Subscribe:

Ads 468x60px

WASHITAKIWA WA MENO YA TEMBO WAACHIWA KISHA KUKAMATWA TENA

WASHITAKIWA WA MENO YA TEMBO WAACHIWA KISHA KUKAMATWA TENA.

“ni waliokuwa polisi kagera na mfadhili wao,kesi yao imehamishiwa
mahakama ya mkoa”

Serengeti.

WATUHUMIWA  wanne wa kesi no 1/2013 ya uhujumu uchumi inayowakabili
waliokuwa askari polisi mkoa wa Kagera na mfadhili wao wamefutiwa
mashitaka na mahakama ya wilaya ya Serengeti kisha wakakamatwa na
kupelekwa Musoma kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka mapya.

Washitakiwa hao Boniphace John Kurwa(31)mkazi wa Geita,Gerald Tuji
Kabalega(33)aliyekuwa askari polisi Bukoba,David Duma
Dalema(36)aliyekuwa askari polisi Biharamulo na Mlangirwa Emmanuel
Paulo(32)maarufu kama Mnywarwanda mkazi wa Biharamulo ambaye anadaiwa
kuwa mfadhili wa mtandao huo waliachiwa machi 25,2013 kisha kukamatwa
na kufikishwa kituo cha Polisi Mugumu.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washitakiwa hao watafunguliwa mashitaka
upya baada ya mwendesha mashitaka wa polisi Paskael Nkenyenge
kujiondoa na kumwachia mwendesha mashitaka wa serikali ili aandae
mashitaka upya dhidi ya watuhumiwa hao na kuhamishiwa Musoma.

Uamzi huo pia unatokana na upande wa mashitaka uliokuwa unaongozwa na
polisi kushindwa kutekeleza ushauri wa Hakimu mkazi mfawidhi wa
mahakama hiyo Amon Kahimba aliyewataka warekebishe mashitaka dhidi ya
washitakiwa kwa kuwa angeweza kuwaachia ,kutokana na udhaifu wake
,hali iliyopelekea Tanapa kwa kushirikiana na Mwanasheria wa serikali
wa mkoa wa Mara kuomba wafutiwe mashitaka kisha kuwakamata upya.

Awali mwendesha mashitaka wa polisi detektivu sajenti Nkenyenge
aliiambia mahakama kuwa januari 5 mwaka huu ,muda na wakati
usiojulikana mjini Mugumu washitakiwa walikamatwa kwa kula njama
kujihusisha na biashara haramu ya nyara za serikali kinyume cha
sheria.

Aliiambia mahakama kuwa siku hiyo walipatikana na meno ya tembo
vipande 18 vyenye zito wa kilogramu 104 yenye thamani ya sh,69,750,000
mali ya serikali.
Kutokana na hati ya mashitaka kusomwa mara nne katika mahakama hiyo
bila kufafanua kila mshitakiwa alipokamatiwa,Hakimu Kahimba machi
12,mwaka huu aliomba mpelelezi wa kesi hiyo,mkuu wa upepelezi mkoa wa
Mara kurekebisha hati hiyo kwa kubainisha kosa ,muda na sehemu
waliyokamatiwa ,kwa kuiacha hivyo kunatoa mwanya kwa mahakama
kuwaachia huru.

Hata hivyo mwendesha mashitaka huyo aliendelea kuacha hati ya
mashitaka kama ilivyokuwa ,hatua ilipelekea mwendesha mashitaka wa
serikali na waendesha mashitaka wa Tanapa kuwasilisha hati ya kufutwa
kesi na kukamatwa kwa washitakiwa na kuandaliwa mashitaka mengine
ambapo watafikishwa mahakama ya mkoa iliyoko mjini Musoma wakati
wowote.


Wakati huo huo watuhumiwa hao wamepandishwa katika mahakama ya hakimu
mkazi wa mkoa wa Mara wakikabiliwa na makosa matatu ya uhujumu uchumi.

Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo Faiser Kahamba mwendesha
mashitaka wakili wa serikali Kainunura alisema washitakiwa hao
wanakabiliwa na mashitaka matatu,ya uhujumu uchumi.

Aliyataja mashitaka hayo kuwa ni kuingia ndani ya hifadhi za
taifa,kuwinda tembo na kukutwa na vipande 18 vya meno ya
tembo,wamepandishwa mahabusu hadi aprili 18,mwaka huu kesi hiyo
itakapotajwa tena.


Mwisho.

0 comments:

Post a Comment