Subscribe:

Ads 468x60px

MSHITAKIWA WA MAUAJI AIDUWAZA MAHAKAMA ,AIBUKA NA KUDAI ALIUA APATE UTAJIRI.



Oktoba 26,201
KATIKA hali isiyo ya kawaida Mshitakiwa wa mauaji ya dreva bodaboda Gwitembe Yagera (68)mbele ya Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Serengeti aliibuka na kudai kuwa yeye ndiye aliua lakini kwa kudanganywa na Sangoma kuwa akipeleka damu ya mtu atakuwa atatajirika.
Mshitakiwa huyo Suguta Turuka(19)mkazi wa kijiji cha Kenokwe wilayani hapa licha ya kuambiwa hatakiwi kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka kisheria kusikiliza kesi za mauaji aliibuka na kudai kuwa ameyatenda hayo kutokana na kudanganywa na mshitakiwa mwenzake.
“Mheshimiwa hakimu nilifanya mauaji hayo mwenyewe baada ya kudanganywa na mshitakiwa mwenzangu ambaye ni mganga wa kienyeji…nilimuua Gwitembe muda mfupi baada ya kutoka kupiga ramli na kuambiwa  kama nataka kuwa tajiri nilete damu ya mtu yeyote…nikaamua kumkodi kisha nikamuua”alisema mshitakiwa na kuifanya mahakama kubaki katika mshangao mkubwa.
“Mganga alinipa masharti mbalimbali ikiwemo kuua na pia kupeleka maziwa ya ng’ombe yenye cream na kuchemshwa pamoja na mafuta ya kasuku .…vikawekwa ndani ya kopo…akasema nisifungue na kuwa nitakuta fedha nyingi siku ya kufungua….na kuwa nikikamatwa nisimtaje..hata hivyo sikupata kitu zaidi ya kuua na kukamatwa”alisema.
Mapema Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Franco Kiswaga mwendesha mashitaka wa polisi Paskael Nkenyenge aliiambia mahakama hiyo kuwa Suguta na Marsha Severino(43)ambaye ni Sangoma anayeishi Mugumu mjini wanashitakiwa kwa kosa la mauaji ya dreva boda boda Gwitembe Yagera(68).
Akisoma maelezo ya shauri la mauaji namba 27/2013 alisema washitakiwa walitenda kosa hilo oktoba 3 majira ya saa 9:00 arasili mwaka huu mpakani mwa kijiji cha Nyichoka na Kenokwe eneo lenye vichaka vingi ambapo kuna kuna mto Nyamburu ,ambapo mshitakiwa Turuka alifanya mauaji hayo ikiwa ni muda mfupi ametoka kupiga ramli kwa Severino.
Na kuwa mshitakiwa wa kwanza Suguta alimkodi marehemu Gwitembe aliyekuwa anaendesha pikipiki aina ya Toyo yenye namba za usajili T608 CKJ kwa lengo la kumpeleka nyumbani kwao Kwitete,lakini baada ya kufika eneo hilo alimtaka asimame wajadiliane,ghafla alichomoa kisu na kumchoma sehemu ya kifua upande wa kulia na kuanguka huku yeye akikimbia na kuacha kisu kikining’inia.
Hakimu Kiswaga aliamru washitakiwa warudishwe mahabusu hadi novemba 7 mwaka huu kesi hiyi itakapotajwa tena.
Mwisho.