wakazi wa nyamwaga na maeneo mengine wilayani Tarime wakiuza na kujipatia mahitaji kwenye mnada
Licha ya mvua kunyesha wajasiliamali na wanunuzi hawakujali kama inavyoonekana kwenye mnada wa Nyamwaga wilayani Tarime.
MATUKIO MBALIMBALI WILAYANI TARIME
UKIFIKA ROSANA WILAYA YA TARIME UTAPOKELEWA NA AKINA MAMA WAJASILIAMALI WANAOUZA NDIZI,MKUNGU MMOJA NI KATI YA SH,5,000-7,000
BIASHARA NI MAELEWANO MTEJA ANAOMBA KUPUNGUZIWA BEI.
AAKINA MAMA WENGI NDIO WANAOJIHUSISHA NA BIASHARA ZA KUUZA MBOGA,NYANYA NA MATUNDA KAMA INAVYOONEKANA HAPO KIJIJI CHA GIBASO WILAYANI TARIME
OONGEZA PESA ANGALAU KIDOGO,NI MANENO YA MAMA NAYEUZA NDIZI KATIKA ENEO MAARUFU KWA JINA LA WAUZA NDIZI KIJIJI CHA ROSANA WILAYANI TARIME
SSI LAZIMA GARI HATA BAISKELI INATUMIKA KUSOMBA MATOFALI KAMA ANAVYOONEKANA HUYO MWANANCHI NA MTOTO WAKE WILAYANI TARIME
SSAFARI NI SAFARI MAANA HAPA WANAHABARI WAMEKWAMA BAADA YA GARI KUHARIBIKA,LAKINI WALIFANIKIWA KUSONGA MBELE.
Kikwete abebeshwa zigo la mawaziri dhaifu
CCM
imemtwisha rasmi Rais Jakaya Kikwete jukumu la kukabiliana na mawaziri ‘mizigo’
wanaoshindwa kutimiza majukumu yao. PICHA | FIDELIS FELIX
Na Fidelis
Butahe, Mwananchi
Posted Jumapili,Decemba15 2013 saa 5:12 AM
Posted Jumapili,Decemba15 2013 saa 5:12 AM
Kwa ufupi
- Mawaziri 7 waliotajwa ni
‘mzigo’ kwa Serikali juzi walihojiwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM
chini ya Mwenyekiti wake Rais Kikwete, ambapo jana Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye alisema wamemshauri Rais Kikwete mambo
matatu; kuwafukuza, kuwahamisha wizara au kuwahimiza wafanye kazi.
Dar es
Salaam. Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kimemtupia mpira Rais Jakaya Kikwete wa kuamua hatima ya
mawaziri saba, wanaotuhumiwa kushindwa kutekeleza majukumu yao.
Mawaziri
hao waliotajwa ni ‘mzigo’ kwa Serikali juzi walihojiwa na Kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais Kikwete, ambapo jana
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye alisema wamemshauri
Rais Kikwete mambo matatu; kuwafukuza, kuwahamisha wizara au kuwahimiza wafanye
kazi.
“Kamati
Kuu imetoa maazimio saba ambayo yote yanazihusu wizara saba zinazoongozwa na
mawaziri hao. Tumemshauri Rais Kikwete, yeye ndiye ataamua nini cha kufanya kwa
sababu ndiye aliyewateuwa mawaziri hao,” alisema Nape.
Wakiwa
Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma katika ziara ya chama hicho, Nape pamoja na
Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana aliwatupia lawama mawaziri hao
wakati wakielezea changamoto zinazowakabili wakulima ambao ni asilimia 80 ya
Watanzania, huku mawaziri husika wakikaa kimya.
Nape
alisema mawaziri hao waliitwa kuhojiwa na kutakiwa kutoa maelezo ya masuala
yaliyoibuliwa wakati wa ziara hiyo ambayo pia iliwahusisha baadhi ya wajumbe wa
Sekretarieti.
Katika
maelezo yake kwa waandishi wa habari jana, Nape aliwataja mawaziri hao kuwa ni
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, Waziri wa Kilimo,
Chakula na Ushirika Christopher Chiza, Naibu Waziri wa Fedha Saada Mkuya
(alihojiwa kwa niaba ya Waziri wa Fedha Dk William Mgimwa).
Wengine
ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda, Waziri wa Maendeleo ya
Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia.
Sakata la
kutaka mawaziri ‘mizigo’ kutoswa limekuwa likiibuliwa na wabunge mbalimbali
katika mikutano ya Bunge mjini Dodoma, huku baadhi wakipendekeza hata Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda naye atoswe kutokana na kushindwa kuwasimamia mawaziri.
Ushauri
wa CCM kwa JK
Nape
alisema kuwa kazi ya Kamati Kuu ni kushauri, “Kazi yetu ni kushauri na siyo
kufukuza. Rais Kikwete ndiye amewateua mawaziri hao, ameupokea ushauri na yeye
ndiye mwenye uwezo wa kuwafukuza, kuwahamisha au kuwasukuma watende kazi. Hiyo
siyo kazi yetu”
Alipobanwa
zaidi kueleza ushauri ambao Kamati Kuu ilimpa Rais Kikwete Nape alisema, “Kuna
ushauri mwingine ambao tumempa Rais Kikwete hatuwezi kuuweka hadharani.”
Alisema
kuwa wakati wa kuhojiwa kila waziri alikuja na majibu yanayoihusu wizara yake
kutokana na udhaifu ulioelezwa na wananchi.
“Katika
kikao kijacho cha Kamati Kuu moja ya mambo yatakayojadiliwa ni pamoja na
kuangalia utekelezaji wa mambo saba tuliyoishauri Serikali kupitia hizo wizara
saba,” alisema.
Nape
alisema kuwa walipoeleza udhaifu wa mawaziri hao hawakueleza kuwa ni mzigo kwa
Serikali, bali walilenga kueleza upungufu wao katika kusimamia masuala
mbalimbali.
“Mfano
Waziri wa Kilimo kwa miaka minne hajawahi kwenda mkoani Ruvuma ambako kuna
ghala la chakula pia hajawahi kushughulikia matatizo yanayowakabili wakulima wa
korosho na mahindi,” alisema.
Hata
hivyo, Nape alisema kuwafukuza mawaziri siyo dawa na kuweka mambo sawa kwa
maelezo kuwa wakati mwingine utendaji kazi ndani ya Serikali unakwenda ovyo kwa
sababu ya mfumo na sheria mbovu.
“Watu
wanadhani ushauri tuliompa Rais Kikwete ni kuwafukuza mawaziri, wakati mwingine
kufukuza siyo mwisho wa suluhisho. Kwa mfano tumebadili mawaziri Tamisemi
lakini kila mwaka ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG) inaonyesha udhaifu katika wizara hiyo,” alisema Nape.
Maagizo
Nape
alisema agizo la kwanza ni kuhusu kilimo cha pamba ambapo Kamati Kuu iangalie
upya Serikali ipitie upya upatikanaji wa pembejeo za ruzuku kwa wakulima wa
pamba nchini.
Alisema
kuwa kuhusu kilimo cha mkataba kwa wakulima wa pamba, Serikali imetakiwa
kuratibu utaratibu wa kilimo hicho ikiwamo kutowalazimisha.
“Kwa
mfano Waziri husika hajafika kwa muda wa miaka minne na nusu mkoani Ruvuma
ambako ndiko kuna ghala la chakula na tulipofika Tunduma tulikuta foleni pale
mizani huku watumishi wakiwa wanafanya kazi kwa saa tisa, lakini baada ya
kueleza udhaifu huo sasa wanafanya kwa saa 24,” alisema.
Aliongeza,
“Chama kimeiagiza serikali kutowalazimisha wakulima kutumia mbegu ya Quiton,
badala yake elimu itumike zaidi badala ya nguvu.”
Alisisitiza
kuwa Kamati Kuu imeitaka Serikali kuangalia upya urasimu katika uwekezaji wa
viwanda nchini, hasa vinavyoongeza thamani ya mazao na kutoa ajira.
Kwa
upande wa wakulima wa korosho, Nape alisema kuwa Kamati Kuu imeisisitizia
serikali kujipanga kutatua tatizo la korosho na kuhakikisha inabanguliwa
nchini.
“Serikali
inatakiwa kuangalia upya orodha ndefu ya makato kwa wakulima hasa wa korosho na
vyama vya msingi au mamlaka zinginezo, ili kuondoa makato yasiyo ya lazima na
kuongeza kipato cha mkulima,”
“Kuhusu
pembejeo za ruzuku Kamati Kuu imepokea taarifa ya malalamiko ya wakulima juu ya
ufanyaji kazi wa mbolea ya Minjingu na kuagiza wananchi wawe huru kutumia
mbolea wanayoitaka badala ya kulazimishwa,” alisema.
Kwa
upande wakulima wa mahindi alisema kuwa serikali imetakiwa kumalizia malipo
yaliyobaki na kuhakikisha wanakomesha utaratibu wa kuwakopa wananchi mazao yao
bila kuwalipa.
“Utaratibu
uwekwe wa kufanya tathmini mapema ya mahitaji na uwezo wa kununua mahindi wa
serikali ili kuepusha utaratibu wa kuchukua mahindi ya wakulima bila
kuwalipa,”alisema.
Nnauye
alisema kwa upande wa madai ya walimu Kamati Kuu imeiagiza Serikali kukamilisha
uhakiki wa madai ya walimu na kuwalipa haki zao ikiwamo kuhakikisha madeni
hayazaliwi tena.
Kamati
hiyo pia imekemea watendaji wachache wanaojihusisha na ubadhirifu kwenye
halmashauri mbalimbali nchini.
“Serikali
imeshauriwa kuangalia upya sheria kama zinakidhi mahitaji ya wakati na
mazingira ya sasa ili kuongeza uwezo wa udhibiti na kuokoa pesa za walipakodi
zinazopotea kwa walafi wachache kwenye halmashauri mbalimbali nchini,” alisema
Nnauye.
Kwa
upande wa matatizo ya upatikanaji wa maji safi na salama serikali imeagizwa
kufanya mkakati wa makusudi na wa dharura kulitafutia ufumbuzi wa haraka na wa
kudumu tatizo hilo ikiwamo kuangalia upya utaratibu uliotumika kuwamilikisha
watu wachache maeneo makubwa ya ardhi, ambao wameshindwa kuyaendeleza badala
yake wanayatumia kuwakodishia wakulima wadogo.
Safari ya wanahabari vijijini
wakazi wa kijiji cha Gibasonkata ya Nyarukoba wilayani Tarime wakiongea na timu ya waanidhi wa habari kuhusiana na ongezeko la wanyama waharibu wa mazao kwa wakazi waishio kando ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti,mazungumzo hayo yalifanyika mbele ya jengo la Serena hoteli iliyokuwa imefunguliwa huku juu fundi akiezeka.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa hawana la kufanya baada ya gari walilokuwa wakilitumia kwenda kijiji cha Kegonga wilayani Tarime wkubadilika.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa hawana la kufanya baada ya gari walilokuwa wakilitumia kwenda kijiji cha Kegonga wilayani Tarime wkubadilika.
Bilal:Watoto waathirika zaidi ukiukwaji haki za binadamu
Na Elizabeth Zaya
12th December 2013
Makamu wa Rais,Dk. Mohammed Gharib
Bilal
Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib
Bilal, amesema kundi la watoto ndiyo limekuwa likiathiriwa zaidi na ukiukwaji
wa haki za binadamu nchini.
Aliyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya haki za binadamu yaliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Dk. Bilal alisema sababu kubwa inayochangia kundi hilo kukumbwa na suala la ukiukwaji haki za binadamu, ni kutokuwa na mtu wa kulisemea.
Alisema kuheshimu haki za binadamu, ni kioo cha kuonyesha nchi imekomaa kidemokrasia, hususan kwa kuwapa wananchi haki zao za msingi.
Alizindua mpango kazi wa kitaifa wa utekelezaji wa haki za binadamu wa miaka mitano utakaotoa mwongozo wa jinsi ya kusimamia utekelezaji wa haki za binadamu.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, alisema lengo kuu la mpango huo ni kukuza na kuimarisha haki za binadamu na kuimarisha uhusiano kati ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Pia kupunguza upungufu uliopo katika kuheshimu, kulinda na kukuza haki za binadamu nchini pamoja na kukuza, kuimarisha na kuongeza uelewa wa haki za binadamu baina ya wananchi wenyewe.
Aliyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya haki za binadamu yaliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Dk. Bilal alisema sababu kubwa inayochangia kundi hilo kukumbwa na suala la ukiukwaji haki za binadamu, ni kutokuwa na mtu wa kulisemea.
Alisema kuheshimu haki za binadamu, ni kioo cha kuonyesha nchi imekomaa kidemokrasia, hususan kwa kuwapa wananchi haki zao za msingi.
Alizindua mpango kazi wa kitaifa wa utekelezaji wa haki za binadamu wa miaka mitano utakaotoa mwongozo wa jinsi ya kusimamia utekelezaji wa haki za binadamu.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, alisema lengo kuu la mpango huo ni kukuza na kuimarisha haki za binadamu na kuimarisha uhusiano kati ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Pia kupunguza upungufu uliopo katika kuheshimu, kulinda na kukuza haki za binadamu nchini pamoja na kukuza, kuimarisha na kuongeza uelewa wa haki za binadamu baina ya wananchi wenyewe.
CHANZO: NIPASHE
Mawakili wamng`ang`ania Pinda kesi ya Kikatiba
Na Hellen Mwango
12th December 2013
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda
Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar
es Salaam imeambiwa kwamba kesi ya kikatiba dhidi ya Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, ina mashiko ya kisheria na inastahili kusikilizwa na mahakama hiyo
na kutolewa maamuzi.
Kesi hiyo ilifunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Madai hayo yalitolewa jijini Dar es Salaam jana na upande wa walalamikaji kupitia kwa Makamu wa Rais wa TLS, Wakili Peter Kibatala, wakati akijibu hoja za pingamizi la awali la walalamikiwa kwamba kesi hiyo ilifunguliwa kimakosa na haina mashiko ya kisheria na hivyo mahakama iitupilie mbali.
Kibatala aliwasilisha hoja zake mbele ya jopo la majaji watatu, likiongozwa na Jaji Kiongozi, Fakihi Jundu, akisaidiana na Jaji Augustine Mwarija na Dk. Fauz Twaib.
Upande wa walalamikiwa uliongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu, George Masaju, akisaidiana na Mawakili wa Serikali Wakuu, Gabriel Marata, Sarah Mlipano na Alesia Mbuya.
Wakili Kibatala alidai kuwa hoja za upande wa walalamikiwa kwamba kesi isisikilizwe kwa madai ni ya kizushi na haina mashiko, hazina ukweli na kwamba inastahili kusikilizwa na kutolewa maamuzi.
"Kesi hii ina mashiko ya kisheria na tuna haki ya kuja mahakamani kusikilizwa hata kama Waziri Mkuu ana kinga lakini imepita ukomo wa kikatiba...walalamikiwa wamethibitisha kwamba ina mashiko na kwa sababu hiyo, Naibu Mwanasheria Mkuu aliomba mahakama kesi hii iendeshwe kwa lugha ya Kiswahili kwa maslahi ya umma," alidai.
Akifafanua zaidi alidai kuwa mahakama inatakiwa iseme kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda kama ni sahihi au la.
Alidai kuwa ili mahakama itoe maamuzi, ni lazima kesi isikilizwe kwa pande zote mbili na siyo itoe amri kwa kusikiliza pingamizi la awali.
Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo ambapo upande wa walalamikiwa watatoa hoja zao.
Katika madai ya msingi, LHRC na TLS, wanapinga kauli iliyotolewa na Pinda bungeni, Juni 20, mwaka huu, wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
Pinda anadaiwa kutoa kauli inayolalamikiwa alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu, aliyetaka kujua msimamo wa serikali na mambo mengine, malalamiko dhidi ya vyombo vya dola katika baadhi ya maeneo kama Mtwara, kuwapiga wananchi.
Kesi hiyo ilifunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Madai hayo yalitolewa jijini Dar es Salaam jana na upande wa walalamikaji kupitia kwa Makamu wa Rais wa TLS, Wakili Peter Kibatala, wakati akijibu hoja za pingamizi la awali la walalamikiwa kwamba kesi hiyo ilifunguliwa kimakosa na haina mashiko ya kisheria na hivyo mahakama iitupilie mbali.
Kibatala aliwasilisha hoja zake mbele ya jopo la majaji watatu, likiongozwa na Jaji Kiongozi, Fakihi Jundu, akisaidiana na Jaji Augustine Mwarija na Dk. Fauz Twaib.
Upande wa walalamikiwa uliongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu, George Masaju, akisaidiana na Mawakili wa Serikali Wakuu, Gabriel Marata, Sarah Mlipano na Alesia Mbuya.
Wakili Kibatala alidai kuwa hoja za upande wa walalamikiwa kwamba kesi isisikilizwe kwa madai ni ya kizushi na haina mashiko, hazina ukweli na kwamba inastahili kusikilizwa na kutolewa maamuzi.
"Kesi hii ina mashiko ya kisheria na tuna haki ya kuja mahakamani kusikilizwa hata kama Waziri Mkuu ana kinga lakini imepita ukomo wa kikatiba...walalamikiwa wamethibitisha kwamba ina mashiko na kwa sababu hiyo, Naibu Mwanasheria Mkuu aliomba mahakama kesi hii iendeshwe kwa lugha ya Kiswahili kwa maslahi ya umma," alidai.
Akifafanua zaidi alidai kuwa mahakama inatakiwa iseme kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda kama ni sahihi au la.
Alidai kuwa ili mahakama itoe maamuzi, ni lazima kesi isikilizwe kwa pande zote mbili na siyo itoe amri kwa kusikiliza pingamizi la awali.
Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo ambapo upande wa walalamikiwa watatoa hoja zao.
Katika madai ya msingi, LHRC na TLS, wanapinga kauli iliyotolewa na Pinda bungeni, Juni 20, mwaka huu, wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
Pinda anadaiwa kutoa kauli inayolalamikiwa alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu, aliyetaka kujua msimamo wa serikali na mambo mengine, malalamiko dhidi ya vyombo vya dola katika baadhi ya maeneo kama Mtwara, kuwapiga wananchi.
UKATILI-AKATWA SIKIO NA SIME KWA KUKATAA KUFANYA NGONO NA SHEMEJI YAKE.
Ghati Mikere akiuguza majeraha
Mratibu wa dawati la polisi la Jinsia WP Sajenti Sijali Nyambuche akichukua maelezo ya Ghati walipotembelea majeruhi mbalimbali hospitalini hapo
“Mwingine aliyeolewa na Mwanamke Nyumba
Nthobu,anusurika kuuawa na mwanamme aliyemzalisha”
Desemba 7,2013
Serengeti:WAKATI wadau
mbalimbali kwa kushirikiana na serikali wakiwa katika kampeini za kupinga
vitendo vya ukatili wa kijinsia,Ghati
Mikere(20)mkazi wa Kijiji cha Bisarara wilaya ya Serengeti amenusurika kufa
kufuatia kukatwa shingo na sikio baada ya kukataa kufanya ngono na shemeji yake .
Tukio hilo
lililompelekea kulazwa wodi ya wanawake hospitali ya wilaya ya Nyerere limethibitishwa
na polisi na uongozi wa hospitali,linadaiwa kutokea novemba 30 mwaka huu majira
ya saa 5:asubuhi nyumbani kwa majeruhi huyo.
Akiongea kwa kugugumia
kutokana na maumivu akiwa wodini alisema
shemeji yake Chacha Kitari alimkata baada ya kukataa kushiriki tendo la ngono
kwa madai ya kuondoa mkosi wa mme wake kufungwa jela ,alipokataa ikapelekea
kukatwa sikio la kushoto na shingo.
“Kabla ya
kunishambulia kwa fimbo na kunikata kwa sime…alinitaka nifanye naye ngono kwa
madai kuwa ni maamzi ya ukoo na itasaidia kuondoa mkosi kwenye ukoo…kisha
amiliki mji na ndiye awe mme wangu ..yaani wameishajipanga kama mme wangu
anafia huko”alisema kwa masikitiko.
Hata hivyo Ghati
hakuwa tayari kusema mme wake kafungwa miaka mingapi na kwa kosa lipi,na
ameanza kutumikia kifungo lini.
Alisema licha ya
kupiga kelele kuomba msaada ,ndugu walimpuuza na ndipo akapata msaada kwa
majilani wa kufika hospitali kwa kupitia polisi.
Mkuu wa kituo
cha Polisi Mugumu ASP Joseph Maganga ambaye aliongoza dawati la jinsia akiwa
hospitalini hapo alisema ,wanaendelea kumsaka mtuhumiwa kwa kuwa matukio ya
ukatili wa kijinsia yameshamiri na kuomba jamii kutoyafumbia macho kwa kuwa
madhara yake ni makubwa kwenye familia na taifa.
Katika tukio
jingine mwanamke mmoja Mgosi Chacha (20)
mkazi wa mtaa wa bomani mjini Mugumu naye amelazwa hospitali baada ya
kujeruhiwa vibaya na mme wake wa kufikia kwa madai ya kukataa kurudisha mahari iliyotolewa na mwanamke
aliyemuoa(Nyumba Nthobu).
Akiwa wodi la
wanawake mbele ya dawati la jinsia la polisi alisema desemba 2.majira ya saa tatu usiku mwaka huu akiwa nyumbani
kwake mtaa wa bomani mwanamme huyo Chacha Charles mkazi wa kijiji cha Bonchugu alimfanyia
unyama huo baada ya kudai hatarudisha mahari ya mwanamke huyo kwa kuwa aliolewa
kwa mila na desturi za Kikurya.
“Nimeolewa kwa
ng’ombe 12 kutoka kwa bibi Bhoke Charles …ndoa ya Nyumba Nthobu…huyo mwanamme
yeye ameteuliwa na ukoo wa bibi ambaye alinitolea mahari…ambaye hakuzaa na
ameishakuwa marehemu …amenizalisha watoto wanne ambao ni mali ya alinitolea
mahar”alisema.
Alisema siku
ya tukio Charles akiwa nyumbani
mtuhumiwa huyo alifika na kusema anataka ng’ombe hao kwa kuwa amemweleza muda mrefu
bila utekelezaji,na kumpa nafasi ya kujibu na alianza kumshambuli na kumjeruhi
sehemu mbalimbali za mwili,kana kwamba haitoshi alimchukuakua usiku huo akiwa
ajitambui na kwenda kumtupa kwenye shimo refu umbali wa kilomita 2 kutoka
nyumbani kwake ambapo aliokotwa asubuhi na wapita njia ambao walitoa taarifa polisi na yeye alipata fahamu na
kujikuta amelazwa hospitali.
“Kwa sasa hali
za wanawake hao zinaendelea vizuri na wanapata huduma ya matibabu , tofauti na mwanzo walipofikishwa Hospitali
walikuwa katika hali mbaya”,alisema Musa
Wilison Muuguzi mwandamizi msaidizi .
Mwisho.
Kenyan Journalists hold protests over media law
By Lucas Barasa
Posted Wednesday, December 4 2013
Posted Wednesday, December 4 2013
In Summary
He said Parliament should raise at least 233 MPs to overturn the changes
proposed by President Kenyatta or the Head of State should withdraw the
proposed law and send a proper one to the House.
Nairobi.Journalists yesterday held protests in Nairobi and other major towns
over changes in the media Bill that curtail press freedom. Editors’ Guild
vice-chair David Ohito led journalists in peaceful picketing in Nairobi.
The protests were also held in Mombasa, Nyeri, Nakuru and Eldoret.
In Nairobi, the journalists converged outside Nation Centre before
starting the procession on Kimathi Street, Moi Avenue and later joined Harambee
Avenue before presenting their memorandum to the Office of the President,
Deputy President, Attorney General and to Parliament.
The media personnel bound their mouth and camera lenses with tapes. Mr
Ohito said journalists would move to court if Parliament passed memorandum
proposed by President Uhuru Kenyatta “which worsened an already bad Bill.”
Mr Ohito said the country requires free and independent media and that
regulations should only be through the Media Council or a professional body
composed of journalists. “The clauses in the media Bill should be in tandem
with the constitution and reflect modern society,” Mr Ohito said.
WITHDRAW PROPOSED LAW
He said Parliament should raise at least 233 MPs to overturn the changes
proposed by President Kenyatta or the Head of State should withdraw the
proposed law and send a proper one to the House.
Media Owners Association said President Kenyatta’s memorandum of refusal
on the Kenya Information and Communications (Amendment) Bill, 2013, should be
taken to a parliamentary departmental committee on Energy and Communication.
MOA on behalf of the Nation Media Group, Radio Africa Group, Royal Media
Services, Kass and Standard Group said the Bill as passed by the National
Assembly on October 31 fundamentally violates the Spirit and Letter of Article
34, Freedom of the Media and is thus unconstitutional.
WAFANYABIASHARA WAWILI WAUAWA ,MMOJA KWA KUPIGWA RISASI NA MWINGINE KUPORWA.
Desemba 1,2013.
Serengeti:WAFANYABIASHARA wawili
wilayani Serengeti wameuawa katika
mazingira na maeneo tofauti mmoja kwa
kupigwa risasi tatu na watuhumiwa
hawakuchukua kitu mwingine kwa kuporwa pikipiki,simu na maiti yake kutelekezwa eneo la shule ya msingi Matare.
Polisi wilayani hapa
wamethibitisha kutokea kwa mauaji hayo kwa tarehe na maeneo tofauti na kumtaja
aliyeuawa kwa kupigwa risasi tatu ni Mugaya Marwa Mnata(37)aliyekuwa na duka la
dawa baridi kijiji cha Rung’abure na Thomas Marwa Nyahure mkazi wa Matare na
aliyekuwa na duka mjini Mugumu.
Kwa mjibu wa taarifa za kipolisi
matukio hayo yametokea Novemba 26 na 28 ambapo maiti ya Nyahure ilikutwa
imelazwa kifudifudi eneo la shule ya
Msingi Matare huku kichwani kukiwa na jeraha la kupigwa na kitu cha ncha
kali,na Mnata aliuawa Novemba 28 kwa kupigwa risasi tatu ubavuni majira ya saa
3:30 usiku na kufa hapo hapo,ambapo maganda yalionekana ni silaha ni Smg.
Akizungumzia tukio la Mnata
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Rung’abure Charles Kibure alisema alikutwa
na mauti muda mfupi baada ya kufunga duka lake akielekea nyumbani.
“Aliuawa eneo la stoo ya kijiji
kitongoji cha Kwanina…watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wakiwa wamejificha
walimpiga risasi tatu ubavuni na moja kuchana masikio kisha
wakakimbia…haijajulikana nia yao maana inaonekana hapakufanyika
uporaji”alisema.
Alisema wananchi walijitokeza
muda mfupi baada ya kusikia mlio lakini watuhumiwa hawakupatikana na kumkuta
ameishakata roho,”haya mauaji yanaacha maswali sana …maana marehemu alihamia
hapa kibiashara miaka mitano iliyopita akitokea kijiji cha Kebweye wilayani
Tarime….alikuwa mfamasia mzuri na alikuwa na wateja wengi sana “alisema
Mwenyekiti.
Ofisa mtendaji wa kijiji hicho
alisema kutokana na matukio ya mauaji kama hayo kujitokeza mara kwa mara
,waliitisha mkutano wa hadhara na wananchi wameahidi kufuatilia na kutoa
taarifa za siri ili wahusika waweze kukamatwa kwa kuwa wanakijiji wanajawa na
hofu.
Naye msemaji wa familia ya
Nyahure Samweli Marwa alisema mdogo wake alitoka novemba 25 asubuhi mwaka huu
kuwa anaenda dukani na hakurejea mpaka maiti yake ilipookotwa novemba 26
asubuhi kijijini hapo.
“Hatujajua chanzo cha mauaji hayo…maana
hakuna mtu anahisiwa ama amekamatwa…sisi tulikuta maiti imelazwa kifudi udi
kichwani kaumizwa na kitu cha ncha kali…pikipiki,simu aliporwa,fedha hatujui
kama alikuwa nazo ama la…lakini kila mara tunapewa taarifa kuwa pikipiki
imeonekana maeneo Fulani tukienda hakuna mafanikio”alisema Marwa ambaye ni kaka
wa marehemu.
Michael Mwita jilani wa marehemu
alisema kuwa kutokana na matukio kama hayo kujiridia rudia mara kwa
mara,ameomba polisi wafanya uchunguzi wa kina ili kukomesha mauaji kama hayo.
Polisi wanaendelea na uchunguzi
na hakuna mtu anashikiliwa kwa matukio yote mawili.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)






