Subscribe:

Ads 468x60px

WALINZI WAWILI WA BWAWA WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI


WALINZI WAWILI WA BWAWA WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI.

Machi 12,2013.

WALINZI wawili wa bwawa la maji la Manchira lililoko Mamlaka ya mji wa Mugumu wilayani Serengeti wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana na maiti kutelekezwa njiani ikiwa ni pamoja na pikipiki waliyokuwa nayo.

Tukio hilo limethibitishwa na polisi wilayani Serengeti na viongozi wa vijiji vya Kebosongo na Rwamchanga linadaiwa kutokea machi 11 majira kati ya saa 2:00 usiku jilani na sekondari ya Mugumu.

Waliouawa ni Itinde Chacha(43)mkazi wa Kebosongo na William Kamambe(40) mkazi wa Rwamchanga ambao wote walikuwa walinzi katika bwawa hilo.

Akisimulia mkasa huo mdogo wa marehemu Itinde,Emmanuel Chacha alisema mazingira ya mauaji hayo ni ya kupanga kwa kuwa hakuna kitu kilichochukuliwa ,ikiwa ni pamoja na fedha ,simu ,sime,na pikipiki waliyokuwa nayo.

“Kaka yangu tumeachana jana usiku akaaga anaenda kazini na hata mkewe alipompigia simu kama anarudi nyumbani alisema hatorudi kwa kuwa alikuwa anatarajia kumsindikiza mtoto wa kaka yetu kuwahi gari asubuhi”alisema kwa masikitiko.

Alisema machi 12,2013 asubuhi alipata taarifa ya mauaji hayo,”hili huwezi sema ni ujambazi kama hawajachukua kitu,lazima nyuma yake kuna kitu kinaendelea ,uchunguzi wa kina unatakiwa kufanyika”alisema.

Naye Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Rwamchanga Joseph Makuru alisema kuwa Kamambe ambaye ni ndugu yake aliaga kuwa anaenda kazini ,lakini wamepokea taarifa ya mauaji kwa masikitiko makubwa.

“Sisi tumetoa maelezo polisi kuhusu hilo tukio lakini polisi wanatakiwa kufanya uchunguzi wa kina kubaini maana mauaji haya ni ya kupangwa ….wote wamepigwa kichwani risasi inasikitisha sana”alisema.

Polisi wanamshikilia Chacha Nyamhanga  kwa uchunguzi huku wakiendelea na upelelezi ,mtuhumiwa  alifukuzwa kazi ya ulinzi bwawani hapo,hata hivyo inadaiwa alitengeneza chuki na marehemu hao.

“Inasemekana alifikisha malalamiko yake kwa viongozi wa halmashauri akashindwa…akaenda mpaka kwa wazee wa mila kumshitaki Itinde kuwa amefukuzisha kazi…nako akashindwa na akaapa lazima kieleweke na hiyo ni tarehe  8 mwezi huu”kilisema chanzo kimoja.

 
“Sijui ni bunduki za wanyama maana wamechakazwa sana …mashimo ni makubwa sana…wote wamepigwa sehemu moja za kichwani…ni hatari”alisema daktari.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment