Subscribe:

Ads 468x60px

WATENDAJI WA MAMLAKA YA MJI WA MUGUMU WATAHADHALISHWA


MIONGONI MWA MAJALALA YANATAKIWA KUONDOLEWA NI HILI LILIKOANZISHWA UWANJA WA WAMICHEZO WA NHC 




MAMLAKA YA MJI WA MUGUMU WAPEWA ONYO.
WATENDAJI wa Mamlaka ya  Mji Mdogo wa Mugumu Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wameagizwa kuhakikisha huduma ya maji,kuwasha taa za barabarani na usafi wa 
mazingira inatolewa kwa uhakika .
Kaimu Mkuu wa wilaya hiyo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe akiongea na wafanyabiashara wa Mji huo kwenye ukumbi wa bwalo la Magereza  kuhusiana na maandalizi ya maadhimisho ya siku ya mto Mara ,amesema mji huo utapokea wageni zaidi ya 200 kutoka ndani na nje ya nchimwezi septemba.
Amesema hatawaonea aibu watendaji wasiotimiza wajibu wao,hivyo wanatakiwa kuhakikisha kuanzia sasa madampo waliyoanzisha kila  kona,yanaondolewa,maji yapatikane na taa za barabarani ziwashwe.
Aidha amewataka wafanya biashara wa mjini hapo kuchangamkia fursa hiyo ambapo wanatarajia kutumia zaidi ya mil.200 kwa wiki hiyo ya maonesho na maadhimisho hayo yatakayofanyika septemba 15 mwaka huu  ambayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Mohammed Ghalib Bilal.
Amewataka kuboresha sehemu zao za biashara ikiwemo nyumba za kulala,hoteli,migahawa ili waweze kunufaika na maaadhimisho hayo yanayotaraji kushirikisha washiriki kutoka Nchini Kenya,na mikoa yote ya kanda ya ziwa ,ambayo pia yatahitimishwa kwa kushuhudia tukio la nyumbu wanavuka Mto Mara kutokea hifadhi ya Maasai Mara kuingia hifadhi ya Taifa yaserengeti.
Hata hivyo  baadhi ya wafanyabiashara wamemwambia kuwa kikwazo katika mji huo ni maji,umeme usiokuwa wa uhakika ikiwemo taa za barabarani kutowashwa kunapunguza usalama wa mji huo,na mamlaka kugeuza maeneo ya michezo  ya watoto kuwa madampo ya takataka.
Mwisho.