Subscribe:

Ads 468x60px

SHULE KUKOSA VYOO WALIMU HULAZIMIKA KURUDI MAJUMBANI KUJISAIDIA.



Machi ,2014
Serengeti:WALIMU 37 wa shule ya Msingi Mapinduzi ‘A’iliyoko Mjini Mugumu wilaya ya Serengeti,hulazimika kurudi kwenye makazi yao kujisadia kutokana na shule hiyo kutokuwa na vyoo vya walimu kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Ofisa Elimu wilaya hiyo William Mabanga amekiri kuwepo kwa tatizo hilo,na kudai kuwa ni shule nyingi hazina vyoo vya walimu,kwa kuwa mkazo uliwekwa kujenga vyoo vya wanafunzi wakasahau walimu,na kuahidi kuwa litashughulikiwa kwa kuwa athari yake ni kubwa kwa walimu na watoto.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo James Johannes amesema tatizo hilo lina muda mrefu,mamlaka husika zinataarifa lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kuwanusuru walimu  kwa kuwa wanaodharirika kwa kukosa vyoo na kuokoa muda wa vipindi ambao huvitumia kurudi majumbani kujisaidia.
“ Mwalimu hutumia  zaidi ya dakika 20  kutafuta eneo la kujistiri…hapa ni katikati ya mji hawawezi kukimbilia vichakani…maana  walimu 32 ni wakike , na wakiume 6 ,wanalazimika kwenda kwenye miji yao ama majilani  kujisaidia….na hii ndiyo shule ya mjini,imeachwa hivi…tunaomba mamlaka zichukue hatua maana watoto wanakosa mtiririko wa vipindi kwa tatizo hilo,”alisema Mwalimu kwa masikitiko.
Alisema awali walikuwa wanatumia choo cha kanisa la Sayuni na baada ya kuweka uzio ,wakakosa sehemu ya kujisaidia,na choo cha wanafunzi inakuwa vigumu kwa kuwa nacho kiko katika eneo la mtu na matundu yaliyopo ni 12 kati ya mahitaji ya matundu 32 kwa watoto 890 waliopo hapo shuleni.
“Baada ya kuweka uzio hatuna sehemu ya kujisaidia…kwa mwalimu anayekaa shuleni anaye ana choo cha muda ambacho kinadhalilisha maisha ya walimu….kuhusu vyoo vya wanafunzi tayari tumeishapata notisi maana ni uwanja wa mtu anataka kuendeleza eneo lake….kuna hatari ya shule kufungwa iwapo  atazuia hapatakuwa na jinsi,”alibainisha.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha NHC ,Elias Nyamraba anasema tatizo hilo linawadhalilisha walimu na kukosa morari ya kufundisha ,na inapotokea amepata mchafuko wa tumbo hupata shida,hivyo Matokeo Makubwa sasa hayawezi kupatikana katika mazingira kama hayo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu,afya na Maji wilaya Daniel Kegocha alikiri kuwepo kwa tukio hilo na kuwa walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu kwa kukosa vyoo.
“Nilifika shuleni baada ya kufuatwa na walimu,kweli  hali ni mbaya …maana wanaacha vipindi na kurudi nyumbani kutafuta vyoo kuna athari kubwa kitaaluma…nitalifikisha hili tatizo halmashauri ya wilaya  ili kuona jinsi ya kuchukua hatua za haraka”alibainisha.
Kuhusu choo cha wanafunzi kuwa katika eneo la mtu,diwani hiyo alisema hakuwa anajua na kubainisha yote yanatakiwa kufanyiwa kazi haraka ili kunusuru shule isijekufungwa.
Hata hivyo baadhi ya wananchi walilaumu madiwani kwa kubadilisha matumizi ya eneo la mnada  linalopakana na shule hiyo,viongozi wakajigawia maeneo ambalo lingeweza kutumiwa na shule hiyo ili kuwanusuru watoto wanaokwenda kujisaidia eneo la jilani kwa kuvuka barabara kuu,hali ambayo ni hatari kwa usalama wao.
Kwa mjibu wa taarifa ya wilaya ,inabainisha kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu wa matundu ya vyoo kwa walimu 1,401,ambapo toka mwaka 2009 mpaka 2013 wamejenga matundu 25 tu,upungufu wa madawati ni 16,460,ambapo zaidi ya asilimia 50 wanasoma wakiwa wamekaa chini.
Mwisho.