Subscribe:

Ads 468x60px

Bomba lililokuwa likitiririsha maji machafu yaliyochanganyika na kinyesi lakarabatiwa





BOMBA LILILOKUWA LIKITIRIRISHA MAJI MACHAFU YALIYOCHANGANYIKA NA KINYESI LAZIBWA.
Na Anthony Mayunga-Serengeti
Novemba 19,2012.

HATIMAYE mamlaka ya mji mdogo wa Mugumu wilayani Serengeti umeziba bomba lililokuwa likitiririsha maji machafu yaliyochanganyika na kinyesi kwenda kwenye makazi wa watu na sehemu za biashara mtaa wa sedeko.

Uzibaji wa bomba hilo umekuja siku chache tu baada ya gazeti la Mwananchi kuripoti tukio hilo ambalo limepigiwa kelele ikiwa ni pamoja na kuwasilishwa katika vikao vya baraza la madiwani bila ufumbuzi.

Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Sedeco waliliambia gazeti hili kuwa siku moja baada ya taarifa kutolewa hukuikionyesha picha ya tatizo hatua ilichukuliwa haraka .

“Tunawashukuru sana waandishi wa habari maana tumeumia sana kwa muda mrefu,mbunge amekuja mara mbili kapuuzwa ,baraza la madiwani lilidanganywa lakini mmekuja hapa na kuandika na hatua zikachukuliwa huku wakilaumu kwa nini tunawaambia waandishi,watendaji hawa hawafai mpaka wasukumwe”alisema mmoja akina mama ntilie eneo hilo jina limehifadhiwa.

Hata hivyo wakazi wa mtaa huo na wafanyabiashara walimtupia lawama afisa afya wa mamlaka hiyo kuwa utendaji kazi wake ni mbaya kwa kuwa wanapompelekea malalamiko anawajibu vibaya.

“Hatujui nafasi hizi wanazipataje maana ofisa afya wa mamlaka hii hafai bomba liko mita kumi toka ofisi yake ,tunamweleza anatujibu kuwa ,harufu hiyo inawapunguzia bajeti ya kula kwa kuwa matumbo yatashida yamejaa,tutegemee nini kwa mtumishi kama huyo analipwa kwa kazi gani”alihoji Phinias Edward mfanyabiashara wa chakula eneo hilo.

Hata hivyo alipotafutwa kwa njia ya simu afisa afya huyo Chironge Hamisi kutaka kujua utekelezaji wa kazi hiyo na malalamiko ya wananchi aling’aka.
“Wewe walikuletea malalamiko ili tutengeneze hilo bomba,kwanza wewe unaniuliza hayo wewe ni mkuu wangu wa kazi,mbona unaniuliza uliza haya mambo unataka nini,wewe nini bwana”alijibu kwa ukali na kukata simu.

Hata hivyo ofisa mtendaji wa mamlaka hiyo Gidioni Obel alidai kuwa matatizo yote hayo yanashughulikiwa kwa awamu na kuwa suala la bomba wamemaliza ,lakini ukarabati wa choo ikiwa ni pamoja na kuweka mifumo ya maji kwa kuwa ilijengwa vibaya inahitaji bajeti kubwa na wakipata fedha wataitekeleza.

Malalamiko ya wananchi wakiwemo wafanyabiashara ndani ya soko yalikuwa ni utiririshaji wa maji machafu yaliyochanganyika na kinyesi kwenye maeneo yao,huku baadhi ya wafanyabiashara wakilalamikia harufu mbaya inayotokana na choo  hicho kutokuwa na mfumo wa kutolea hewa na maji .

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment