Subscribe:

Ads 468x60px

visima vingi vilivyochimbwa kwa ajili ya maji mbadala kwa wakazi wa North Mara havina maji


VISIMA VINGI WALIVYOCHIMBIWA WAKAZI WA NORTH MARA HAVIJAWAHIN KUFANYA KAZI KWA KUKOSA MAJI.
Na Anthony Mayunga-Nyamongo
Septemba 3,2012.

TATIZO la ukosefu wa maji linaendelea kuwatesa wakazi wanaozunguka mgodi wa African Barrick North Mara ulioko Nyamongo wilayani Tarime ,kutokana na visima vingi vilivyochimbwa kama vyanzo mbadala kutokuwa na maji.

Mwaka 2009 kamati za bunge mara baada ya kujiridhisha kuwa maji yam to Tighite hayafai kwa matumizi kutokana na kuathiriwa na maji ya sumu yaliyovuja kutoka mgodi wa Gokona.

Uchunguzi wa blogu hii ulibaini kampuni haijachimba visima maeneo mengi kama ilivyoagizwa badala yake inasambaza maji kwa kutumia magari yake,huduma ambayo wananchi wanadai inawafanya wasichimbe visima ili wawe wanachota kwa wakati wanaotaka si kama wanavyopelekewa kwa muda maalum.

Pia visima vingi vilivyochimbwa na halmashauri havina maji ,ingawa serikali imekuwa ikijinasibu kuwa wameishachimba visima kwa wakazi wanaozunguka mgodi huo.

Uchunguzi ulibaini kuwa katika kisima kilichoko kitongoji cha Nyabikondo kijiji cha Kewanja kata ya Kewanja kilichochimbwa na halmashauri hakina maji ,hata bomba hakuna na eneo lote limegeuka kichaka.

Katika kitongoji cha Kemambo  kisima kilichochimbwa na kampuni ya African Barrick North Mara hakina maji hali ambayo inapelekea wananchi wa vitongoji hivyo kulazimika kupanga misululu kusubiri magari ya kampuni kuwasambazia maji ambayo hawajui yanakotolewa.

Pia kisima kingine katika eneo la Kenyatanka kilichochimbwa na kampuni hiyo hakifanyi kazi kwa kuwa hakina maji,hali ambayo inawapelekea wananchi kwenda kuchota maji kwenye kisima kingine kilichoko sekondari ya Ingwe na shule ya msingi Nyamongo kilichochimbwa na halmashauri ya wilaya.

Visima viwili kwa kijiji kizima ndivyo vina maji ambavyo ni kilichoshuleni na kitongoji cha Mjini kati ambacho kimechimbwa na shirika la Japani (Jaica) wengine kwenye lambo la Kewanja ambalo maji yake hayafai kwa matumizi ya kunywa wala kupikia .

Wanne Mwita mlinzi wa lambo hilo alisema kuwa maji ya lambo hilo ambalo lilikuwepo lakini kampuni imesaidia kulipanua hayafai kwa matumizi ya kunywa,wala kupikia lakini kutokana na tatizo la maji wengine huyatumia kwa kupikia na kuoga.

Hata hivyo alisema liko hatarini kuziba kwa kuwa linazidi kujaa tope kutokana na kuwa limetengezwa vibaya,hali ambayo ililalamikiwa na baadhi ya wananchi kuwa wanalazimika kutumia maji yasiyokuwa safi na salama kutokana na serikali kuwapuuza kwa kutoa taarifa za uongo.

Fanuel Sasi mkazi wa kijiji hicho alisema kuwa visima vilivyochimbwa hapakuwahi kufanywa tafiti kabla ili kujua kama kuna maji nan i salama ama eneo limeathiriwa na sumu kutoka mgodini,hata ufuatiliaji wa halmashauri haupo ndiyo maana eneo la kisima limegeuka kuwa kichaka kabla ya kutumika.

Diwani Kibasuka.
Diwani wa kata ya Kibasuka Yusuph Moya (CCM)alisema eneo lake ndilo liliathiriwa na maji ya sumu kwa kuua na viumbe hai lakini hawajahi kuchimbiwa visima.

“Wegita na Nyarwana hawana maji wanatumia vyanzo vya kienyeji,visima vimechimbwa Nyakunguru kuna vya Jaica na halmashauri ,vitongoji vipo saba vitatu vya Nyamange,Nyakunguru na Nyamuma vina maji lakini Nyakwirambe,Itandura,Nyamichare na Turuturu havina maji,hakuna maelezo tunayopewa”alisema kwa uchungu.

Mhandisi wa maji wilaya.
Vita Mkubwa mhandisi wa maji wilaya ya Tarime katika hali ambayo inaonyesha hajui walichimba visima vingapi na wapi na kama vina maji na havina alisema ,anaomba apewe muda awasiliane na wenzake ili kujua ukweli wake ndipo ataeleza.

“Niko kwenye kikao mkoani ,lakini naomba muda ili nifuatilie hilo tatizo maana nashindwa kukujibu ,vipo tulivyochimba sisi na Jaica,kama huna nafasi ya kukutana kesho tuongee nitakupigia baada ya kuwasiliana na wenzangu,”alijibu.

Mgodi.
Mmoja wa maafisa habari mgodini hapo aliyejitambulisha kwa jina la Robert alipoulizwa alidai kuwa yuko mbali na ofisi na kudai kuwa yupo Shayo na kuahidi kutoa namba yake kwa maelezo zaidi.

Hata hivyo badala ya kutoa namba yake alidai ametoa namba ya mwandishi kwa Shayo ambaye atapiga,alipotakiwa kutoa namba ya shayo aliahidi kutuma,hata hivyo alipotafutwa tena hakutaka kupokea simu ,hadi tunakwenda mitamboni Shayo hakupiga kama walivyoahidi.

Mwisho,inaendelea.

Nilifanyiwa unyama na kaka yangu

Nilifanyiwa unyama na kaka yangu  Send to a friend
Sunday, 02 September 2012 07:24

ALINIZIBA MDOMO KWA NGUO YA NDANI, AKANIFUNGA KWENYE MTI PORINI, AKANIBAKA
Anthony Mayunga
UKATILI wa kijinsia unaendelea kushika kasi nchini ambapo hivi karibuni, mkazi mmoja wa Kijiji cha Kemugesi, wilayani Serengeti mkoani Mara amembaka dada yake na kasha kumfunga porini kwa zaidi ya saa saba, huku yeye akitokomea kusikojulikana.
Kijana huyo, jina tunalo alitenda unyama huo saa 1:00 asubuhi ya Julai 22, mwaka huu, huku taarifa nyingine zikidai kuwa kijana huyo pia aliwahi kumtendea ukataili kama huo shangazi yake.
Akisimulia mkasa huo, binti aliyeathirika na ukatili huo(Jina tumelihifadhi kwa sababu za kimaadili), alisema kuwa kaka yake huyo alimbaka huku akiwa amemsokomeza nguo ya ndani mdomoni kumzuia asipige kelele.
“Kaka alinibaka akiwa ameniwekea nguo yangu ya ndani mdomoni,  huku akinibana nisipige kelele. Kisha akanifunga kwenye mti na nilikaa kuanzia  saa 5 asubuhi hadi saa 12 jioni,” anasimulia binti huyo mwenye umri wa miaka 15.
Anaelezea kuwa kaka yake huyo ambaye wanachangia baba, alimwomba aende naye shambani akamsaidie kuvuna pamba na ndipo alitekeleza unyama huo.

Binti huyo ambaye ni mmmoja wa watoto 29 wa baba yao aliye na wake wanne anasema kuwa  licha ya kupata maumivu makali kutokana na kubakwa, kaka yake huyo pia alimpiga sana na kumsababishia maumivu makali sehemu mbalimbali za mwili.
Hata hivyo, mbali na binti huyo kufanyiwa unyama, baba yake mzazi anahaha kuhakikisha kwamba binti huyo na mama yake wanamaliza suala hilo nyumbani akidai kuwa kijana wake anasumbuliwa na majini na kwamba akifungwa anaweza kufia jela.

Ilivyotokea
Binti huyo anasimulia kuwa siku ya Jumapili  Julai 22, saa 1:00 asubuhi mwaka
huu, walikwenda na kaka yake huyo kuvuna pamba wakiwa na kijana wao wa kazi, anayewasaidia kuchunga ng’ombe.
"Tulivuna pamba bila matatizo, kwenye saa 4:45 asubuhi akasema tukachume mahindi shambani kwetu kwa ajili ya kwenda nayo nyumbani kwa
ajili ya kuchoma. Tukatoka vizuri hadi tulipoacha madumu ya pamba. Nikakaa, lakini yeye akamwagiza kijana wa kazi arudi shambani kumbe, alitaka kutekeleza nia yake. Hapo alinivamia na kunikaba shingoni,"anasema kwa unyonge na kuongeza:
"Alinibeba na kukimbia nami hadi kichakani na kuchana nguo yangu ya ndani, gagulo na kuniwekea nguo ya ndani mdomoni huku amenibana shingo, akaanza kunibaka. ...Nilipata maumivu makali sana, alichukua muda mrefu akinifanyia unyama huo.”
“Damu zilivuja sana na baada ya kumaliza akanipiga na kwenda kunifungia kwenye mti,   kisha akanipiga teke na kusema kuwa nitafia hapo na nyumbani hawataniona tena,” anaeleza binti huyo.
Anasema kuwa kijana wao wa kazi aliposikia kelele alifika eneo la tukio, lakini kaka yake huyo alimfukuza na kutishia kumuua na kuwa akisikia popote kasema jambo hilo, atamuua.
“Nilihangaika sana kujinasua, nikawa nasugua mikono kwenye mti ndio maana nimechubuka hivi. Hatimaye kitambaa cha machoni kikalegea nikapata nafasi ya kuangalia alipofungia, nilihangaika hadi nikaweza kufungua,” anasema.
Anasema kuwa baada ya kujifungua kwenye mti alikwenda nyumbani na kumkuta mama yake akiwa na wasiwasi kwa kuwa alioongozana nao walirudi na hawakueleza walipomwacha.
Anasema kuwa alimsimulia mama yake kilichotokea naye aliamua kumpeleka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji.
Anaongeza kuwa njiani walikutana na mama wa mtuhumiwa na baada ya kumweleza alichofanya motto wake, alisema kuwa kijana wake ana matatizo mengi, hivyo hawezi kushangaa kusikia hilo.

"Kama aliweza kumbaka shangazi yake, kisha akamfunga na kamba na kumwacha porini, sishangai kama amemtendea mdogo wake, maana anatisha kwa matendo yake,”alisema mama wa kijana huyo.

Julai 23,walifika Kituo Kidogo cha Polisi Kenyana na kupewa fomu ya matibabu (PF 3) ambapo polisi walidai wapewe Sh30,000 za mafuta ili wakamtafute mtuhumiwa.
“Walisema wanataka hizo fedha wanunue petroli na waende watatu kwa pikipiki, mama alisema kuwa hana, basi ikawa ndiyo tumekosa ushirikiano zaidi ya kwenda zahanati ya Kenyana kupata matibabu, kisha tukarudi nyumbani,"anaeleza binti huyo.
Kwa mujibu wa binti huyo, Julai 29 mjomba wake,  Chacha Makindi mkazi wa Kemugesi alimchukua hadi Kituo cha Polisi Mugumu ambapo walifungua jalada na kupewa barua ya kwenda kwa Mtendaji wa Kijiji ili mtuhumiwa
akamatwe.
Hata hivyo mtuhumiwa huyo hajakamatwa kwa kile kinachodaiwa kuwa baba yake amemficha.

Binti huyo anadai kuwa hajui kusoma wala kuandika licha ya kuwa alisoma hadi darasa la tano na kuacha kutokana na matatizo ya
kifamilia ambapo wenzake sasa wako kidato cha kwanza.


"Kwetu hakuna hata mtoto aliyefika sekondari, yaani watoto wote 29 na baba
hajali kabisa hata kununua sare. Ndiyo maana niliacha masomo na sasa
sipendi kurudi kijijini nitakaa hapa kwa ndugu yangu...maana hali huko
si nzuri,"anadai binti huyo.


Wanaharakati
Julai 30 akiwa na mjomba wake walifika ofisi ya Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu, ili kupata msaada wa kisheria hali iliyomfanya
baba yake mzazi ajisalimishe baada ya kuandikiwa barua na kuanza kumhudumia kwa ajili ya matibabu .


Kaimu Katibu Mtendaji wa Shirika la Wasaidizi wa Sheria na Haki za Binadamu wilayani Serengeti, Monica Daniel anasema kuwa baada ya kuona mchezo uliopo wa baba yake, waliamua kuingilia kati na wanasimamia matibabu yake .


"Baba yake anataka mambo yaishe, anamlaumu sana mke wake kwa madai kuwa alishamwacha, hivyo kwa tatizo hili hataki kutoa msamaha kwa mtoto wa mke mwenzake.
Sisi tulibaini kuwa huyu mzazi alipoachana na mke wake mdogo hata watoto pia hawapi huduma,"anasema Monica.

Kuhusu vipimo alivyofanyiwa binti huyo Monica alisema: "Katika vipimo amekutwa na maambukizi katika njia ya mkojo(UTI) na macho pia yalikuwa yameumizwa, ambapo baba yake ametoa Sh00,000 za matibabu.”

Anaongeza kuwa wanajiandaa kwenda kumpima binti huyo kama amepata maambukizi ya Vurusi vya Ukimwi.
Hata hivyo, alisema kuwa baba wa binti huyo anaomba shirika lao lisaidie kumshauri mama ya binti huyo ili wayamalize nyumbani na kuendelea na matibabu ya kienyeji akiamini kuwa kijana wake aliyetenda unyama huo anasumbuliwa na majini.
“Sisi tumempa msimamo kuwa haki lazima itendeke, kama ni mgonjwa anatakiwa akapimwe
akili ikithibitika watamwachia. Kwa nini anamficha kama ni mwehu? Hilo tumelikataa kwa kuwa hata aliyejeruhiwa anataka afikishwe mahakamani,"anabainisha Daniel.

Monica aliomba hatua kali zichukuliwe kwa mtuhumiwa wa tukio hilo kwa kuwa kitendo alichofanya ni cha kikatili na hakifai kunyamaziwa.
Alidai kuwa hata mzazi wake anatakiwa kuhojiwa na polisi sababu za kutetea unyama aliofanya kijana wake kwa kuwa ni kinyume kabisa cha sheria ya Mtoto ya mwaka 2009.

Polisi
Polisi wanadai kuwa wanaendelea kumsaka mtuhumiwa huyo na kuwa maagizo yalishatolewa kwa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Kemugesi kuhakikisha kuwa wanamnasa au kutoa taarifa ili akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya
sheria .



kanisa laweka ratiba kuombea taifa


KANISA LAWEKA RATIBA KUOMBEA AMANI YA NCHI.
Na Anthony Mayunga-Serengeti
Agosti 19,2012.

KUTOKANA na taifa kukabiliwa na matatizo mengi ambayo yanachangiwa na ukosefu wa maadili kwa baadhi ya watumishi na kupelekea malalamiko kila kona ,kanisa la Mennote la Kiinjili Tanzania wilayani Serengeti limepenga ratiba ya maombi kwa ajili ya taifa.

Hivi karibuni madhehebu ya dini yamejitokeza kuombea taifa kutokana na kuibuka migomo,maandamano kila kona,migogoro ya kisiasa,lengo likiwa ni kuhakikisha taifa linapata amani na utulivu.

Shemasi wa kanisa hilo Wilson Itumbi katika mahubiri yake alisema maombezi hayo yatakuwa yakifanyika kila siku ya jumatano jioni hapo kanisa ili kuhakikisha amani,upendo na mshikamano unaimarika kwa kuwa nchi inakwenda vibaya.

“Amani inaonekana kutoweka na hali ikiendelea hivi nchi itakuwa kwenye vita kali chanzo ni kutoelewana kwa vyama vya siasa na kupelekea migogoro kwa viongozi walioko madarakani kutopendana wao kwa wao na kuwajengea mazingira magumu wananchi kujiletea maendelo”alisema.

Alisema kuwa licha ya Tanzania kusifika kuwa nchi ya amani na kusifika katika maeneo mbalimbali ya nje ya nchi,lakini kwa hali ilivyo sasa sifa hiyo imeanza kutoweka.

Aliwataka viongozi wa dini na washirika wa madhehebu mbalimbali kusimama imara katika kusimama imara kuliombea taifa na viongozi wote kuanzia rais ,wabunge na  madiwani waweze kuliongoza taifa vema kwa kutanguliza maslahi ya taifa wala si vyama vyao.


Mwisho.

viongozi wa CWT washikiliwa na polisi Tarime

VIONGOZI WA CWT WASHIKILIWA NA POLISI
Na Anthony Mayunga-Mara
Agosti 1,2012.

MGOMO wa walimu kwa Mkoa wa Mara sasa umechukua sura mpya kwa wilaya ya Tarime viongozi wa chama cha walimu wamekamatwa na polisi kwa madai kuwa wanachochea mgomo.huku  wanafunzi  wengi wakiamua  kutokwenda shuleni kwa kuwa hawafundishwi.

Hali hiyo inajitokeza ikiwa ni siku ya tatu toka Mgomo mkubwa wa kitaifa umetangazwa na uongozi wa CWT wakitaka waongezewe misharaha asilimia mia na malimbikizo ya madeni.

Akiongea na Mwananchi kwa njia ya simu Mwenyekiti wa CWT wilaya ya Tarime Matinde Magabe alisema kuwa yeye na katibu wake John Magoko walikamatwa na polisi wakati wakiwa wamefuatilia Mwalimu wa shule ya msingi Rebu Esther Magesa aliyekamatwa julai 30,2012 kuhusiana na mgomo.

"Tukiwa polisi tumefuatilia dhamana ya Mwalimu Esther ,ocd akampigia ofisa elimu simu kuwa tupo,nikiwa nakunywa chai walifika askari wawili mmoja kavaa kiraia mwingine sare za polisi wanadai wananitaka mimi nachochea mgomo,kulitokea vurugu kidogo maana wananchi walichachamaa"alisema

Na kuwa walimfikisha kituo cha polisi kwa mahojiano,"niliona wanampango wa kunionea nikatoka kama napiga simu nikapanda bodaboda na kutoka kasi ,wakaamua kwenda kumkamata katibu wangu John Magoko na kumkwida"alisema Magabe.

Alisema hata yeye anatafutwa ili akamatwe ,kwa madai kuwa wamekuwa chanzo kikuu cha mgomo kusambaa wilaya nzima,huku akidai uamzi huo wa Mwajiri kutumia polisi ni kwenda kinyume na sheria kwa kuwa taratibu za mgomo zimefuata sheria vinginevyo wangekamatwa viongozi wa kitaifa wa chama.

Rpc akana.
Kamanda wa mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya Justus Kamugisha alipoulizwa alikana kuwepo kwa tukio hilo na kudai kuwa wao wanamshikilia mwalimu Esther kwa tuhuma za kuchochea wanafunzi wa shule ya Msingi Rebu kuandamana na kuwa yuko nje kwa dhamana na uchunguzi unaendelea.

Katibu adai alikamatwa.

Wakati Kamanda anakanusha kutokuwepo tujkio hilo Katibu wa CWT wilaya Tarime Magoko alilithibitishia Mwananchi kwa njia ya simu kuwa alikamatwa akituhumiwa kumtorosha Mwenyekiti wa wilaya walipokuwa polisi.

"Ndio kwanza naachiwa nimehojiwa hapo kituoni wakidai mimi niwaambie Mwenyekiti alipo ,maana wanadai nimemsadia kutoroka,nimekataa nimejieleza na nilikuwa na katibuwa CWT mkoa mwisho wameniachia"alisema.

Katibu Cwt Mkoa akiri kukamatwa kwa katibu wake.

Katibu wa CWT mkoa wa Mara Fatuma Bakari alilithibitishia Mwananchi kukamatwa kwa katibu huyo kisha kuachiwa,"niko hapa Tarime ni kweli amekamatwa na kuhoojiwa lakini ameachiwa ndio tunaendelea kufuatilia kwa undani zaidi"alisema.

Wakati serikali ikitumia njia hiyo kama vitisho wanafunzi katika shule nyingi za msingi na sekondari wilayani Serengeti na Tarime  wameamua kutokwenda shuleni kwa kile wanachodai wanakwenda kucheza kwa kuwa hawafundishwi.

Kwa wilaya ya Serengeti imerbainika kuwa wazazi wengi waliamua kuwatumia watoto wao kwa shughuli mbalimbali za kuuza vitu vido vidogo mnadani ambao hufanyika kila tareme moja ya mwezi.

Uamzi huo pia unadaiwa kuungwa mkono na baadhi ya wazazi kwa madai kuwa wasubiri uamzi wa madai yaliyoko Mahakamani kama mgomo utasitishwa ama la,huku wakiwatuhumu baadhi ya viongozi wa serikali kuwa hawana uchungu na madhara ya mgomo huo kwa kuwa watoto wao hawasomi katika shule za serikali.

mwisho.