Subscribe:

Ads 468x60px

WANANCHI WAUA WATATU KWA TUHUMA ZA WIZI-BUTIAMA


WATATU WAUAWA NA WANANCHI KWA KUWATUHUMU KUHUSIKA NA WIZI-MARA

Oktoba 11,2013
WAKAZI wa Bukima wilaya ya Butiama mkoani Mara wamewaua watu watatu  kwa kuwakata kwa mapanga,kuwapiga mawe sehemu mbalimbali za mwili baada ya kuwatuhumu kuhusika na jaribio la wizi  katika kijiji cha Kwitare  kata ta Makojo.
Tukio hilo limetokea oktoba 8 majira ya saa 12:00 alfajiri kijijini hapo limethibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Mara,mkuu wa wilaya hiyo na uongozi wa kijiji.
Waliouawa ni Masola Magesa Magoti(40)mkazi wa Bukima ,Sagaya Mussa Sagaya(30)mkazi wa kijiji cha Bugoji wilaya ya Butiama, ambaye inadaiwa alikuwa mwizi sugu na alikuwa chini ya uangalizi wa polisi kutokana na kuhusika katika unyang’anyi wa kutumia silaha,na Chikaka Chikaka(32)mkazi wa kijiji Tegeruka.
Mkuu wa wilaya hiyo Anjelina Mabula amesema kutokana na kukithiri kwa matukio ya wizi na mauaji amesema itapigwa kura ya siri kijijini hapo kubaini watu wanaijihusisha na wizi,mauaji na wanaowahifadhi ili hatua ziweze kuchukuliwa.
Amesema sambamba na upigaji kura za siri pia kutakuwa na madaftari ya wakazi wa kila kitongoji ,kujua wageni wanaoingia,na kuwa kukitokea uhalifu viongozi wa eneo hilo watashughulikiwa.

Hata hivyo baadhi ya wananchi wamesema kuwa uamzi huo ni matokeo ya kukosa imani na polisi kwa kuwa watuhumiwa wakifikishwa kituoni huachiwa na matukio yanazidi,hivyo njia pekee ya kukomesha uhalifu ni kuwaua.

Maelezo hayo yamepingwa na kaimu mkuu wa polisi wilaya ya Butiama Abubakari Kunga kuwa wananchi wanapotakiwa kwenda kutoa ushahidi hawaendi na matokeo yake watuhumiwa huachiwa.

Kauli ya wananchi kukoma imani na vyombo vya serikali yamesemwa pia na Dc wa Tarime John Henjewelle kuwa wanapoitwa kuchukua majeruhi polisi husema hawana mafuta,lakini muda huo huo wakiambiwa kuna magendo mafuta hupatikana.

Hali hiyo pia inajitokeza kwa askari wa taasisi za uhifadhi tembo wanapovamia mashamba na makazi ya watu,hudai hawana magari,risasi ama mafuta ,lakini wakiambiwa kuna jangili magari humiminika eneo hilo kwa muda mfupi. 

Kamanda wa polisi mkoa wa Mara Fernandi Mtui amewataka wananchi kutojichukuliwa sheria mikononi kwa kuwa ni kosa,badala yake wawapeleke watuhumiwa polisi na watoe ushirikiano wanapohitaji,hata hivyo hakuna mtu anashikiliwa kutokana na tukio hilo.
Mwisho.