Subscribe:

Ads 468x60px

ukosefu wa maji safi na salama kwa wakazi wa nyamongo wananchi walia na serikali na mgodi



UKOSEFU WA MAJI NYAMONGO WANANCHI WAZIDI KUIKABA KOO HALMASHAURI.
Na Anthony Mayunga-Nyamongo.
Septemba 6,2012.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tarime na Kampuni ya African Barrick North Mara wameendelea kulaumiwa na wananchi kwa kushindwa kutatua tatizo la maji safi na salama kwa wakazi wa Nyamongo.

Mapema wiki hii gazeti hili lilifanya uchunguzi katika vijiji vinavyozunguka mgodi huo ili kubaini  wa utekelezaji wa ahadi za serikali kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka mgodi huo baada ya chanzo cha mto Tighite kuharibiwa na sumu toka mgodi wa Gokona unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick North Mara.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kewanja Tanzania O’mtima ameliambia blogu  hii kuwa tatizo la maji safi na salama ni kubwa kwa wakazi wa kijiji chake kwa kuwa serikali imeshindwa kutimiza ahadi zake kwa wakati.

“Visima vimechimbwa na kutelekezwa havitoi maji,badala yake kampuni inatum,ia gari kusambaza maji ambayo serikali haijawahi kutuambia kama wameyapima na kubaini ni safi na salama ,kwa kuwa kampuni inadai yanatoka mgodini”alisema.

Alisema baadhi ya maeneo magari hayafiki kutokana na ubovu wa barabara hivyo wananchi wanapata shida kubwa kupata maji “hakuna nafuu yoyote maana tungekuwa na maji ya bomba tungesema limetatuliwa si kama ilivyo kwa kuletewa na gari maeneo mengine halifiki”alisema O’Mtima.

Alikwenda mbali na kudai kuwa viongozi wa serikali wamebaki kuzungumzia kwenye majukwaa wakati hakuna utekelezaji wowote ya maagizo ya toka mwaka 2009.

Hata alibainisha kuwa wamefunga mkataba na mgodi kuhakikisha kila mwaka wanawachimbia visima virefu viwili na wameanza mwaka huu ambapo yeye katika kitongoji cha Magina ambacho kina hali mbaya zaidi wamechimbiwa visima viwili.
Afisa maji.
Afisa maji wilaya ya Tarime Madaraka Mahando alikiri halmashauri kuchimba visima lakini havijatumika kwa kukosa maji huku akirusha lawama kwa jamii kuwa iliviharibu kabla ya kutumika.

“Kuna tatizo la kisiasa maana wananchi baadhi ya maeneo walikata  na kudumbukiza udongo,taarifa zipo mpaka wizarani,na Mkurugenzi baada ya kuwa umefuatilia amesema akitoka safari naye anataka tuzunguke naye kubaini vingapi havifanyi kazi”alisema.

Alivitaja visima walivyochimba kuwa ni vinne “vile vya Task Force kama serikali ilivyoelekeza tumechimba Matongo viwili,Kewanja 1 na Nyakunguru kitongoji cha Itandura kimoja lakini baadhi havifanyi kazi”alisema.

Hata hivyo alishindwa kuthibitisha kama maji yanayosambazwa kwa gari na kampuni ni safi na salama na yamepimwa na mamlaka gani.

Kampuni.
Mmoja wa maafisa katika mgodi wa North Mara upande wa maji Saimoni Shayo alikiri kusambaza maji kwa gari kutokana na kuwa maeneo mengi hayana maji kwa kuwa hakuna visima.

“Tunawasambazia maji ambayo tunatumia sisi ,wakati wa usiku kwa kuwa hatuyatumii ndipo tunachota kuwapelekea hata hivyo hayatoshi ,tuna mpango wa kuchimba visima viwili viwili kila kijiji kwa kila mwaka”alisema.

Alidai kuwa mpango mwingine ni kutandaza mabomba ambao unategemea kukamilika mwaka 2014,kuhusu visima vingi kutokuwa na maji “si kwamba kote hakuna maji kwingine kuna madini tembo ambayo hayafai kwa matumizi hiyo ni kitaalam si kwamba mgodi ndio umeharibu”alisema.

Hata hivyo alipingana na halmashauri na kauli za serikali kutoa maagizo kwa kampuni kuhakikisha wanawapatia vyanzo mbadala vya maji baada yamto Tighite kuchafuliwa na sumu kutoka mgodini kwa madai kuwa hawana waraka wowote wa serikali wa kuwataka kufanya hivyo.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment