Subscribe:

Ads 468x60px

Kilimo kwanza


KIKUNDI CHA VICOBA CHAPATA MKOPO WA TREKTA,
Na Anthony Mayunga-Serengeti
3,0ktoba 2012.

KIKUNDI cha Jipe Moyo (VICOBA)kijiji cha Nyambureti kata ya Nyambureti wilayani Serengeti kinatarajia kulima ekari 30 za mpunga baada ya kupata mkopo wa trekta kutoka Suma JKT lenye thamani ya tsh,mil.21.9

Kikundi hicho ni kwanza kati ya vikundi vya Vicoba zaidi ya 80 vilivyopo wilayani hapo kupata mkopo wa treka ambao wataulipa kwa kipindi cha miaka minne.

Mbele ya Mbunge wa jimbo hilo Dk,Stephen Kebwe katibu wa kikundi hicho---- alisema wanategemea kulima ekari hizo za mpunga kama mradi wa kikundi lakini kwa mwanachama mmoja mmoja watamlimia ekari moja kwa gharama nafuu .

Alisema watawalimia na wananchi wengine kwa kulipia ili waweze kulipa mkopo huo ambao wanaamini wataweza kwa kuwa malengo yao kwa kuwa kikundi hicho kiongeza uzalishaji ili kuongeza mapato ya kikundi na wanakikundi wenyewe.

“Kama kikundi tumechangia tsh,mil.6.9 ili kupata kikundi ambazo zimetokana na kununua hisa wenyewe,faini na faida inayotokana na mikopo ya wanachama kwenye mifuko yetu ya asilimia 10 kwa tsh,100,000=”alisema.

Alisema licha ya kuwa kikundi kina miaka miwili wanachama wameweza kunufaika kwa kukopa kwa ajili ya biashara zao,hatua ambayo inaonyesha mafanikio kwa kuwa lengo ni kuhakikisha wananufaika kiuchumi.

Kuhusu malengo ya baadae ni kuwa mawakala wa kuuza pembejeo katika eneo hilo ili kuwarahisishia wananchi kupata kuzipata haraka tofauti na sasa wanalazimika kwenda wilayani zaidi ya kilometa 50.

Akizungumzia Changamoto zinazowakabili alisema mtaji mdogo,trekta kutokuwa na tela ambalo lingewasaidia kusomba mizigo mbalimbali ikiwemo mbolea kupeleka shambani na kumwomba Mbunge awasaidie kututua changamoto hiyo.

Naye Katakata Sangi mmoja wa wanachama alibainisha kunufaika kwa mikopo kwenye kikundi ambao umekuza mtaji wake kutoka 200,000 alizokuwa nazo sasa amefikisha tsh,mil.1 kwa kuuza soda na dizeli na anasomesha watoto wawili sekondari  kupitia mfuko wa elimu wa kikundi.

Kwa upande wake mbunge Dk,Kebwe aliwataka walitunze vizuri ili liweze kuwanufaisha kiuchumi,kwa kuwa watakuwa wameachana na kilimo cha mkono na hivyo wataongeza uzalishaji.


Kikundi hicho cha Vicoba kilianzishwa juni 27,2010 kikiwa na wanachama 30 kati yao wanaume wakiwa 18 na wanawake 12.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment