Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Majimoto Kata ya Maji Moto wilayani Serengeti Johannes Masioni kulia akikabidhi vifaa ,karo na michango kwa watoto wanne wa mazingira magumu ,alioamua kuwasaidia ili waanze masomo kidato cha kwanza Busawe Sekondari,msaada jumla ya msaada wake ni sh,420,000=
Someni
Saidieni watoto wasome si kuchangia harusi
watoto wanaahidi kusoma
SHULE KUKOSA VYOO WALIMU HULAZIMIKA KURUDI MAJUMBANI KUJISAIDIA.
Machi ,2014
Serengeti:WALIMU 37 wa shule ya Msingi Mapinduzi ‘A’iliyoko Mjini
Mugumu wilaya ya Serengeti,hulazimika kurudi kwenye makazi yao kujisadia kutokana
na shule hiyo kutokuwa na vyoo vya walimu kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Ofisa Elimu wilaya hiyo William
Mabanga amekiri kuwepo kwa tatizo hilo,na kudai kuwa ni shule nyingi hazina
vyoo vya walimu,kwa kuwa mkazo uliwekwa kujenga vyoo vya wanafunzi wakasahau
walimu,na kuahidi kuwa litashughulikiwa kwa kuwa athari yake ni kubwa kwa
walimu na watoto.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo James
Johannes amesema tatizo hilo lina muda mrefu,mamlaka husika zinataarifa lakini
hakuna hatua zilizochukuliwa kuwanusuru walimu
kwa kuwa wanaodharirika kwa kukosa vyoo na kuokoa muda wa vipindi ambao
huvitumia kurudi majumbani kujisaidia.
“ Mwalimu hutumia zaidi ya dakika 20 kutafuta eneo la kujistiri…hapa ni katikati
ya mji hawawezi kukimbilia vichakani…maana walimu 32 ni wakike , na wakiume 6 ,wanalazimika
kwenda kwenye miji yao ama majilani kujisaidia….na hii ndiyo shule ya
mjini,imeachwa hivi…tunaomba mamlaka zichukue hatua maana watoto wanakosa
mtiririko wa vipindi kwa tatizo hilo,”alisema Mwalimu kwa masikitiko.
Alisema awali walikuwa wanatumia
choo cha kanisa la Sayuni na baada ya kuweka uzio ,wakakosa sehemu ya
kujisaidia,na choo cha wanafunzi inakuwa vigumu kwa kuwa nacho kiko katika eneo
la mtu na matundu yaliyopo ni 12 kati ya mahitaji ya matundu 32 kwa watoto 890 waliopo
hapo shuleni.
“Baada ya kuweka uzio hatuna
sehemu ya kujisaidia…kwa mwalimu anayekaa shuleni anaye ana choo cha muda
ambacho kinadhalilisha maisha ya walimu….kuhusu vyoo vya wanafunzi tayari
tumeishapata notisi maana ni uwanja wa mtu anataka kuendeleza eneo lake….kuna
hatari ya shule kufungwa iwapo atazuia
hapatakuwa na jinsi,”alibainisha.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha NHC
,Elias Nyamraba anasema tatizo hilo linawadhalilisha walimu na kukosa morari ya
kufundisha ,na inapotokea amepata mchafuko wa tumbo hupata shida,hivyo Matokeo
Makubwa sasa hayawezi kupatikana katika mazingira kama hayo.
Mwenyekiti wa Kamati ya
Elimu,afya na Maji wilaya Daniel Kegocha alikiri kuwepo kwa tukio hilo na kuwa
walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu kwa kukosa vyoo.
“Nilifika shuleni baada ya
kufuatwa na walimu,kweli hali ni mbaya …maana
wanaacha vipindi na kurudi nyumbani kutafuta vyoo kuna athari kubwa
kitaaluma…nitalifikisha hili tatizo halmashauri ya wilaya ili kuona jinsi ya kuchukua hatua za
haraka”alibainisha.
Kuhusu choo cha wanafunzi kuwa
katika eneo la mtu,diwani hiyo alisema hakuwa anajua na kubainisha yote
yanatakiwa kufanyiwa kazi haraka ili kunusuru shule isijekufungwa.
Hata hivyo baadhi ya wananchi
walilaumu madiwani kwa kubadilisha matumizi ya eneo la mnada linalopakana na shule hiyo,viongozi
wakajigawia maeneo ambalo lingeweza kutumiwa na shule hiyo ili kuwanusuru
watoto wanaokwenda kujisaidia eneo la jilani kwa kuvuka barabara kuu,hali
ambayo ni hatari kwa usalama wao.
Kwa mjibu wa taarifa ya wilaya
,inabainisha kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu wa matundu ya vyoo kwa
walimu 1,401,ambapo toka mwaka 2009 mpaka 2013 wamejenga matundu 25 tu,upungufu
wa madawati ni 16,460,ambapo zaidi ya asilimia 50 wanasoma wakiwa wamekaa
chini.
Mwisho.
SHULE MBILI ZENYE WATOTO 1,005 ZINA WALIMU WATANO,
“kati yao watoto 777 husoma wamekaa chini,kutokana na ukosefu wa
madawati.
Machi 10,2014
Serengeti:WALIMU
watano wa shule za msingi Kitarungu na Matanka kata ya Nyansurura wilayani
Serengeti wanalazimika kufundisha
wanafunzi 1005 ,moja yenye watoto 557 ina walimu 2 na nyingine yenye
watoto 448 ina walimu 3.
Mbali na upungufu wa walimu shule hizo zote mbili zina
madawati 76 ambapo wanafunzi 777 kwa shule hizo mbili husoma wamekaa chini hali
ambayo inabainisha changamoto kwa sekta ya Elimu ambayo ni miongoni mwa sekta 5
zilizokwisha zindua mikakati ya Matokeo Makubwa sasa(BRN).
Mratibu elimu kata hiyo Benard Misolo aliliambia Mwananchi
kuwa kwa hali hiyo wastaraji miujiza kwa walimu wawili kufundisha wanafunzi 557
kuanzia darasa la kwanza hadi la saba ,wakati huo Mwalimu mkuu ana majukumu ya
utawala.
“Tatizo hili ni la muda mrefu ,ofisi ina taarifa ….kupitia
uongozi wa kata na elimu toka mwaka 2007 shule ilipoanzishwa bila mafanikio…tukipata
walimu sita watasaidia kupunguza tatizo ,kwa shule ya Matanka walimu watatu
hawakidhi… wanaopata shida hapa ni watoto”alisema.
Kuhusu madawati alisema shule ya Kitarungu wanafunzi wanaosoma
wamekaa kwenye madawati ni 108,huku wanafunzi 449 wanasoma wakiwa wamekaa
chini,na shule ya Matanka wanaokalia madawati ni 120,huku 328 wanasoma wakiwa
wamekaa chini.
“Kuna upungufu mkubwa wa vyumba vya Madarasa ,maana darasa
moja watoto wanakaa kuanzia 50 hadi 120…wengi wakiwa wamekaa chini…hakuna
usikivu hapo..hayo yote ni madhila yanayowakuta walimu wawili,”alisema.
Diwani wa kata ya Nyansurura Jackson Mwita(Chadema)
aliliambia Mwananchi kuwa kata yake inahali mbaya kwa upande wa elimu kwa shule
za msingi,kwa kuwa shule zote saba hazina walimu wa kutosha.
“Tumeomba sana walimu lakini hatupewi…wanadai hakuna nyumba
za walimu…lakini hakuna kata yenye nyumba za walimu za kutosha….mjini shule
moja ina watoto 800 ina walimu 37,hakuna nyumba wamepanga….hapa watoto zaidi ya
500 walimu wawili….uwiano gani huo…harafu mwisho unalaumu watoto na
wazazi….nadhani kuna mitizamo hasi ya kisiasa,”alisema kwa masikitiko.
Mwenyekiti wa kamati ya Elimu,afya na Maji halmashauri hiyo
Daniel Kegocha amekiri kuwepo kwa upungufu huo na kuwa lilikwishatolewa agizo
idara ya elimu kupitia vikao kuwa wapeleke walimu shule zenye upungufu.
“Walimu wapya watakaporipoti mwaka huu shule zenye upungufu
zitapewa kipaumbele…si hizo hata Nyahende kata ya Kebancha bancha ina walimu
watatu wanafunzi zaidi 500…maana shule za mjini wamerundikwa walimu wengi
lazima uwiano uwepo,”alisisitiza.
Hata hivyo imebainika kuwa shule nyingi hazina nyumba za
walimu,na hata vijijini wanakosa nyumba za kupanga hali ambayo inapelekea
walimu kukimbia,ambapo mwaka 2013 walimu 80 walihama mkoa huo,wengi
wakilalamikia mazingira magumu ya kazi.
Uongozi wa idara ya elimu wilaya wamekiri kuwepo kwa
upungufu na kudai kuwa tatizo kubwa ni ukosefu wa nyumba ,hata nyumba za walimu
kupanga baadhi ya maeneo ni changamoto na kuomba jamii kujitolea kujenga nyumba
,na kutengeneza madawati ili kuboresha elimu.
Mwisho.
M4C PAMOJA MUGUMU SERENGETI
TANAPA KUENDESHWA KWA MFUMO WA KIJESHI ILI KUDHIBITI UJANGILI
Katika kukabiliana na vitendo vya ujangili vinavyoendelea kushika
kasi ndani nan je ya mipaka ya nchi yetu, Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)
litaendeshwa katika mfumo wa jeshi-usu katika siku chache zijazo ambapo
watumishi wake watalazimika kupitia katika mafunzo maalum ya kijeshi.
Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA aliyasema hayo mwishoni mwa wiki alipokuwa
akifunga rasmi mafunzo ya askari wapya 96 walioajiriwa na TANAPA na kuhudhuria
mafunzo ya miezi minne katika Hifadhi ya Taifa Katavi mwishoni mwa wiki.
Kijazi alisema kuwa TANAPA imeanzisha utaratibu mpya ambapo sasa
askari wanaoajiriwa na shirika kutoka katika Vyuo vya Wanyamapori vya Mweka na
Pasiansi pamoja na wale wa kutoka Jeshi la Kujenga Taifa watalazimika kupitia
mafunzo maalum yanayoandaliwa na shirika kwa ajili ya kuwawezesha waajiriwa
wapya kufahamu mazingira halisi ya utendaji kazi katika eneo la uhifadhi katika
maeneo ya Hifadhi za Taifa.
Tunakufunga usitoroke usubiri kuchinjwa
wanafunzi wa shule ya msingi Kisangura Serengeti wakifunga kuku walionunuliwa kwa ajili ya hafla ya kukabidhi vifaa mbalimbali kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ,chini ya ufadhili wa New York Yearly Meeting la Marekani kwa usimamizi wa shirika la Zinduka la wilayani Bunda
Tunakufunga usitoroke usubiri kuchinjwa ,ndivyo inavyoonekana wanafunzi hawa wanasema huku wakiwafunga kuku kwa kamba wasijetoroka wasubiri kuchinjwa
Tunakufunga usitoroke usubiri kuchinjwa ,ndivyo inavyoonekana wanafunzi hawa wanasema huku wakiwafunga kuku kwa kamba wasijetoroka wasubiri kuchinjwa
Mbegu mbovu zatengeneza mafuta ya kula Mara
Meneja wa Kiwanda cha Bundaa, Roharl
Parmar (kushoto) akiwa na Kaimu Afisa Shughuli wa kiwanda hicho, Paul Aaron
wakati alipohojiwa na gazeti hili ofisi kwake. Na Mpigapicha Wetu.
Posted Jumatatu,Januari27 2014 saa 10:3 AM
Kwa ufupi
- Uchunguzi
uliofanywa gazeti hili ulibaini kuwa baadhi ya viwanda vya kuzalisha
mafuta vimekuwa vikinunua mbegu hizo kwa bei nafuu kwa madai ya kuzitumia
kutengenezea mashudu (chakula cha mifugo) na kuchomea
Bunda. Baadhi ya viwanda Mikoa ya
Mara na Mwanza vinadaiwa kutumia mbegu za pamba zilizooza kwa ajili ya
kuzalisha mafuta ya kula, hali ambayo inahatarisha afya za watumiaji wa mafuta
hayo.
Uchunguzi uliofanywa gazeti hili
ulibaini kuwa baadhi ya viwanda vya kuzalisha mafuta vimekuwa vikinunua mbegu
hizo kwa bei nafuu kwa madai ya kuzitumia kutengenezea mashudu (chakula cha
mifugo) na kuchomea
`boiler’ (chombo cha kuchemshia
malighafi ya mafuta), lakini zimekuwa zikitumika kinyume.
Badala yake zimekuwa zikitumika
kukamua mafuta ambayo kutokana na kuwa machafu, huchanganywa na mafuta mengine
masafi kisha kuingizwa sokoni.
Uchunguzi ulibaini kuwa mchezo huo
umekuwa ukifanyika kwa muda mrefu, kabla ya kugunduliwa na wataalamu wa Mamlaka
ya Chakula na Dawa nchini (TFDA), Kanda ya Ziwa, kutokana na kuwapo kwa
malalamiko mengi kutoka kwa walaji.
Imebainika kuwa TFDA walifanya
ukaguzi wa kushtukiza katika Viwanda vya Bundaa Oil Mill kilichoko wilayani
Bunda mkoani Mara na Brichand Oil Mill Ltd kilichopo jijini Mwanza kutokana na
kudaiwa kujihusisha na mchezo huo.
Meneja wa TFDA, Kanda ya Ziwa, Moses
Mbambe alisema: “Malalamiko ya walaji yalitusukuma kufanya msako wa kustukiza
kwenye Kiwanda cha Brichand Oil Mill Ltd…Wakakiri kuuza mbegu zilizooza kwa
Kampuni ya Bundaa Oil Mill Ltd na katika kufuatilia ndipo tulibaini ukiukwaji
huo wa sheria huo,” alisema Mbambe.
Mbambe alisema uongozi wa Brichand
Oil Mill Ltd ulisema kuwa mbegu hizo waliwapa Bundaa Oil Mill Ltd kwa madhumuni
ya kutengeneza mashudu na siyo vinginevyo, lakini TFDA katika ukaguzi wao
walibaini mbegu hizo zilitumika kwa ajili ya kuzalisha mafuta.
Mkaguzi wa Vyakula katika Mamlaka ya
Mji mdogo wa Bunda, Mafuru Madaraka alikiri kiwanda hicho kuhusika kutumia
mbegu zilizooza kutengeneza mafuta ya pamba.
“Ni kweli tulivamia tukiwa na
wataalamu wa TFDA na kukuta wakizalisha mafuta kwa kutumia mbegu
zilizooza…mafuta mengine yakiwa yameshaingia sokoni na mengine yakiwa
yamehifadhiwa stooni,” alisema Madaraka.
Alisema mbegu hizo zilichukuliwa na
kuamriwa kuteketezwa chini ya usimamizi wao na TFDA, huku uongozi wa kiwanda
hicho ukidai kuwa mbegu hizo waliuziwa na Kiwanda cha Brichand Oil Mill Ltd.
“Inaonekana ni mtandao licha ya kudai
waliwauzia mbegu zilizooza lakini kulikuwa na ndoo za Kampuni ya Brichand Oil
Mill Ltd…Ina maana mafuta yaliyokuwa yanazalishwa ilikuwa kampuni hiyo
iyachukue…Hatujui wanayaingizaje sokoni yakiwa hivyo,” alisema Madaraka.
Viongozi
wa viwanda
Meneja
wa Bundaa Oil Mill Ltd, Rohan Parmar alikiri kukamatwa wakisaga mbegu chafu na
kudai kwamba walipewa mbegu hizo na Kampuni Brichand Oil Mill Ltd.
Alipotakiwa
kufafanua sababu za kukubali kupokea mbegu chafu wakati wakijua sheria
hairuhusu alisema: “Kwanza muda huo nilikuwa Igunga sijui mambo mengi…Sisi
tumepata shida sana tumekosa mbegu sasa tumesimamisha uzalishaji ….Hayo mengine
sipendi kuyasemea.”
Baada
ya gazeti hili kumbana kwamba alikuwapo kama msimamizi wakati TFDA
walipowakamata, aling’aka akisema: “Sasa wewe unataka mambo mengi ya
nini…Walikamata mbegu wakachoma ...Sisi sasa tumefunga kiwanda…Unataka nini
tena…Mimi siwezi kusema mpaka mwanasheria wa kampuni awepo.”
Alipotakiwa
kumtaja mwanasheria ili afuatwe kutoa ufafanuzi, Maramar alikataa akisema:
“Siwezi kusema majina, wala alipo, wala namba…Wewe ‘tafuta’ sisi baada ya wiki
moja.”
Jitihada
za gazeti hili ziliwezesha kupatikana kwa Mwanasheria wa Kampuni, Denis Masami
ambaye alipoulizwa kuhusu uzalishaji wa mafuta kwa kutumia mbegu zilizooza
aliomba apewe nafasi ya kufuatilia kwa kuwa wakati wanakamatwa na TFDA alikuwa
bado hajaajiriwa.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Brichand Oil Mill Ltd, Mohammed Sharif alikiri kiwanda
chake kuwauzia Bundaa Oil Mill Ltd, mbegu chafu lakini kwa kwa ajili ya
kusafisha `Boiler’.
“Walichukua
kwa makubaliano kuwa wanakwenda kusafisha mashudu ili yawe meupe badala ya
mafuta…Maana wana mtambo usio wa kawaida una uwezo wa kuchanganya mbegu
zilizooza na safi ukasaga bila matatizo…Mitambo mingine haiwezi kufanya hivyo,”
alisema.
Wasemavyo
wananchi
Uchunguzi
umebaini kuwa baadhi ya wananchi walilalamikia mafuta yanayotokana na mbegu
hizo, lakini kwa upande mwingine yalikuwa yakipendwa na wakaanga samaki
kutokana na kuuzwa kwa bei rahisi ikilinganishwa na mafuta ya aina nyingine.
Mkazi
wa Kijiji cha Migungani, Bunda ambao Kichere Gikaro (60 alisema kulikuwa na
malalamiko mengi kutoka kwa watumiaji wa mafuta yalitoka katika Kiwanda cha
Bundaa Oil Mill Ltd.
“Hapa
kwetu sisi ndio tulitakiwa kuwa wateja wakubwa kwa kuwa kiwanda kiko
hapa……lakini kutokana na malalamiko ya watumiaji wengi kuhusu ubora wake,
tulilazimika kwenda kununua mafuta mengine mjini, malalamiko
aya
yaliwafikia watu wa afya, lakini hatukupata majibu,” alisema Gikaro.
Muuzaji
wa mafuta katika Soko Kuu la Bunda Mjini aliyejitambulisha kwa jina la Nashon
alikiri kwamba alikuwa na wakati mgumu kuuza mafuta hayo kutokana na
kulalamikiwa kwamba yalikuwa na uchafu pia harufu mbaya.
“Ilikuwa
shida kweli maana licha ya kwamba bei yake iko chini lakini soko lake ni gumu
sana, kama unavyojua sisi wafanyabiashara tunataka unaponunua mali basi itoke
ili pesa yako izunguke,” alisema Nashon.
Naye
Sundi Juma ambaye ni muuza samaki stendi Kuu ya Bunda, alisema yeye anayapenda
mafuta hayo kutokana na ukweli kwamba ni mazito hivyo hayaishi haraka anapokuwa
akikaanga samaki wake.
“Kwanza
mafuta haya ni bei ni nafuu…Ni mazito, ukinunua kidogo unakaanga samaki
wengi…unatumia gharama ndogo, ingawa wateja wanalalamika harufu hasa samaki
wakila lakini kwetu ni nafuu…Maana mafuta mengine bei iko juu na ni
mepesi,”alisema Juma.
Alisema
bei ya mafuta hayo yanayozalishwa na Bundaa Oil Mill Ltd ni Sh 1,400 kwa lita
moja, ikilinganishwa na mafuta aya aina nyingine ambayo yanauzwa Sh2,000 kwa
kiasi hicho.
“Ukinunua
mafuta ya bei kubwa unalazimika kuuza samaki pia kwa bei kubwa, wakaanga samaki
hatuko tayari kununua mafuta ya bei ya juu…Kwa kuwa ukinunua wewe mwenzio
anachukua ya bei ya chini, anauza samaki bei nzuri, wako wanabaki,” alisema.
Juma
alikiri kuwapo kwa watu wanaolalamika kujisikia vibaya hasa wanapokuwa
wanakaanga samaki kutokana na mvuke unaotokana na mafuta hayo kubadili hali ya
hewa na kuwa nzito.
Madhara
kiafya
Mmoja
wa maofisa wa TFDA, Kanda ya Ziwa ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe kutokana
na kutokuwa msemaji wa taasisi hiyo, alisema miongoni mwa madhara yanayoweza
kumpata mtumiaji ni saratani.
“Uzalishaji
wa mafuta hayo hutumia kemikali aina ya caustic soda ambayo kisheria lazima
isimamiwe na mtaalamu, lakini hata mkemia hawakuwa naye…Wanazalisha mafuta kwa
mbegu zilizooza…Wanawalisha watu vitu visivyo stahiki…madhara yake ni makubwa
kiafya,”alisema.
Mfamasia
na mmiliki wa zahanati binafsi wilayani Serengeti Mkoa wa Mara, Thomas Burito
alisema madhara kwa watumiaji wa mafuta hayo ni makubwa kwa kuwa husababisha
mishipa kuziba na matokeo yake ni watumiaji kuugua saratani na figo.
“Matumizi ya mafuta kama hayo
ni hatari kwa maisha ya walaji, kiafya wanaathirika polepole na wengi hupata
kansa, ugonjwa ya moyo, figo na hayo ni magonjwa hatari na mwisho kama
hakuchukua hatua haraka ni vifo,” alisema Burito.
Ofisa Afya wa Wilaya Bunda, Fadhili
Kinyogoli alisema matatizo ya kuzalisha mali zisizo na kiwango na kuziingiza
sokoni ni kubwa kutokana na wananchi ambao ni walaji kutokutoa taarifa kwa
wakati ili hatua ziweze kuchukuliwa.
ZABURI YA 72 ALIYOITUMIA DK,MATHAYO DAVID MATHAYO KUSALI WAKATI MAWAZIRI WALIPOWEKWA KITI MOTO KISHA KUMWAGWA
.1.Ee mungu ,mpe mfalme
hukumu zako, na
mwana wa mfalme
haki yako.
2.Atawaamua watu wako kwa haki, na watu wako walioonewa kwa
hukumu.
3.Milima
itawazalia watu amani,na
vilimaa navyo kwa
haki.
4.Atawahukumu
walioonewa wa watu,atawaokoa wahitaji
, atamseta mwenye kuonea.
5.Watakuogopa
wakati wote wa
kudumu jua,na wakati wa
kung’aa mwezi kizazi
hata kizazi.
6.Atashuka kama mvua
juu ya majani yaliyokatwa,Kama manyunyu
yainyweshayo nchi.
7.Siku zake yeye,
mtu mwenye haki
atasitawi,na wingi wa
amani hata mwezi
utakapokoma.
8.Na awe na enzi
toka bahari hata bahari,Toka mto
hata miisho ya
dunia.
9.Wakaao jangwani na wainame
mbele zake;adui zake
na warambe mavumbi.
10.Wafalme wa
tarshishi na visiwa na
walete kodi,Wafalme wa Sheba
na Seba na
watoe vipawa.
11.Naam, wafalme
wote na wamsujudie,na
mataifa yote wamtumikie.
12.Kwa maana
atamwokoa mhitaji aliapo,na
mtu aliyeonewa iwapo
hana msaidizi.
13.Atamhurumia
aliye dhaifu na maskini,na nafsi za
wahitaji ataziokoa.
14. Atawakomboa
nafsi zao na kuonewa
na udhalimu,na damu
yao ina thamani
machoni pake.
15.Basi na aishi;na
wampe dhahabu ya Sheba;na wamwombee daima;
nakumbariki mchana kutwa.
16.Na uwepo wingi
wa nafaka katika
ardhi juu ya milima;matunda yake
na yaweyawe kama lebanoni,
na watu wa
wastawi kama majani
ya nchi.
17.Jina lake na
lidumu milele,Pindi ling’aapo
jua jina lake
liwe na wazao.
Mataifa yote na wajibariki katika
yeye,na kumwita heri.
18.Na ahimidiwe Bwana,
Mungu,Mungu wa Israeli,atendaye miujiza
yeye peke yake.
19.Jina lake tukufu
na lihimidiwe milele;dunia
yote na ijae
utukufu wake. Amina na
amina.
20.Maombi ya Daudi
mwana wa yese
yamekwisha.
j
MISA YA SHUKRANI YA JUMUIA YA MT.MARIA NA KWAYA YA MARIA PAROKIA YA MUGUMU SERENGETI
PAOKO WA KANISA KATOLIKI MUGUMU SERENGETI,AKIENDELEA NA MISA
KWAYA YA MTAKATIFU MARIA MAMA WA MUNGU WAKIIMBA
WAUMINI WA JUMUIA YA MT.MARIA WAKIPEANA AMANI
TUNAIMBA
POKEA MWILI WA KRISTO
CHAKULA KINAPELEKWA UKUMBINI
NI WAKATI WA CHAKULA
KWAYA YA MTAKATIFU MARIA MAMA WA MUNGU WAKIIMBA
WAUMINI WA JUMUIA YA MT.MARIA WAKIPEANA AMANI
TUNAIMBA
POKEA MWILI WA KRISTO
CHAKULA KINAPELEKWA UKUMBINI
NI WAKATI WA CHAKULA
Subscribe to:
Posts (Atom)



