Subscribe:

Ads 468x60px

WATHAILAND WAFURAHIA UTALII SERENGETI

 NIKIWA NA MIHAYO NA MUSSA KIKAZI ZAIDI WAKATI WA ZIARA YA WAZIRI MKUU WA THAILAND YINGLUCK SHIWANATRA
 MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPA AKIWA NA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII KHAMISI KAGASHEKI,WENGINE NI MKURUGENZI WA TANAPA ALLAN KIJAZI
 MKUU WA MKOA WA MARAJOHN TUPA,MKURUGENZI WA WANYAMA PORI TANZANIA PROFESA ALEXANDRE SONGORWA NA BAADHI YA WATU WALIOAMBATANA NA WAZIRI MKUU WA THAILAND UWANJA WA NDEGE SERONERA
 CHAKULA HIKI KILITUMIKA KWA WAGENI WA THAILAND NA WATANZANIA HOTEL YA FOUR SESSION SAFARI LTD
WAZIRI KAGASHEKI,KIJAZI NA MMOJA WA WAGENI WALIOKUWEPO ZIARA YA SHINAWATRA

 Utalii wamkuna Waziri Mkuu wa Thailand
Kwa ufupi
Alisema kutokana na ziara hiyo, Tanzania na Thailand zimekubaliana na kutiliana saini mkataba wa miaka mitatu wa ushirikiano katika kulinda, kuendeleza na kukomesha biashara haramu ya wanyamapori.
Dar es Salaam. Ziara ya siku tatu ya Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra imemvutia kiongozi huyo na kuahidi kufanya ziara binafsi katika mbuga za wanyama akiambatana na familia yake.
Akizungumza wakati wa kumuaga waziri huyo aliyeondoka nchini jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki, alisema ziara ya Shinawatra imekuwa ya mafanikio makubwa kwa taifa.
Alisema kiongozi huyo ameahidi kurudi nchini wakati wowote akipata nafasi.
“Amesema anakwenda lakini atarudi katika ziara ya kibinafsi yeye na mume wake, mtoto wake na ndugu zake na tumemwambia akiwa tayari atufahamishe,” alisema Balozo Kagasheki.
Alisema kutokana na ziara hiyo, Tanzania na Thailand zimekubaliana na kutiliana saini mkataba wa miaka mitatu wa ushirikiano katika kulinda, kuendeleza na kukomesha biashara haramu ya wanyamapori.
Mkataba huo ulisainiwa na Balozi Kagasheki na Naibu Waziri Mkuu wa Thailand Plodprasop Suraswad, aliyeambatana na Shinawatra.
Akizungumzia manufaa ya mkataba huo, Waziri Kagasheki alisema utasaidia taifa kuongeza mapato kupitia sekta ya maliasili kwa kuongeza watalii.