Subscribe:

Ads 468x60px

WANASHERIA(AG)KENYA,UGANDA NA RWANDA WAFUNGULIWA MASHITAKA MAHAKAMA YA A.MASHARIKI



 Wakili Jimmy Obedi kushoto akiwasilisha maombi ya kufungua kesi katika mahakama ya Afrika Mashariki kuitaka mahakama hiyo itoe amri ya kusitisha utekelezaji wa maazimio ya vikao vitatu vilivyoshirikisha Uganda,Kenya na Rwanda kwa kuwa ni ukiukwaji wa vifungu vya sheria ya jumuiya hiyo,anayepokea ni afisa wa masijala ya mahaka hiyo Richard Ogoti kwa niaba ya msajili wa mahakama hiyo




 Wakili Jimmy Obedi mwenye miwani akipokea hati maalum kutoka kwa karani wa masijala wa mahakama ya Afrika Mashariki Richard Ogoti mara baada ya kuwasilisha maombi na kufungua kesi namba 9/2013 iliyofunguliwa na watu watatu(picha zote na Blog hii)


WAFUNGUA KESI MAHAKAMA YA A.MASHARIKI
Novemba 18,2013

Arusha-
WANASHERIA wakuu wa nchi  za Kenya,Rwanda na Uganda wamefunguliwa mashitaka katika Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutokana na kukiuka vifungu vya Mkataba wa jumuiya hiyo.

Maombi namba 6 kesi namba 9/2013 imefunguliwa na wanajumuiya hiyo Ally Msangi,David Makata na John David Mbendo wanaowakilishwa na wakili Jimmy Obedi wa kampuni ya Jimmy Obedi ya jijini Dar es salaam imepokelewa leo na afisa masijala wa mahakama hiyo

Boniphace Ogoti  kwa niaba ya msajili.

Mbele ya waandishi wa habari wakili Obedi amesema wamewasilisha maombi ya kutaka maazimio yote ya vikao vilivyofanyika juni 24,25 mwaka huu Entebe Uganda,kikao cha agosti 28,2013 Mombasa na oktoba 28,2013 Kigali Rwanda bila kushirikisha nchi mwanachama ambaye ni Tanzania.

“Lengo la maombi haya ni kuzuia utekelezaji wa maamzi yaliyofikiwa kwenye vikao hivyo kwa kuwa ni kinyume na vifungu vya mkataba wa jumuiya,ibara ya 71(f)71(b) na vingine….mahakama itoe amri ya kusitisha vikao vyote vinavyoendeshwa kinyume cha sheria ya jumuiya .... tumeomba maombi hayo yasikilizwe upande mmoja na kutoa uamzi wa kusitisha utekelezaji huo”amesema wakili.

Wakili huyo amesema wakati kesi hiyo ikisubiri kupangiwa jaji watu wengine kutoka katika jumuiya hiyo wanaruhusiwa kujiunga na walalamikaji hao ,kwa nia ya kuhakikisha mkataba wa shirikisho hilo unafuatwa kwa mjibu wa  vifungu vya sheria iliyounda shirikisho hilo.
.
“Hapa walalamikiwa ni wanasheria wakuu wan chi hizo tatu ambao marais wao wamekuwa wakikutana kinyume cha mkataba wa shirikisho la jumuiya ya Afrika Mashariki….na sisi tunataka sauti ya kimahakama ya kusitisha utekelezaji wa maazimio yao… mahakama ndio chombo kikuu kitakachotoa tafsri si siasa tena…amebainisha wakili.

Kwa upande wake Msangi ambaye amewakilisha walalamikaji wenzake mahakamani hapo amesema kuwa wamefikia uamzi huo ili kupata ufafanuzi wa kisheria kwa kuwa taarifa zinazotolewa na wanasiasa zinawachanganya wananchi wan chi zote ili kujua hatima ya shirikisho hilo.
mwisho.