Subscribe:

Ads 468x60px

DIWANI APIGWA


DIWANI APIGWA NA MTOTO WA KAKA YAKE KWA SABABU ZA KISIASA
Na  Blog
Oktoba 7,2013
Serengeti:DIWANI wa kata ya Majimoto  wilayani Serengeti Mkoa wa Mara Rashidi Mugare(CCM)amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ,baada ya kupigwa na mtoto wa kaka yake kufuatia ugomvi unaodaiwa kuwa wa kisiasa wakati wanakunywa pombe.
Tukio hilo limetokea oktoba 5 ,majira ya usiku mwaka huu limethibitishwa na polisi wilayani  hapa ambao wanamshikilia mtuhumiwa Makuri Chacha(36)kutokana na tuhuma za kumpiga diwani  na kumjeruhi sehemu za pua na mdomo.
Akiongea kwa njia ya simu na Blog hii kwa njia ya simu  diwani huyo amekiri kushambuliwa na kuwa hali yake kwa sasa si nzuri na anatarajia kwenda hospitali ya Mkoa Musoma kwa ajili matibabu,huku akishindwa kubainisha chanzo cha ugomvi huo.
“Huyo ni mtoto wa kama yangu ninayemfuata…alinishambulia vibaya sana na kuniumiza …huyo amewahi kumpiga mke wangu wakati wa uchaguzi wa 2010 akamuumiza…tukakaa kama familia tuakayamaliza…ana kisa na mimi kwa masuala ya kisiasa maana wao wako CUF”alisema.
Alipotakiwa kuelezea chanzo ni nini akisita sita ,kisha akasema”kuna mwenyekiti mmoja wa Cuf amekataliwa na wananchi wao wanahisi mimi nilihusika kumng’oa …ndipo siku hiyo nilipowakuta baa kukatokea mgogoro kisha wakaanza kunishambulia kwa maneno …hatimaye akanivaa na kunipiga “alisema.
Mmoja wa viongozi wa serikali ya kijiji jina limehifadhiwa alisema kisa ni diwani kwa kushirikiana na ofisa mtendaji wa kata kufanya mapinduzi ya nafasi ya Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nyamokhobiti Gidion Maitari(CUF)kwa madai kuwa anawashitaki wananchi walioshiriki zoezi la kuhamisha mifugo yake na kumsababishia hasara kwa mingine kufa,na kupotea.
“Baada ya kufanikisha mapinduzi hayo diwani na timu yake walikutana baa wakaanza kusherehekea kuwa wamefaulu…mwenyekiti akakata rufaa kwa Ded na Dc na kupewa tuhuma akazijibu…kwa majibu hayo timu yake nayo ilikutana na kuanza kujipongeza kama walivyofanya diwani na wenzake…ndipo diwani akaingia kwenye kikao kisichomhusu “alisema.
Shuhuda huyo alisema kitendo cha diwani kuingia baa waliyokuwa wanakunywa kundi lisilo lake kuliibua mzozo na kutupiana maneno kwa misingi ya kambi,ndipo mtuhumiwa akamsukuma diwani ambaye alikuwa amelewa akaangukia pua na kuumia.
“Vurugu zilikuwa kubwa kwa kuwa kaka ya diwani John Mantage alimpiga na tofali Bwire Masisi ambaye aliwahi kugombea udiwani kwa tiketi ya Chadema kwa misingi kuwa anashabikia mwenyekiti wa CUF…kwa kuwa hao ni ndugu ugomvi ukawa mkubwa ukahama kwenye koo ukawa wa mlengo wa kisiasa Cuf na CCM “alibainisha.
Hata hivyo Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi mtendaji wanatarajiwa kufika kijiji cha Nyamokhobiti oktoba 8 kujiridhisha na hatua zilizotumika kumkataa mwenyekiti kama ni za kisheria au ni kikundi cha watu wachache.
Mwisho.