Subscribe:

Ads 468x60px

polisi Nyamongo wadaiwa kuua kwa risasi



POLISI NYAMONGO WADAIWA KUUA KWA RISASI
Na Anthony Mayunga-Mara
Novemba 6,2012.

ASKARI polisi wa mkoa wa kipolisi Tarime na Rorya wanadaiwa kumuua mkazi mmoja wa kitongoji cha Nyabegena kijiji cha Kewanja wilayani Tarime kwa kumpiga risasi baada ya kutokoea vurugu wakati wanawatawanya wananchi waliokuwa wamepata mchanga unaodaiwa kuwa na dhahabu.

Tukio hilo linadaiwa kutokea novemba 6 majira ya saa 9.10 arasili mwaka huu  katika eneo la Nyabegena kuliko na mgodi  Gokona wa kampuni ya African Barrick North Mara .

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Tanzania O’mtima amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kumtaja aliyeuawa kuwa ni Kibwabwa Ghati Marembera mwenye umri katii ya miaka 22-25 mkazi wa kijiji hicho ambaye alipigwa risasi na kufumua fuvu la kichwa na ubongo kumwagika.

“Ni kweli amekufa mimi nilikuwa kwenye kikao ofisini sikuwepo eneo la tukio sijajua ilivyokuwa,…lakini  kuna taarifa kuwa watu walikuwa wanataka kuingia mgodini kuchukua mawe ya dhahabu…risasi zimepigwa nyingi sana na eneo hilo ni karibu na makazi ya watu”alisema.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio akiongea na Mwananchi kwa njia ya simu anasema kuwa polisi walikuta wananchi wana mawe yanayodaiwa kuwa ya dhahabu waliyoyapata kwenye vifusi na kutaka kuwanyanganya ndipo vurugu zikaanza.

“Polisi wamezoea kuwanyanganya wananchi mawe ya dhahabu na kujimilikisha,yalifika magari kama matano ya polisi na kuanza kuwazingira kwa lengo la kuwapora ndipo vurugu zikaanza,wananchi wakipinga ,wamepiga risasi nyingi sana ndipo wakawapiga risasi watu wawili mmoja ni Marembera aliyekufa hapo hapo na mwingine hatujajua jina lake amepigwa ubavuni”alisema shuhuda.

Na kuwa baada ya kuwa wamewapiga risasi vurugu zimeendelea huku polisi wakitaka kuchukua mwili wake waondoke nao lakini wamezidiwa na wananchi na kufanikiwa kuchukua majeruhi mmoja na kukimbia kwenda Tarime.

“Polisi wamezidiwa na wananchi wakashindwa kuchukua mwili wa marehemu kuondoka nao,lakini majeruhi ambaye hajafahamika wamemchukua ,kwa hali aliyokuwa nayo sidhani kama atapona”anasema.

Alibainisha kuwa mwili wa marehemu huyo umepelekwa kituo cha afya cha Nyangoto maarufu kama sungusungu kwa ajili ya kuhifadhiwa na uchunguzi zaidi.

Mmoja wa waganga katika kituo hicho cha afya aliyefahamika kwa jina moja la Kenedy alipoulizwa na Mwananchi kwa njia ya simu kama wamepokea mwili wa Marembera ama kuwepo majeruhi wengine alidai kuwa yeye alitoka kazini mapema hivyo hajui.

Hata hivyo alipoulizwa kama tukio limetokea kabla ya muda wa kazi haujasha imekuwaje atoke muda mrefu na hakurudi kazini ,alidai,”mimi nakwambia nimetoka muda mrefu sijui na wala sijui nani yupo zamu”alijibu.

Kamanda wa polisi wa mkoa huo wa kipolisi Justus Kamugisha alipoulizwa kwa njia ya simu alidai,” taarifa nilizopata ni kwamba kuna vurugu zimetokea za watu kuvamia mgodi na mmoja nasikia ameumizwa haijulikani yuko wapi,nafuatilia habari kamili nitatoa baadae”alisema.

Huo ni mwendelezo wa matukio ya askari polisi wa kanda hiyo kuua raia katika mgodi huo ,inadaiwa sababu kubwa ni serikali kutokutenga maeneo ya wachimbaji wadogo wadogo.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment