Subscribe:

Ads 468x60px

ABAKA NA KULAWITI MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI


                                
.

MWANAFUNZI wa darasala tano mwenye umri wa miaka (12) shule ya msingi(Nyichoka)wilayani Serengeti amelazwa katika hospitali ya wilaya akiguza majeraha ya kubakwa na kulawitiwa na mkazi mmoja wa kijiji cha Matare wilayani humo.
Mratibu wa dawati la jinsia la polisi wilaya Wp Sijali Nyambuche amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Marwa Ibrahimu(33) ambaye anadaiwa kutenda unyama huo Novemba 20 majira ya saa 2 usiku katika kitongoji cha Bukore kijiji cha Nyichoka kata ya Kyambahi.
Alisema mtuhumiwa huyo ambaye wanamshikilia alimfanyia ukatili(jina limehifadhiwa)baada ya kumkamata kwa nguvu na kumchania nguo zake  za siri  .
“Siku ya tukio mtuhumiwa ambaye anafanya kazi kwenye roli la kusomba mawe,walifika kijijini hapo ili kununua mawe na mchanga…mtoto huyo alikuwa na mawe aliyokusanya kwa ajili ya kuuza apate fedha za mahitaji yake ya shule…gari liliharibika wakashindwa kuondoka na kulazimika kulala….ndipo usiku akamfanya ukatili huo”alisema mratibu wa dawati.
Nyambuche alisema kuwa kabla ya kumfanyia unyama huo usiku mtuhumiwa aliombwa kuwa mlinzi wa gari hilo na kusindikizwa na  mtoto huyo kuelekea kwenye gari,ghafla akamkamata na kumwingiza ndani ya gari na kumtendea unyama huku akimtishia kumuua.
“Tulimpkea mtoto huyo na kumpeleka hospitali kwa matibabu baada ya kupata PF3 kwa ajili ya matibabu  na uchunguzi zaidi ili kubaini amejeruhiwa kiasi gani na kama amepata magonjwa ya zinaa”alisema Nyambuche.
Akiongea kwa kusita sita mtoto huyo alisema baada ya kufika kwenye gari mtuhumiwa alimlazimisha kupanda ndani ya gari,alipokataa  akanishika kwa nguvu na kumpandisha ndani ya gari  akafunga mlango na kuchana nguo zake za  ndani na kuanza kumlawiti na baadae kumbaka na kuchanika sehemu zote na damu pamoja na kinyesi kutoka mfululizo.
“Nilipochelewa kurudi nyumbani usiku huo mama alniifuatilia…nilipomsikia nilimwita nikilia…akamkuta  mtuhumiwa akiendelea kunifanyia maneno ya aibu..akapiga yowe wananchi wakajitokeza na kuanza kumpa kipigo mtuhumiwa na kumpeleka polisi.”alisema.
Waganga katika hospitali ye Nyerere wamesema hali ya motto huyo inaendelea vizuri na polisi wanasema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote.
Matukio hayo yanatokea ikiwa wanaharakati wametawanyika nchi nzima katika kampeini za siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.      
MWISHO.