Subscribe:

Ads 468x60px

wakamatwa na smg,rissasi 96 na nyara za taifa


WAKAMATWA NA SMG,RISASI 96 NYARA IKIWEMO MAYAI YA MBUNI,
Na Anthony Mayunga-serengeti
Oktoba 29,2012.

WATU watatu  wakazi wa kitongoji cha Mageriga kijiji cha Motukeri kata ya Natta wilayani Serengeti wamekamatwa na bunduki ya kivita aina ya Smg ,risasi 96,vipande 10  vya nyara za nyama pori na mayai 4 ya mbuni.

Tukio limetokea ikiwa ni siku chache katika kijiji cha Makundusi kata hiyo tembo watatu walidaiwa kuuawa kwa njia ya sumu na meno yake kuchukuliwa na watu wasiojulikana.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara Absalom Mwakyoma amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na watuhumiwa walikamatwa kwa kati ya oktoba 25 na 26 katika maeneo tofauti ya wilaya za Serengeti na Bunda.

Kukamatwa kwao kunatokana na taarifa za wananchi polisi na Tanapa ambao baada ya kukithiri matukio ya ujangili wanahaha kila kona kuhakikisha mtandao huo unadhibitiwa kabla ya kuleta madhara makubwa.

Watuhumiwa wanaoshikiliwa na jeshi hilo ni  Sabasaba Nyagekubwa (31)aliyekutwa na silaha na risasi hizo zikiwa chini ya godoro  wamelalia na kuwataja  wenzake ambao ni Pius Mayengo mkazi wa Kyandege wilayani Bunda na  Timoth mkazi wa Kisii Kenya.

Mkisii huyo alidai kuwa yeye alifika kwa mtuhumiwa huyo kutoa mahari baada ya kumtorosha binti wa mtuhumiwa e ,madai ambayo yanapingwa na baadhi ya majilani kwa madai kuwa huo ni mtandao wao wa kuvusha  nyara kwenda nchini Kenya .

Habari kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo zinadai kuwa Nyagekubwa alikamatwa oktoba 25 majira ya saa 11 alfajiri akiwa kwa hawala yake na kuwampeleka nyumbani walipokuta silaha na risasi zikiwa zimefungwa kwenye mfuko.

Bunduki hiyo aina ya SMG inadaiwa ni ya kisasa  kwa kuwa ina stendi za kusimamisha wakati wa kutenda uharifu,inadaiwa kuingizwa nchini  kutokea nchi za Rwanda na Burundi kupitia Kigoma na mtu mmoja ambaye inadaiwa aliingia kijijini hapo akijifanya mganga wa kienyeji(Sangoma)

Sangoma huyo ambaye jina lake limehifadhiwa  anasakwa alitajwa na mtuhumiwa kuwa ndiye aliyeingiza silaha na risasi kwa lengo la kuwindia tembo na uhalifu mwingine na  kuwa hata soko la nyara ndiye anajua.

Watuhumiwa  walikutwa harusini .

Kwa mjibu wa habari hizo inasemekana watuhumiwa wengine walifanikiwa kutoroka baada ya kukutwa kwenye harusi na polisi katika kudhibiti watu wote watuhumiwa wakafanikiwa kutoroka .

Wengine walitaarifiwa kwa simu na kutoroka na nyara.

Habari hizo zinasema kuwa  watuhumiwa wengine walitaarifiwa na hawala wa Nyagekubwa  kwa njia ya simu baada ya polisi kuchukua simu ya mtuhumiwa na wengine huku moja ikifichwa ndiyo ilisaidia watuhumiwa kutoroka na nyara walizokuwa nazo.

Mtuhumiwa anakesi mbili za nyara kwa majina tofauti.

Imebaini kuwa mtuhumiwa Nyangekubwa anakabiliwa na kesi mbili za kukutwa na nyara kwa majina tofauti na moja akidaiwa kuruka dhamana na alipokamatwa kwa tukio kama hilo aliandika jina lake halisi.

Kesi ya kwanza aliandika jina la Ndalahwa Makaranga  tukio la mwaka 2010 ambalo aliruka dhamana.

Silaha za kivita huingizwa kutokea Kigoma.
Matukio ya watu kuingiza silaha kutokea mkoani Kigoma yanazidi kushika kasi kwa ajili ya uwindaji wa tembo na uhalifu mwingine,ikiwemo mtandao uliowahi kutikisa bunge lililopita kwa kuwataja watuhumiwa ambao walipewa dhamana kinyamera licha ya kukamatwa na Smg 4 na risasi zaidi ya 460.

Watuhumiwa walifutiwa kesi.
Hata hivyo wale watuhumiwa waliokamatwa na shehena ya silaha hizo na kelele kusambaa hadi bungeni walifutiwa mashitaka kinyamera katika mazingira ambayo inadaiwa kutawaliwa na rushwa kwamba hawana mashitaka ya kujibu.

Kuachiwa kwao kuliibua maswali mengi kutoka Tanapa kwa kuwa wanakamata watuhumiwa  na vielelezo ikiwemo bunduki za kivita lakini polisi huwaachia linadaiwa kusimamiwa na aliyekuwa mkuu wa upelelezi wilaya ya Serengeti,ambaye kutokana na kashifa hiyo ameshushwa cheo na kupelekwa ofisi ya kamanda wa upelelezi mkoa wa kipolisi Tarime na Rorya.

Hata hivyo baada ya kubainika waliachiwa kwa mazingira ya rushwa watuhumiwa baadhi walikamatwa tena kwa maelekezo ya ngazi za juu za jeshi la polisi na wako chini ya kamanda wa polisi mkoa wa Mara huku wakiendelea kuwasaka wengine.

Mwisho,itaendelea.
























































































0 comments:

Post a Comment