Subscribe:

Ads 468x60px

UKUKWAJI HAKI ZA BINADAMU


WALIMU WALALAMIKIWA KWA UBAGUZI WA UKABILA.
Serengeti:UBAGUZI wa kikabila,ukiukwaji wa Haki za Binadamu unadaiwa kutawala zoezi la kuhamisha wafugaji katika kijiji cha Nyamokhobiti kata ya Maji moto  Tarafa ya Ngoreme wilayani Serengeti,umevuka mipaka hadi shuleni .
Ubaguzi huo umeanza kuleta madhara kufuatia baadhi ya watoto wa wafugaji wa jamii ya Wakenye kutoka wilaya ya Butiama waliokuwa wanasoma Isereserekutokwenda shule kwa madai ya ubaguzi kutoka kwa walimu wa shule hiyo ambao wengi ni kabila la Wangoreme wazawa wa kijiji hicho.
Alex Mang’era(68)mfugaji alisema aliingia kijijini hapo mwaka 2003 kwa kuridhiwa na serikali ya kijiji na mkutano mkuu,na wanae watatu wanaosoma hapo kwa sasa hawaendi shule kutokana na ubaguzi ulio ndani ya jamii na walimu wa shule.
“Wanangu Kadogo Alex wa darasa la 6,Neema na Habibu wa darasa 3 hawaendi shule…wanabaguliwa na wanafunzi,jamii nahadi walimu kuwa ni Wakenye warudi kwao Butiama ….wamezaliwa na kuanzia shule hapa..mimi nimekaa miaka 10…nimepiga kura hapa…ubaguzi huu ni mbaya sana”alisema kwa masikitiko.
Alisema shule hiyo yenye walimu 7 watano ni wazawa wakijijini hapo na wanaishi kwenye miji yao ,badala ya kutekeleza majukumu yao wamegeuka kuwa sehemu ya jamii,wanashiriki vikao vya kimila ritongo na matokeo yake wanapeleka ubaguzi shuleni.
 Moroni Nyancharu(30)wa kitongoji Getenga kijijini hapo  anasema katika zoezi hilo mtoto wake  Bhoke Mroni wa darasa la kwanza haendi shule kwa kuhofia usalama wake,na kubaguliwa .
”Walimu wanatutukana sisi kuwa Watoto wa Wakenye ni wajinga hamjui kusoma…na wanafunzi nao wanatutukana kuwa sisi ni watu wa kuja…njiani mkipita jamii inatuzomea kuwa Makenye mrudi wilayani kwenu…hatuna raha shuleni”anasema mwanafunzi wa darasa la tatu jina tunalo.
Ofisa elimu akiri.
Ofisa elimu ufundi wilaya Christopher Mossi alikiri kuwa walimu karibu wote ni wazawa wa kijijini hicho,”ni kweli ni hapo…kwa malalamiko hayo tunafuatilia kwa kuwa yanalenga kuwanyima elimu hao watoto”alisema.
Mwenyekiti  wa serikali ya kijiji cha Iseresere Mosi Ng’ombe alipotakiwa kujibu tuhuma za kuwapokea wafugaji na sasa amewakana,alisema yeye hawezi kulizungumzia hilo labda aulizwe mkuu wa mkoa ama Dc.
Agizo la RC  latekelezwa na wazee wa mila badala yaSerikali ya kijiji.
Katika hali isiyo ya kawaida  ambayo imechangia ukiukwaji wa Haki za Binadamu agizo la Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tupa la kuhamisha  wafugaji haramu linatekelezwa na wazee wa mila chombo kisicho cha kiserikali.
Uamzi huo umelalamikiwa na makundi ya wanaharakati akiwemo Mbunge wa jimbo hilo Dk,Stephen Kebwe ambaye aliiambia blog hii  kuwa chombo hicho hushughulikiwa masuala ya ulinzi na usalama ,lakini hakina nguvu kwa maagizo ya kiserikali kama hayo.
“Zoezi lilikuwa na nia njema lakini njia zilizotumika si sahihi…huwezi tumia ritongo kwa agizo la serikali wakati inavyombo vyake…uonevu ,ukiukwaji haki utatendeka…pia kuna udhaifu katika zoezi hilo maana hakuna waraka wenye maelekezo alioutoa kwa watekelezaji,hii inaweza kuleta vurugu”alisema Mbunge.
Alikwenda mbali zaidi na kudai ameishamwambia mkuu wa mkoa ajaribu kuangalia vema suala hilo kwa kuwa tafsri ya mhamiaji haramu ijulikane,na wabainishwe na wananchi ,kwa kuwa watu walipokea kwa utaratibu ,wameishi miaka mingi,wanamazao,wana vitu kuwaondoa kwa kutumia ritongo hawatapata muda wa kuweka sawa mali zao,wala kusikilizwa.
Wazee wa mila wafunga zizi kwa dawa.
Mbali na malalamiko ya ubaguzi na ukiukwaji haki za binadamu,wazee wa mila wamelazimika kufunga zizi la ng’ombe wa Simion Maitari Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nyamokhobiti kijiji jilani kwa kuweka matawi ya miti ambayo inaaminika kuwa wamezindika ng’ombe wakirudi humo watakufa,na wao ndio wenye uwezo wa kuzindua tego hilo.
 Majeruhi.
Wakati Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara  Ferdinand Mtui na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Iseresere Mosi Ng’ombe kudai kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa wakati wa zoezi la kuwafukuza wafugaji,Mwananchi  imebaini watu wawili kujeruhiwa kwa kupigwa na kukatwa kwa sime.
Polisi kituo cha Maji moto kimekiri kuwapokea majeruhi hao na kuwapa Pf 3 agosti 5 ,mwaka huu iliyosainiwa ditektivu Mohammed ambayo nakala yake tumeiona ,pia hati ya kuwakamata watuhumiwa George Rabani na Mohi Morigo kwa kosa kujeruhi Ref No MAJ/RB/281/2013 hata hivyo hawajakamatwa
Wanaharakati.
Mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu (Washehabise)Samwel Mewama anasema zoezi hilo limekiuka haki za binadamu,kwa kuwa linavunja katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977.
“Ibara ya 17,uhuru wa mtu kwenda atakako,sheria ya 1984  na ibara ya 24 haki ya kumiliki mali,kwa kitendo hiki kilichofanyika ni uvunjaji wa katiba,watu wamekosa haki ,watoto wanashida ya chakula,wameacha mazao,chombo kinachotumika kutekeleza si cha kisheria,tutahakikisha haki inatendeka,maana mhamiaji haramu anawezaje kuchagua kiongozi yeye akawa halali”anasema.
Rc
Mkuu wa mkoa wa Mara John Tupa anasema waraka wake amesambaza kwa wakuu wa wilaya,na kuwa mwisho wa zoezi hilo ni agosti 16 mwaka huu,hata hivyo waraka huo wakuu wa wilaya hawajausambaza kwa viongozi wa vijiji .
Mwisho.