Subscribe:

Ads 468x60px

mwanafunzi atuhumiwa kwa kuua kwa mshare

MWANAFUNZI WA SEKONDARI ATUHUMIWA KUUA KWA MSHARE,
Na Anthony Mayunga-Serengeti.
Oktoba 27,2012.


MWANAFUNZI wa kidato cha tatu katika sekondari ya Busawe kata ya Majimoto wilayani Serengeti mkoani Mara Peter Lucas Wambura(17)anasakwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga mshare kifuani Chacha Damiani Mangali(18) na kufa papo hapo.

Tukio hilo linalodaiwa kutokea oktoba 26,majira ya saa 2 mwaka huu  usiku nyumbani kwa marehemu Mangali limethibitishwa na uongozi wa kitongoji na polisi linahusishwa na wivu wa kimapenzi.

Mwenyekiti wa kitongoji hicho Daud Mgendi aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa mtuhumiwa huyo ambaye ni jilani yake na marehemu alimpiga mshare kifuani na kufa papo hapo wakati anafungua mlango atoke nje ya nyumba yake.

“Sababu hazijajulikana kuwa ni vijana waliokuwa wanalingana huenda wamegongana kwa wanawake ,maana inaonekana marehemu alifungua mlango akidhani ni mambo ya kawaida ndipo akapigwa mshare kifuani na kupiga kelele kisha akakata roho”alisema Mwenyekiti.

Alisema mara baada ya kutenda unyama huo mtuhumiwa aligeuka kama kichaa na kitishia usalama wa wananchi kwa kuwa alikuwa na upinde na mishare mingi ,na kutokana na giza walishindwa kumdhibiti na kutokomea kusiko julikana.

“Kumdhibiti ilikuwa vigumu kwa kuwa alionekana kuwa kama kichaa na kutishia watu kwa kurusha mishare ovyo na kutokana na giza kila mtu aliamua kuchukua tahadhari kwa kuwa hakuwa katika hali ya kawaida”alisema.

Baba mzazi wa marehemu Damiani Mangali akiongea na gazeti hili kwa njia ya simu alisema kuwa kijana wake alikuwa hajaoa na wanahisi huenda wamegongana kwa wanawake kwa kuwa hakuna madai mengine ambayo ameyasikia.

“Kama ingekuwa deni tungesikia lakini kwa matatizo ya wanawake mara nyingi huwa siri zao maana wote walikuwa vijana na majilani,nilipigiwa simu na kaka yake na marehemu kuhusiana na tukio hilo,tunaendelea kufuatilia chanzo lakini inauma kifo cha ghafla namna hii bila hata kuwaeleza sababu”alisema.

Polisi wilayani hapa waanaendelea na uchunguzi ikiwa ni pamoja na kumsaka mtuhumiwa ,ambapo wameomba wananchi watoe ushirikiano wa chanzo na alikojificha kwa kuwa anaweza kusababisha madhara makubwa zaidi.

Hivi karibuni mwanafunzi mmoja wa  kidato cha pili Mugumu  sekondari  wilayani wilayani hapa  Mwang’omba Kegocha(16)amefikishwa katika mahakama ya wilaya  kwa tuhuma ya kumchoma kisu Chacha Pasta(29)

Tukio ambalo linadaiwa lilitokea wakati wanacheza kamali ambapo mtuhumiwa inadaiwa alikuwa ana mdai marehemu  ths 5,000  na katika kudaiana wakakorishana ndipo akamchoma kisu ubavuni na kufa papo hapo.



Mwisho.



0 comments:

Post a Comment