Subscribe:

Ads 468x60px

watakaokeketa watoto wa kike kukiona


VIONGOZI WA SERIKALI WAKUNJUA MAKUCHA KWA WATAKAOKEKETA WATOTO WA KIKE.
Na Anthony Mayunga-Serengeti
Novemba 7,2012.

VIONGOZI wa serikali  mkoani Mara wamevun ja kimya na kutoa  onyo kwa wananchi watakaojihusisha na shughuli za kukeketa watoto wa kike kuwa  watashughulikiwa kwa kuwa ni uvunjaji wa sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 na makosa ya kujaamiina ya mwaka 1998.

Hatua hiyo inakuja huku tayari maandalizi ya ukeketaji watoto wa kike katika wilaya mbalimbali mkoani Mara yakipamba moto kutoka kwa wazazi na walezi.

Mkuu wa mkoa wa Mara John Tupa akiongea na Mwananchi kwa njia ya simu amesema viongozi wa ngazi zote wameishaelezwa mikakati ya kukabiliana na wale watakaokaidi.

“Ukeketaji ni ukiukwaji wa sheria kama serikali tunatambua mwaka huu watafanya hivyo,kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo viongozi wa dini zote,watendaji wa ngazi zote na wazee wa mila lengo ni kuhakikisha wanakomesha ukatili huo”alisema.

Alikwenda mbali zaidi na kudai hata ngariba wameishaambiwa kuachana na kazi hiyo inayokiuka sheria za nchi”hatutasita kuwakamata wataokiuka kwa kuwa ni makosa ,naomba kila mmoja atimize wajibu wake”alisema mkuu wa mkoa.

Kuhusu viongozi wa kisiasa hasa wa kuchaguliwa kuogopa kuwakemea wananchi kwa hofu ya kupoteza kura alisema mkakati wa sasa ni kuhakikisha wanahusika kwa kuwa kila kiongozi anatakiwa kuwa mlinzi wa sheria za nchi.

Aliwataka wanaharakati mbalimbali wanaojihusisha na utoaji wa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia hususan ukeketaji wa watoto wa kike washirikiane na serikali.

Rpc kanda maalum.
Kamanda wa mkoa wa kipolisi Tarime na Rorya Justus Kamugisha alipoulizwa mikakati waliyonayo kukabiliana na watakaohusika alisema ,suala hilo wanalichukulia kama ilivyo kwa makosa mengine ya jinai.

“Ukeketaji ni kosa la jinai tutawakabili wahusika kama ilivyo kwa makosa ya jinai,maana kama ni elimu wameambiwa sana kuhusu madhara ya ukeketaji wanatakiwa kuepuka kujihusisha na matukio hayo ili kuepuka mikono ya serikali”alisema.

Hata hivyo alisema sekta ya maendeleo ya jamii inatakiwa kujipanua zaidi ili kuweza kuwafikia wananchi waachane na uvunjaji wa sheria .

Mratibu wa mradi wa Childrens Dignity Forum (Cdf) Joram Wimmo alisema katika utafiti wao walibaini kwa mwaka huu watoto zaidi ya 4,000 wako hatarini kukeketwa kwa wilaya moja tu ya Tarime.

Hatua ambayo anaona kuwa inahitaji ushirikiano mkubwa na wadau mbalimbali kwa kuwa wilaya zingine za Serengeti,Rorya,Bunda,Butiama na Musoma kuna jamii hizo zinazohusika na ukeketaji,hivyo idadi huenda ikawa kubwa zaidi.

Kutokana na tafiti hizo kwa sasa wamejikita kutoa elimu kwa jamii hasa ya koo 5 za Kikurya kwa kuwashirikisha wazee wa mila ili watambue madhara na waweze kuachana na kazi hiyo.

Hata hivyo imebainika kuwa baadhi ya wazazi waishio mpakani mwa Tanzania na Kenya kupeleka watoto huko kwa ajili ya kukeketwa na watarudi baada ya kupona.

Mwaka 2010 licha ya serikali kupiga marufuku lakini ukeketaji wa watoto wa kike uliendelea kwa kuambatana na sherehe za kifahali huku watoto waliokeketwa wakipitishwa mbele za ofisi za serikali ikiwemo polisi bila kuchukuliwa hatua.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment