Subscribe:

Ads 468x60px

UTEGEMEZI WA MISAADA CHANZO CHA KUKARIBISHA USHOGA.



Padri Alois Magabe wa kanisa Katoliki Mugumu wilayani Serengeti
Serengeti:Nchi za  Magharibi kutoa misaada yenye masharti ya kuruhusu ushoga kwa nchi za Kiafrika ni matokeo ya kushindwa kutumia rasilimali walizo nazo kwa ajili ya kuendesha nchi zao.
Hivi karibuni kumekuwa na mjadala kwa nchi nyingi za Kiafrika kutokana na shinikizo la Nchi za Magharibi kuzishinikiza nchi za kiafrika ili zipate misaada zinatakiwa kukubali ndoa za jinsia moja.
Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Fransisco wa Asizi Mugumu wilayani Serengeti Alois Magabe  hivi karibuni akihubiri wakati wa misa ya Ekaristi Takatifu alisema utegemezi wa misaada ndiyo chanzo cha nchi hizo kutoa masharti yanayokinzana na maagizo ya Mungu kwa nchi za Kiafrika.
“Ukristo umeanzia nchi hizo za Magharibi miaka zaidi ya elfu mbili iliyopita….licha ya kujua masharti wanayoyatoa yanakinzana na maagizo ya Mungu aliyeweka ndoa ya mme na mke…..leo nchi kama za Marekani na Uingereza na washirika wao wanaziwekea masharti hayo   nchi zinazotaka misaada…sababu kubwa ni udhaifu wan chi hizi zenye rasilimali tele kutegemea misaada”alisema.
Alisema masharti kama waliyotoa kwa Uganda ni ishara tosha kuwa hawamuogopi Mungu ,na kuzitaka nchi zingine kuungana na msimamo wa Uganda kupinga ushoga kwa kuikataa misaada hiyo inayokweza utu wao ”misaada kama hii hatuhitaki bora ipotelee mbali huko”alisema na kushangiliwa.
Hata hivyo aliwataka viongozi wan chi hizo kubadili mitizamo ya kutaka kusaidiwa wakati utajiri walionao unazidi hata nchi hizo zinazotoa misaada kwa masharti,kwa kuwa wao wana nidhamu ya kukusanya na kutumia si kama ilivyo kwa nchi za kiafrika hakuna nidhamu ya matumizi ya mali za umma.
“Hiyo misaada yenye masharti wanayotaka kutoa kwa nchi zetu hizi wamekusanya Afrika kiujanja ujanja wanataka kuileta kwa masharti ya kijinga kijinga kisha wapata nafasi ya kuchota rasimali zetu”alisema.
Katika hatua nyingine alitaka serikali wilayani hapo kuhakikisha inamaliza mgogoro wa ardhi kati ya kigango cha Nyamburi cha kanisa Katoliki na serikali ya kijiji ambayo imeanzisha mnada kwenye eneo la kanisa ,hatua ambayo inaweza kuleta uvunjifu wa amani.
“Suala hili toka mwaka jana oktoba nimewaeleza lakini hakuna utekelezaji…..eneo la kanisa limeporwa kwa nguvu na baadhi ya viongozi wabovu wanaotumia nafasi zao vibaya ili kutafuta kura katika uchaguzi ujao….kwa hili nimewaandikia polisi nao wameahidi kufuatilia,maana suala hilo linaweza kupelekea uvunjifu wa amani”alibainisha.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment