Subscribe:

Ads 468x60px

posho ya sensa ya tsh,15,000=yakataliwa na wenyeviti wa vitongoji Tarime


WENYEVITI WAKATAA POSHO YA SENSA TSH,15,000=,

Makarani wahofu kukabidhi madodoso mpaka walipwe,
Na Anthony Mayunga-Mara.
Septemba 5,2012.


WAKATI zoezi la Sensa likiongezewa siku hadi tarehe 8,viongozi wa vitongoji wilayani Tarime wamekataa kupokea malipo ya tsh,15,000 kwa  siku zote za kazi hiyo.

Hali hiyo inatokana na kutofautiana kwa Malipo hayo kwa kila wilaya ndani ya mkoa mmoja ,licha ya wote kudai waraka kutoka ofisi ya mkoa.

Baadhi ya wenyeviti wa vitongoji wilayani humo ambao hawakupenda kutaja majina yao waliliambia gazeti hili kuwa hawako tayari kulipwa kiasi hicho kwa kazi hiyo waliyoifanya.

“Tumezoea kutumiwa kama watu tusiokuwa na majukumu ya kifamilia,toka utekelezaji wa miradi hadi sensa,yaani unalipwa tshs  15,kwa siku 7 wastani wa tsh,2,000= kwa siku ambazo hazitoshi hata mlo wa mchana,hii ni dharau kubwa sana”alisema mmoja wao.

Walidai kuwa walilazimika kuacha shughuli za kilimo na kushinda wakizunguka na makarani ambao walikuwa wakipwa tsh,35,000= kwa siku, na kuwa wameamua kuziacha ili serikali ifaidike.

“Wengine kwa kazi hizi hizi walilipwa tsh,50,000= wilayani Serengeti,Bunda tunasikia walilipwa tsh,20,000= sisi tsh,15,000= mkoa huo huo kuna kitu kinaendelea maana hata fedha ya uhamasishaji watu wamekula sisi ndio tulifanya kazi ya hamasa na kushawishi wananchi”walisema .

Walisema hata posho kwa mwezi wenyeviti wa vijiji kwa wilaya hiyo wanalipwa tsh,5,000= kwa mwezi licha ya kuwa wanakabiliwa na kazi nyingi za kuhamasisha maendeleo.

Mratibu wa sensa wilaya hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Juma alikiri wenyeviti kukataa fedha hizo kwa madai kuwa ni kidogo.

“Ni kweli wamekataa tunaendelea kushughulikia ili waweze kuchukua kwa kuwa hawakuwemo kwenye hesabu,waliokuwa wanatajwa ni wenyeviti wa mitaa,watendaji wa vijiji na kata ,hivyo sisi hatuna mitaa tukawaingiza wenyeviti”alisema.
Alisema kuwa katika utafiti wake alibaini kuwa wilaya hiyo inalipa kiasi kikubwa ikilinganisha na Rorya na Serengeti ,hata hivyo wilaya ya Serengeti walilipa tsh,50,000 kama ilivyokuwa imeelekezwa awali,lakini mkoa ukabadilisha viwango.

Kwa wilaya ya Rorya wenyeviti wa vitongoji walilipwa tsh,10,000= kama mkoa ulivyoelekzwa,hata hivyo hawakushiriki zoezi hali iliyopelekea makarani kuzunguka wenyewe.

Katibu tawala mkoa wa Mara Clement Lujaji akizungumzia suala la malipo ya wenyeviti wa vitongoji alisema waraka ulisambazwa kwa waratibu wote kutokana na kuwa hawakuwemo kwenye mchakato na kuwa halmashauri zilikuwa na nafasi ya kuwalipa zaidi ya hapo kulingana na mapato yao.

Blogu hii imebaini kuwa baadhi ya makarani hawakuweza kuendelea na zoezi la sensa licha ya kuongeza siku kwa kile kinachodaiwa kuwa maelekezo hayo hayafafanuliwi jinsi watakavyolipwa.

Na kuwa walilipwa nusu ya posho na hawajalipwa nusu iliyosalia ,hata madodoso  hata waliokamilisja hawajakabidhi kwa kuwa hawajalipwa,na wanahofu kukabidhi bila kulipwa fedha zao hali .

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment