Subscribe:

Ads 468x60px

jina serengeti laibua mvutano


Mbunge wa jimbo la Serengeti Dk,Stephen Kebwe ameapa kuonana na waziri wa miundo mbinu ili kumaliza utata ambao umeanza kujitokeza wa jiji la Mwanza kutaka kubadili jina la uwanja wa ndege kuitwa Serengeti wakati tayari Serengeti wameishapata kibali cha kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa wa serengeti


MABADILIKO YA JINA LA UWANJA WA NDEGE MWANZA ,WAKUU WA MIKOA WATOA KAULI TOFAUTI.
Na Anthony Mayunga-Mara
Oktoba 4,2012.

SAKATA la Serengeti kutumika  kama jina jipya la uwanja wa  ndege wa kimataifa  Mwanza wa wakuu wa mikoa  watoa kauli tofauti ,  mkuu wa mkoa wa Mara adai wanajadiliana vizuri  wa Mwanza akisisitiza kuwa mchakato uko idara ya uchukuzi.

Hivi karibuni Mbunge wa jimbo la Serengeti Dk,Stephen Kebwe akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mjadala unaoendelea Mwanza kutaka kutumia jina hilo aliwataka Mwanza watafute jina jingine.

Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tupa akiongea na Mwananchi kuhusiana na sakata hilo alikiri kuwa mjadala huo upo na wanaendelea kujadiliana na mkuu wa mkoa wa Mwanza na watapata muafaka.

“Hilo linazungumzika mimi na mwenzangu mkuu wa mkoa wa Mwanza tunaendelea kujadiliana naamini tutapata muafaka,maana hili halitashindikana tutapata muafaka mzuri na hata ngazi za juu zipo zitatoa ushauri”alisema.

Alisema kuwa na viwanja vingi itasaidia kupata wageni wengi ,hivyo mjadala huo wanalenga kuumaliza vizuri kwa majadiliano ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda vizuri na kuahidi kuwa taarifa itatolewa .

Wakati Mkuu wa Mkoa wa Mara akidai wako kwenye majadiliano mazuri Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndukilo alipoulizwa na Mwananchi mjadala huo unaendeleaje na hatima yake alisema suala hilo litatolewa taarifa.

“Nasema mtajulishwa na wala si sasa maana mchakato wake umeishapelekwa wizara ya uchukuzi kama mnataka taarifa fuatilieni huko “alisema kwa mkato.

Wakati majibu yakitofautiana ya wakuu wa mikoa mbunge wa jimbo la Serengeti dk,Kebwe amesisitiza kuwa msimamo wake wa kuwataka waache kutumia jina hilo kwa kuwa tayari wameishapata kibali cha ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Serengeti ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete kwa wakazi wa wilaya na Taifa ilimkurahisishia wageni kufika hifadhini kwa urahisi.

Pia amesema  anakwenda kuonana  na watendaji wa wizara ya mambo ya anga ili kumaliza mvutano huo ambao hauna maslahi kwa taifa kwa kuwa Mwanza wangeweza kukuza hifadhi za Saanane na Lubondo kwa kuita uwanja huo.

Aliuchukulia mjadala huo unaendeshwa Mwanza kufifisha juhudi za watu ambao wameishajitokeza kujenga uwanja huo kama Kampuni ya Singita Grumeti Reserves kupitia kwa mmiliki wake Paul John Tudor raia wa Marekani.

Uwanja wa ndege wa Kimataifa Serengeti unajengwa kwa ubia wa kampuni ya Grumeti reserves,halmashauri na Serikali kuu,tayari wana hati ya ekari 5,000 na wananchi wameishalipwa fidia ikiwemo kuhamishwa kwa shule ya Msingi Burunga na kujengwa maeneo mengine.

Rais Kikwete katika kampeini zake na mikiutano mingine ikiwemo hotuba za mwisho wa mwezi amekuwa akizungumzia dhamira ya kujenga uwanja huo Mugumu lengo likiwa ni kuwawezesha wageni kutua hapo na kuingia hifadhi ya Taifa ya Serengeti na mapori ya akiba kwa madai kuwa wanapotelemkia Kilimanjaro ama Mwanza wanasafiri umbali mrefu na hayo ni malalamiko yao.

Kujengwa uwanja huo kutafungua milango ya kiuchumi kwa jamii na taifa kwa kuwa kutakuwa na ongezeko la wageni wengi ambao walikuwa hawapendi kufika hifadhi hiyo kutokana na umbali na ubovu wa miundo mbinu ya barabara.

Hivi karibuni katika wiki ya tamasha la utalii mkoani Mwanza hoja ya kutaka jina hilo litumike kwa ajili ya uwanja wa ndege wa Mwanza ambao unakarabatiwa kwa lengo la kuwa wageni wataongezeka iliibuka na kuzua mjadala kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment