa tisa ya Iringa, Kagera, Shinyanga, Manyara, Njombe, Mbeya, Morogoro, Katavi na Tanga zilisahihishwa kwa mkono.
Alisema baada ya kufanya ulinganifu wa usahihi wa karatasi zilizosahihishwa kwa mkono na zile zilizosahihishwa kwa mashine, ilibainika kuwa zile zilizosahihishwa kwa mashine zilikuwa na usahihi wa hali ya juu.
“Usahihishaji wa kutumia kalamu ulikuwa na makosa machache ya kibinadamu, makosa hayo yalikuwa ya kukosea kusahihisha swali kwa kutumia mwongozo wa usahihishaji na dosari za kujumlisha alama,” alisema Dk Msonde.
Alibainisha kuwa, kati ya sampuli za karatasi za watahiniwa 20,795 zilizosahihishwa kwa mkono, 249 sawa na asilimia 1.2 ndizo zilizobainika kuwa na makosa aliyosema ni ya kibinadamu.
Mbali na usahihi wa usahihishaji, alisema pia mfumo huo umesaidia kupunguza wasahihishaji kutoka 4,000 waliokuwa wakitumika awali na kufikia 301 waliofanya shughuli hiyo mwaka huu.
Alibainisha pia kuwa, OMR imepunguza siku za kusahihisha mtihani huo kutoka 30 za awali mpaka 16 zilizotumika mwaka huu.
Waliofanya mtihani
Alisema watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani huo walikuwa ni 867,982 wakiwamo wasichana 455,896 sawa na asilimia 52.52 na wavulana 412,087 sawa na asilimia 47.48.
Alieleza kuwa, kati ya watahiniwa hao walikuwemo wenye ulemavu wa kuona, 597 walikuwa na uono hafifu na wengine 88 ni wasioona.
“Watahiniwa 844,938 sawa na asilimia 97.34 ya waliosajiliwa walifanya mtihani huo. Wasichana walikuwa 446,115 sawa na asilimia 99.85 na wavulana walikuwa 398,823 sawa na asilimia 96.78,” alisema Dk Msonde.
Alisema kuwa, watahiniwa ambao walisajiliwa na hawakufanya mtihani huo ni 23,045 sawa na asilimia 2.66, kati yao wasichana wakiwa 9,781 sawa na asilimia 2.15 na wavulana 13,264 sawa na asilimia 3.22.
Alieleza kuwa utoro na ugonjwa ni miongoni mwa sababu za wanafunzi hao kutofanya mtihani huo.
Lengo la BRN halijafikiwa
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa akizungumza katika warsha ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN-Big Results Now), kwenye sekta ya elimu iliyotolewa kwa watendaji wa elimu ngazi ya kanda, mkoa na wilaya, Agosti 14, mwaka huu, alisema moja ya lengo la mpango huo ni ufaulu kwa darasa la saba mwaka huu kufikia asilimia 60 kutoka 31 ya mwaka jana.
“Katika kutekeleza vipaumbele hivyo, kila mmoja wenu atakuwa na eneo la kutekeleza na atapimwa kutokana na utekelezaji katika eneo lake, hii ni katika kuhakikisha kuwa kuanzia mwaka huu ufaulu katika elimu ya msingi unaongezeka kutoka asilimia 31 hadi kufikia 60,” alisema Dk Kawambwa.
Mara baada ya Dk Kawambwa kutangaza suala hilo, baadhi ya wadau walisema itaongeza hali ya kupata matokeo yasiyo halisi kwani hakukuwa na muda wa kuandaa mikakati ya kufikia lengo hilo, kwani mpango huo ulitangazwa Agosti na Septemba watoto wa darasa la saba walikuwa wanaanza mitihani.

Kenyan MPs pass harsh media law


The East Africa News

Kenyan Parliament during a past session. Kenyan MPs have passed a new draconian media law that imposes harsh penalties on Journalists 
By John Ngirachu, The Citizen

Posted  Saturday, November 2  2013 
In Summary
  • Journalists now face punitive measures for violating the Code of Conduct for journalists, including fines of up to Sh20 million.
Nairobi. Kenyan parliament has passed a new draconian media law that imposes harsh penalties on journalists.
Journalists now face punitive measures for violating the Code of Conduct for journalists, including fines of up to Sh20 million.
They also risk being deregistered and their bank accounts frozen.
MPs Thursday evening voted to create a tribunal that will handle complaints against the media and have power to impose the harsh penalties.
This happened through the introduction of a surprise change to the Kenya Information and Communication Bill, which was passed last evening with 17 per cent of MPs (60) present in the chambers in the National Assembly.
The House accepted a proposal by the Energy, Information and Communication Committee for the creation of Communications and Multimedia Appeals Tribunal.
The Tribunal would have the power to “impose a fine of not more than Sh20 million on any respondent media enterprise…adjudged to have violated either that law or the Code of Conduct for the Practice of Journalism.”
It has the power to fine individual journalists “not more than Sh1 million” for violating the same code.
It would also get worse because the fine would be a debt, meaning the person or organisation found to have broken the law would be liable to have his bank accounts raided or their property sold off for misreporting.
The tribunal also has the power to “recommend the suspension or removal from the register of the journalist involved.”
It has also been granted the power to make any orders it feels would be necessary to carry into effect the orders or directives it would make. Proposed by Energy Committee chairman Jamleck Kamau, the creation of this tribunal was among amendments introduced with a mere 28 MPs in the chambers.
Only a handful shouted aye when the vote was called for but the fact that there was no one in opposition was taken as evidence that all were in agreement.
As they were going through the amendments, Majority Leader Aden Dualle and Mr Kamau detected that the Bill was not going to be passed without the quorum of 50 MPs and they rushed out to get the rest to come in.
“This is a controversial and good law but the members are not here. This House is more full when passing other Bills,” Mr Dualle would later say.
After that, the 32 who hadn’t been in the House came in and helped bring the numbers up to 60 and then Speaker Justin Muturi called for the verbal vote, the ayes had it and the Bill was passed.

MIKAKATI YA MATOKEO MAKUBWA SASA


BRN imezinduliwa agosti 14 mwaka  huu.
 1. Upangaji wa shule kwa ubora wa matokeo ya mtihani kitaifa kuanzia shule iliyoongoza hadi ya mwisho. Lengo la mkakati huu ni kuongeza uwajibikaji na ushiriki wa jamii katika usimamizi wa utoaji wa elimu bora.

2. Utoaji wa tuzo kwa shule zilizofanya vizuri. Utaratibu wa kutoa tuzo kwa shule utatoa motisha kwa shule kuongeza bidii na kutoa matokeo bora zaidi.

3. Kuwa na kiongozi cha usimamizi wa shule. Mkakati huu utasaidia kuimarisha utendaji wa shule kwa kuwawezesha viongozi wa shule kutekeleza majukumu yao kikamilifu

4. Upimaji wa kitaifa wa stadi za kusoma, kuandika, kuhesabu. Lengo la mkakati huu ni kuhakikisha wanafunzi wanamudu stadi msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu katika madarasa ya chini ya elimu ya msingi kabla ya kujiunga na madarasa yanayofuata

5. Utoaji mafunzo kwa walimu kuhusu ufundishaji mahiri wa stadi za KKK. Lengo la mkakati huu ni kuwawezesha walimu kumudu ufundishaji wa stadi za KKK katika darasa la kwanza na la pili. Mafunzo atatolewa kwa walimu kutoka shule 6,167 za halmashauri 40.

6. Programu ya kujenga uwezo wa walimu na wanafunzi katika ufundishaji na kujifunza-Students Teachers Enrichment Program (STEP). Mkakati huu utajenga utamaduni wa kuwabaini wanafunzi wenye kuhitaji msaada katika kujifunza. Aidha, utoaji mafunzo ya walimu kwa ajili ya utekelezaji yanalenga kumpa mwalimu nyenzo na uwezo zaidi wa kufundisha na kubaini na kuzingatia maeneo yenye changamoto kwa wanafunzi.

7. Ujenzi wa miundombinu muhimu ya shule. Lengo la mkakati huu ni kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia na upatikanaji wa vifaa muhimu shuleni.

8. Utoaji ruzuku ya uendeshaji wa shule. Utekelezaji wa mkakati huu utawezesha uboreshaji wa upatikanaji vitabu vya kiada na vifaa vya kufundishia na kujifunzia shuleni.

9. Utoaji wa motisha kwa walimu. Mkakati huu utawezesha kuwatambua walimu, kutatua changamoto zinazowakabili na kuwapa motisha za kifedha na zisizo za kifedha kwa kujali maslahi na madai yao ya kimsingi.

Wasomi wadai mabadiliko mitihani ya sekondari ni siasa tu




Na Fredy Azzah, Mwananchi

Posted  Novemba2  2013 
Kwa ufupi
  • Baadhi ya wadau hao wakizungumza na gazeti hili jana, walisema Tanzania imeweka rekodi kwa nchi za Afrika kwa kuwa na kiwango kidogo sana cha ufaulu cha alama F kuanzia 0 mpaka 19.

Dar es Salaam. Siku moja baada ya Serikali kutangaza kupunguza viwango vya ufaulu kwa mtihani ya kidato cha nne na sita, baadhi ya wasomi na wadau wa elimu wameponda uamuzi huo na kusema una malengo ya kisiasa.
Baadhi ya wadau hao wakizungumza na gazeti hili jana, walisema Tanzania imeweka rekodi kwa nchi za Afrika kwa kuwa na kiwango kidogo sana cha ufaulu cha alama F kuanzia 0 mpaka 19.
Walisema, Serikali imechukua uamuzi huo kisiasa ili kuhakikisha kuwa, wanatimiza lengo la Mpango wa Maendeleo Makubwa Sasa (BRN), ambalo ni kuhakikisha matokeo ya ufaulu kwa Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu yanafikia asilimia 60 kutoka 33 ya mwaka jana.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Herme Mosha alisema kuwa kilichofanywa na Serikali ni kupanua wigo wa watu kufaulu.
“Wanataka watu ambao walikuwa wanapata daraja la nne wapate daraja la tatu, daraja la tatu wapate la pili na la pili wapate la kwanza.
Hata hivyo, kwa muda wote, wadau wa elimu ambao wanataka siyo kuona tu watu wanafaulu, wanataka elimu iliyo bora. Kwa hatua hii waliyoichukua haitasaidia lolote katika kuongeza ubora wa elimu ambao umekuwa kilio cha muda mrefu,” alisema Profesa Mosha.
Alisema kuwa, washikadau wengi wangependa kuona ubora wa elimu umeongezeka na siyo kuongeza wigo wa ufaulu.
“Huku ni kujidanganya, jambo la kwanza wangetakiwa waende katika shule mbalimbali waone ni nini walimu wanataka, tatizo lipo wapi halafu wachukue hatua kwa sababu ukiangalia sasa ni kama kuna mgomo fulani hivi,” alisema.
Kwa upande wake Dk Kitila Mkumbo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Saikolojia ya Elimu na Masomo ya Mitalaa ya Shule Kuu ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema tatizo la elimu Tanzania halijawahi kuwa ni viwango vya ufaulu.
“Wanataka tu kuona hiyo asilimia 60 waliyojipangia inafikiwa. Walijiwekea lengo hilo wakijua kabisa kwenye elimu hakuna miujiza, lazima mtu ufanye kazi ndiyo matokeo yaonekane,” alisema.
Alisema kiwango cha kufeli kilichowekwa kinaifanya Tanzania kuwa nchi yenye viwango vidogo sana vya elimu kwenye bara hili.
“Burundi wenyewe mtoto akipata 50 ndiyo anakuwa amefeli, sisi huku tumeweka mpaka 19 ndiyo tunasema amepata hiyo F, lakini bado tunaita amefaulu, huu ni utani,” alisema.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekia Oluoch alisema Matumizi ya Alama za Maendeleo ya Mwanafunzi (CA) ni suala la kupongeza.
Hata hivyo, alisema kuwa kuna matatizo ya msingi kwenye elimu na ni lazima yafanyiwe kazi.
“Lengo lao la kushusha ufaulu ni ili ionekane kuwa BRN imefikia lengo, watoto wamefaulu ndiyo iwe furaha yao,” alisema.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi Tanzania (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema wamepokea suala hilo kwa mikono miwili.
“Zamani mtu alikuwa amapata sifuri na mwingine 33 wote tunasema wamepata F, lakini sasa kuna utofauti kwa hiyo unaweza kuona ni namna gani uwatumie hawa watu.
Pia suala hili linatoa mwanya mpana hata kwa Serikali na taasisi nyingine za elimu, ikitokea kwamba watu wa C wamekosekana unaweza kuona sasa tutumie wapi,” alisema.
Alisema kuwa, kwa sasa sera ya elimu inasema watu watakaoingia kidato cha tano wanatakiwa wawe na C tatu, lakini mwaka huu Serikali ilichukua C moja na D mbili wakaenda kidato cha tano.
“Yote hii ni kwa sababu hakukuwa na njia mbadala, lakini kwa sasa kutakuwa na mianya mingi sana.
Hata hivyo, tujue kuwa, tatizo la elimu Tanzania halikuwa madaraja, hii ilikuwa ni sehemu tu, lazima tuhakikishe tunatafuta matatizo ya msingi ya elimu yetu tuyafanyie kazi. Tukibaki kwenye hizi alama, basi nchi yetu itakwenda shimoni,” alisema.