Subscribe:

Ads 468x60px

MWALIMU AMFANYIA UKATILI MWANAE,AMWEKEA PILIPILI KWENYE VIDONDA NA KUMLAZIMISHA KULA KINYESI CHAKE.



Serengeti:MWALIMU wa shule ya MsingI Morotonga wilayani Serengeti Karata Mugunda anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kumpiga kisha kumlazimisha kula kinyesi mwanae wa darasa la tano aliyedaiwa kujisaidia ndani kwa kuogopa kwenda nje sababu ya giza.
Tukio hilo ambalo limepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi linadaiwa kutokea agosti 13,2013 majira yausiku nyumbani kwa mwalimu huyo anayeishi shuleni,limethibitishwa na Mwalimu mkuu wa shule,polisi,wanaharakati na uongozi wa hospitali teule ya Nyerere ddh.
Akisimulia tukio hilo Mwenyekiti mtendaji wa shirika la Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu wilaya ya Serengeti(Washehabise)Samwel Mewama amesema ,mtoto huyo alisema aliogopa kwenda kujisaidia nje kutokana na giza nene na kujisaidia ndani ,hatua iliyopelekea kupata adhabu hiyo.
“Baba yake licha ya kutambua umri wake na nafasi a;liyonayo aliamua kumfanyia ukatili mwanae ikiwa ni kinyume cha sheria ya mtoto ya mwaka 2009… kumpiga bila huruma…matako yameharibiwa kwa viboko…kana kwamba haitoshi akachukua kitambaa na kuweka pilipili akamwekea…kisha akamlazimisha kula kinyesi chote na hakumpa huduma ya tiba”alisema.
Mewama alisema agosti 14 baba yake alimlazimisha kwenda shuleni ,hata hivyo hakuweza kukaa kutokana na vidonda matakoni”mwalimu wa darasa alipomuuliza na kueleza ,akaona hali aliyonayo akanipigia simu…nilikwenda kumchukua nikampeleka hospitali kupitia polisi”alibainisha.
Alisema kabla ya kwenda alimpigia simu baba yake lakini akamjibu aendelee na hatua anayoona inafaa ,na kulazimika kumfikisha hospitali Teule ya Nyerere ddh,hata hivyo alipokea simu ya vitisho kutoka kwa mwalimu huyo kuwa hana imani na chakula anachompa,hali iliyompelekea kumkabidhi Mwalimu mkuu wa shule hiyo aliyemtaja kwa jina la Mlay,ambaye naye alitishwa na mtuhumiwa.
Kutokana na vitisho hivyo Mwalimu Mlay alilazimika kutoa taarifa polisi na mtuhumiwa kukamatwa na polisi wamesema atafikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya taratibu kukamilika,huku mtoto akiwa amekabidhiwa ndugu zake kwa uangalizi zaidi.
Akiongea kwa wasiwasi mtoto huyo alisema ,hiyo ni mara ya tatu anapigwa na kuumizwa yeye na ndugu zake,na kuwa mama yao aliachika kutokana na vipigo na mama yao mdogo ndiye anawachongea yeye na ndugu zake watano ili wafukuzwe hapo.
Mmoja wa wanafunzi wa darasa la tano jina tunalo alisema tabia ya kupiga si kwa watoto wake tu hana wanafunzi darasani anawachapa bila utaratibu maalum,na walimu wanajua lakini wanaonekana kumwogopa kuwa ni mkorofi.
Baadhi ya walimu wamesema matukio ya kupiga watoto ni ya mara kwa mara lakini hilo ni kubwa zaidi nainapaswa sheria ichukue mkondo wake.
Mganga wa zamu Hooka Paul alisema majeraha hayo ni makubwa na anapaswa kupata kinga ya tetenasi kwa kuwa amechelewa kupata matibabu,na kisaikolojia mtoto huyo ameathirika kwa kuwa anastuka mara kwa mara.
Polisi wanaendelea na mahojiano kwa walimu wengine na wamesema utaratibu ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Mwisho.