Subscribe:

Ads 468x60px

ABAKA


MWENYEKITI WA KITONGOJI ATUHUMIWA KUBAKA WATOTO WAWILI WA SHULE YA MSINGI,
Agosti 17,2013.
Serengeti;MWENYEKITI wa kitongoji cha Matumaini kijiji cha Miseke kata ya Manchira wilayani Serengeti Machaba Morumbe(53)(CCM)anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kubaka watoto wawili wa shule ya msingi.

Matukio hayo yanayodaiwa kutendeka kwa nyakati tofauti yamethibitishwa na polisi wilaya na Shirika la wasaidizi wa kisheria na Haki za Binadamu(Washehabise)na uongozi wa hospitali teule ya Nyerere ddh yanadaiwa kutokea agosti 9 na 13 katika kitongoji hicho mwaka huu.
                  
Akielezea matukio hayo  akiwa eneo la polisi Mwenyekiti wa shirika hilo Samwel Mewama alisema ,tukio la kwanza linadaiwa kutokea agosti 9 majira ya saa 10 jioni,ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la 5 mwenye umri wa miaka 12 shule ya msingi  Zakhia Meghji kijijini hapo.

“Akiwa machungani alimsihi mtoto huyo apeleke ng’ombe mtoni na kufika huko akambaka,huku akimtishia kutosema…hakusema kabisa licha ya kuwa na maumivu makali…lakini alipata ushujaa baada ya mwenzake kutendewa siku nyingine  naye akawaeleza wazazi wake kuhusu unyama wa kiongozi huyo”alisema Mewama.

Kujitokeza kwa mtoto huyo alipokelewa na dawati la jinsia la polisi Mugumu na kufunguliwa jalada Mug/dawati 148/2013 na kupelekwa hospitali teule ya Nyerere ddh kwa uchunguzi zaidi.

Katika tukio la pili mtuhumiwa huyo kwa mtindo ule ule anatuhumiwa kumbaka  mwanafunzi wa darasa la 3 mwenye umri wa miaka 10  Agosti 11 majira ya saa 11.00 jioni mwaka huu wakati akichunga ng’ombe na mbuzi.

Mtoto huyo alisema mtuhumiwa alimwambia eneo la mtoni kuna malisho mazuri ,walipofika ghafla akamkamata na kumvua nguo na kuanza kumwingilia huku amemziba mdomo,na kumsababishia majeraha sehemu za siri.

Baba mzazi wa mtoto huyo jina tunalo alibaini hali hiyo baada ya kumwona mwanae akiwa katika hali isiyo ya kawaida,na alipoulizwa alibainisha unyama aliotendewa na kiongozi huyo na kuchunguza walibaini amechanika vibaya na kumpeleka hospitali kupitia polisi na kufunguliwa jalada Mug/dawati 147/2013.

Mganga wa zamu hospitalini hapo aliyejitambulisha kwa jina moja la  Nyanokwe aliyempokea na kumfanyia uchunguzi mtoto huyo amebaini kuchanika vibaya sehemu za siri na pia katika nyonga zake.

Mganga mkuu wa hospitali teule ya Nyerere ddh,Dk,Kelvin Mwasha amethibitisha kumpokea mtoto huyo kuwa wamemlaza wakiendelea na matibabu,hata hivyo mtuhumiwa ametoroka kijijini baada ya kusikia anasakwa.

Mwisho.