Subscribe:

Ads 468x60px

KANISA KATOLIKI LAZINDUKA



ILI kukabiliana na changamoto za kidunia  zinazochangia kuporomoka kwa Imani ,maadili na ukiukwaji wa utawala bora kwa waumini na viongozi  kanisa  Katoliki hapa nchini limeanza kujitathimini na kuweka mikakati mipya.
Akitoa semina wakati wa ibada ya misa kwa waumini wa kanisa katoliki Parokia ya Mugumu katibu wa baraza la maketikisa jimbo la Musoma Antony Marwa alisema hatua hiyo ya haraka imetokana na tafiti zilizofanywa na wataalam wa kanisa na kukabidhi baraza la maaskofu Tanzania.
Alisema licha ya waumini kuongezeka ndani ya kanisa katoliki imani inazidi kushuka kwa kuwa hawajengwi kwa misingi mizuri na wanayumbishwa na changamoto nyingi za kidunia ikiwemo suala la madhehebu mengine.
“Kanisa limeruhusu dunia kuingia ndani na kuporomosha imani za waumini…watu wanaingia kanisani wamevaa nguo zisizo na staha …waumini hawasemi,viongozi wa kanisa wako kimya…lakini waumini wakiulizwa wanasema kanisa linaruhusu….wapi kanisa limeruhusu uchafu kama huo?”alihoji.
Alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa watakao ingia kanisa na vimini,wanaume wamevaa mregezo na heleni wafukuzwe kabla ya kuingia,na kwa wanaotoa komnio wasiwape kwa kuwa hawana sifa stahiki.
“Suala la ulevi kuna watu wanasema kanisa linaruhusu…wapi imeandikwa kwenye biblia kuwa wamewaruhusu kulewa…muwe watu wa kiasi….haya si maadili mema kwa viongozi wa kanisa na waumini lazima mageuzi yafanyike ili kujenga imani ya waumini”alisema na kushangiliwa na kanisa zima.
Akizungumzia suala la utawala bora kanisani alielezea kuwa viongozi wanaochanguliwa na waumini kuongoza baraza la walei wanatakiwa kuwa wawazi kwa kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa waumini,ikiwemo vyanzo vyao na jinsi fedha wanazochanga zinavyofanya kazi.
“Kila wakati harambee harambee kanisani  hawasemi zinazochangwa zinafanya nini…kanisa linakwenda bila bajeti,fedha zinakusanywa kila wiki zinaishia mifukoni benki haziendi…wekeni bajeti za kuhudumia nyumba za mapadri na watawa na huduma za kiroho zinazobaki zipelekwe benki”alisema.
Katekista huyo alisema kukosekana kwa mipango kwenye makanisa kumepelekea elimu ya dini haifundishwi kwa kuwa walimu wa dini hawalipwi,wanaishi maisha magumu huku fedha zikitumiwa vibaya na imani ikiporomoka makanisani.
“Maktekista hawathaminiwi wakati ndio wanafundisha waumini wakabatizwa na kupata kipaimara…shukrani wanachangia mapadri na maaskofu waliofundisha hawapati kitu…wamekata tamaa ndiyo maana hawafundishi..wanaingiza waumini wengi wakabatizwa lakini wasiokuwa na misingi ya imani maana hawana mafunzo…wanawafanya walimu wa dini kama kibao cha matofali kikimaliza kazi hutupwa”alisisitiza.
Alisema maazimio hayo yanayotokana na semina ya wiki nzima iliyoshirikisha majimbo yote Tanzania ilifanyikia Kurasini Dar es Salaam yanatakiwa kufanyiwa kazi ili ujumbe wa Papa  mstaafu Benedict wa 16 wa kutangaza mwaka 2013 na 14 kuwa wa imani uweze kutimia.
Mwisho.