Subscribe:

Ads 468x60px

wanaharakati watakiwa kuandamana kupinga mauaji ya wananchi mgodi wa nyamongo


WANAHARAKATI WATAKIWA KUANDAMANA KUPINGA MAUAJI NYAMONGO.
Na Anthony Mayunga-Nyamongo.
Septemba 11,2012.

SIKU moja tu baada ya polisi kujeruhi watu 6 kwa mabomu ya machozi wakiwa majumbani kwaoWanaharakati na mashirika ya  kiraia wilayani Tarime wameombwa  kufanya maandamano ya hiari kupinga mauaji na vitendo vya kikatili vinavyofanywa na askari polisi wanaolinda mgodi wa African Barrick Gold North Mara.

Wito huo wakati waandishi wa habari hapa Tanzania wakiandamana kimya kimya kulaani mauaji ya kikatili ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Channel ten mjini Iringa katika kijiji cha Nyololo na raia wasiokuwa na hatia yanayofanywa na polisi.

Mtafiti kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC)Onesmo Ole ngurumwa akiongea na gazeti hili alisema zaidi ya watu 30 wameuawa na jeshi la polisi katika mgodi wa African Barrick North Mara kwa kipindi cha kuanzia 2009-sasa.

“Matukio hayakomi kila wakati wananchi wanauawa ,inabidi wanaharakati na mashirika ya kiraia mkoani Mara kuunganisha nguvu na kufanya maandamano ya amani ili kupinga mauaji na ukatili wanaofanyiwa wananchi hao ambao hawajawekewa mazingira mazuri”alisema.

Ole ngurumwa ambaye ni mfuatiliaji wa karibu wa mauaji yanayotokea Nyamongo alisema kwa kipindi cha mwaka 2009 watu 21waliuliwa  na polisi ama na walinzi wa mgodi huo.


Na kuwa mauaji yanaongezeka kila mwaka hivyo inatakiwa wanaharakati na mashirika ya kiraia kujitokeza ili kupinga ukatili huo.

“Kabla hawajauza ama kukodisha mgodi huo vitendo hivyo vinatakiwa kukomeshwa kwa kuwa ikiachwa watawarithisha wawekezaji wengine,tulaani vitendo hivyo”alisema.

Akizungumzia ulipuaji wa mabomu hadi kwenye makazi ya watu alisema ni utendaji mbovu wa jeshi hilo kwa kuwa hali hiyo ikiachwa iendelee madhara yanazidi kuwa makubwa.

Alibainisha kuwa serikali ni chanzo kwa kuwa imeunda vikundi vya wachimbaji wadogo lakini hawakuwahi kusaidiwa zaidi ya kuahidiwa kila kukicha.

Ushirika wa wachimbaji walia na ahadi hewa.
Mwenyekiti wa Ushirika wa wachimbaji wadogo Tarime Daud Makona alisema licha ya kusajiri ushirika wao mwaka 2010 hawajawahi kupata msaada wowote toka wizara ya Nishati na madini.

“Mauaji yanayoendelea Nyamongo yana mkono wa serikali,maana kama wangekuwa wametuwezesha wachimbaji o kusababisha vifo,naibu waziri Masele alikuja akaahidi,Waziri Profesa Sospeter Muhongo ameelezwa,hakuna kitu”alisema kwa uchungu.

Wakati analalamika serikali kutowasaidia Waziri Mkuu Mizengo Pinda ziarani Geita katika mgodi wa Mugusu alihimiza uundaji wa ushirika wa wachimbaji wadogo kuwa watasaidiwa na serikali.

Mtandao wa mashirika kukutana kutoa tamko.
Mratibu wa mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali Tarime(Tangonet)Bonny Matto alisema wanakutana kesho(leo)na moja ya agenda ni kutoa tamko juu ya mauaji na ukatili unaoendelea wilayani hapo.

Wakati huo huo habari zinadai kuwa majeruhi wa mabomu yanayodaiwa kurushwa na polisi wakati wanawafukuza vijana wanaodaiwa kuvamia kifusi hali zao zinaendelea vizuri.

Mwisho.



0 comments:

Post a Comment